Sourate: ATTUR 

Verset : 1

وَٱلطُّورِ

Nina apa kwa mlima wa Tur



Sourate: ATTUR 

Verset : 2

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa kitabu kilichoandikwa



Sourate: ATTUR 

Verset : 3

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika karatasi ya ngozi nyembamba iliyokunjuliwa



Sourate: ATTUR 

Verset : 4

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na (nina apa) kwa Nyumba iliyoimarishwa (iliyojengwa imara)



Sourate: ATTUR 

Verset : 5

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na (nina apa) kwa sakafu (za mbingu) zilizonyanyuliwa



Sourate: ATTUR 

Verset : 6

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na (nina apa) kwa bahari yenye kuwashwa moto)



Sourate: ATTUR 

Verset : 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

(Nina apa kwamba) Hakika, adhabu ya Mola wako Mlezi bila ya shaka yoyote itatokea



Sourate: ATTUR 

Verset : 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia



Sourate: ATTUR 

Verset : 9

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku hiyo mbingu itatikisika kutikisika kikweli



Sourate: ATTUR 

Verset : 10

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na majabali yatatembea mwendo wa kasi



Sourate: ATTUR 

Verset : 11

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao Siku hiyo kwa wakadhibishao



Sourate: ATTUR 

Verset : 12

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wamo katika kushughulika na upuuzi wakicheza



Sourate: ATTUR 

Verset : 13

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watasukumwa katika Moto wa Jahannam kwa msukumo wa nguvu



Sourate: ATTUR 

Verset : 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Huu ndio ule moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha



Sourate: ATTUR 

Verset : 15

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, hivi ni uchawi huu au nyinyi hamuoni?



Sourate: ATTUR 

Verset : 16

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Ingieni muungue humo kwenye Jahannam, mkistahamili au msistahamili ni sawasawa kwenu, hakika hapana ila mnalipwa yale mliyokuwa mkiyatenda



Sourate: ATTUR 

Verset : 17

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema



Sourate: ATTUR 

Verset : 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahia kwa ambayo Amewapa Mola wao, na Akawaokoa na adhabu ya moto uwakao vikali mno



Sourate: ATTUR 

Verset : 19

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kwa sababu ya mliyokuwa mnatenda



Sourate: ATTUR 

Verset : 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hali ya kuegemea juu ya makochi ya fakhari yaliyopangwa safu safu, na Tutawaozesha huwr ‘ayn, (wanawake weupe) wazuri wenye macho makubwa ya kupendeza



Sourate: ATTUR 

Verset : 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na wakafuatwa na dhuriya wao kwa Imani Tutawakutanisha nao dhuriya wao na Hatutawapunguzia katika ‘amali zao kitu chochote. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma



Sourate: ATTUR 

Verset : 22

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na Tutawapa matunda na nyama katika ambavyo wanatamani



Sourate: ATTUR 

Verset : 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watabadilishana humo gilasi za mvinyo usiosababisha maneno ya upuuzi na wala ya dhambi



Sourate: ATTUR 

Verset : 24

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Na watawazungukia watumishi vijana kwa ajili yao kana kwamba ni lulu zilizohifadhiwa



Sourate: ATTUR 

Verset : 25

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengine wakiulizana



Sourate: ATTUR 

Verset : 26

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Watasema hakika sisi tulikua kabla ya hapa kwa watu wetu wenye kuwafanyia upole



Sourate: ATTUR 

Verset : 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Allah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya mvuke wa moto (unaobabua)



Sourate: ATTUR 

Verset : 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi tulikuwa tunamuabudu kabla ya hapa hakika yeye ni mwema mwingi wa rehma



Sourate: ATTUR 

Verset : 29

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha (Ewe Muhammad) na haukua wewe kwa neema ya mola wako mlezi kuhani wala mwendawazimu



Sourate: ATTUR 

Verset : 30

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema (huyu Muhammad þ ni) mshairi, tunamtarajia kupatikana maafa ya dahari