Sourate: QAAF 

Verset : 1

قٓۚ وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡمَجِيدِ

Qaaf. Nina apa kwa Qur’ani Tukufu



Sourate: QAAF 

Verset : 2

بَلۡ عَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٞ مِّنۡهُمۡ فَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا شَيۡءٌ عَجِيبٌ

Bali wamestaajabu kwamba amewajia muonyaji miongoni mwao, na kwa sababu hiyo makafiri wakasema: “Hili ni jambo la ajabu sana!



Sourate: QAAF 

Verset : 3

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗاۖ ذَٰلِكَ رَجۡعُۢ بَعِيدٞ

Je, hivi tukifa na tukawa udongo (tutafufuliwa)? Kurejea huko kuko mbali sana”



Sourate: QAAF 

Verset : 4

قَدۡ عَلِمۡنَا مَا تَنقُصُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۡهُمۡۖ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظُۢ

Hakika, sisi tumejua kila ambacho ardhi inakipunguza kwao[1] na tunacho Kitabu kinachohifadhi barabara


1- - Kinachokusudiwa hap ani kwamba, kwa Allah hakipotei kitu. Pamoja na kwamba, makafifiri katika Aya iliyopita kabla ya hii wanaona kwamba wakifa na kuzikwa miili yao inaoza ardhini na kwamba si jambo linalowezekana kurejea tena kwenye hali yao ya zamani, Allah anasema hilo kwake ni jepesi na hakuna kitakachopotea.


Sourate: QAAF 

Verset : 5

بَلۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَهُمۡ فِيٓ أَمۡرٖ مَّرِيجٍ

Bali wameikadhibisha (wamei-pinga) haki ilipowajia. Basi wao wamo katika jambo la mkorogeko



Sourate: QAAF 

Verset : 6

أَفَلَمۡ يَنظُرُوٓاْ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوۡقَهُمۡ كَيۡفَ بَنَيۡنَٰهَا وَزَيَّنَّـٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٖ

Je, hawatazami mbingu juu yao, vipi Tumezijenga na Tumezipamba, na wala hazina mipasuko yoyote



Sourate: QAAF 

Verset : 7

وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجِۭ بَهِيجٖ

Na ardhi Tumeitandaza na Tukaiwekea milima thabiti, na Tukaotesha humo kila aina ya mimea ya kupendeza



Sourate: QAAF 

Verset : 8

تَبۡصِرَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِكُلِّ عَبۡدٖ مُّنِيبٖ

Ni ufumbuzi wa macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea kwa Allah



Sourate: QAAF 

Verset : 9

وَنَزَّلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ مُّبَٰرَكٗا فَأَنۢبَتۡنَا بِهِۦ جَنَّـٰتٖ وَحَبَّ ٱلۡحَصِيدِ

Na Tukateremsha kutoka mbinguni maji yaliyobarikiwa, kisha Tukaotesha kwayo mabustani na nafaka za kuvunwa



Sourate: QAAF 

Verset : 10

وَٱلنَّخۡلَ بَاسِقَٰتٖ لَّهَا طَلۡعٞ نَّضِيدٞ

Na mitende mirefu yenye mashada (makole) ya matunda yenye kuzaa kwa wingi



Sourate: QAAF 

Verset : 11

رِّزۡقٗا لِّلۡعِبَادِۖ وَأَحۡيَيۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗاۚ كَذَٰلِكَ ٱلۡخُرُوجُ

Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na Tukahuisha kwayo nchi iliyokufa, kama hivyo ndivyo utakavyokuwa ufufuaji



Sourate: QAAF 

Verset : 12

كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ وَأَصۡحَٰبُ ٱلرَّسِّ وَثَمُودُ

Walikadhibisha kabla yao watu wa Nuhu na wakazi wa Ar-Rass na kina Thamud



Sourate: QAAF 

Verset : 13

وَعَادٞ وَفِرۡعَوۡنُ وَإِخۡوَٰنُ لُوطٖ

Na kina Aad na Firaun na ndugu wa Lutwi



Sourate: QAAF 

Verset : 14

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ وَقَوۡمُ تُبَّعٖۚ كُلّٞ كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ

Na wakaazi wa Machakani na watu wa Tubbaa, wote walikadhibisha Mitume. Basi onyo likathibitika juu yao



Sourate: QAAF 

Verset : 15

أَفَعَيِينَا بِٱلۡخَلۡقِ ٱلۡأَوَّلِۚ بَلۡ هُمۡ فِي لَبۡسٖ مِّنۡ خَلۡقٖ جَدِيدٖ

Je, kwani Tulichoka kwa uumbaji wa kwanza? Bali wao wamo katika shaka juu ya uumbaji upya (kufufuliwa)



Sourate: QAAF 

Verset : 16

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ وَنَعۡلَمُ مَا تُوَسۡوِسُ بِهِۦ نَفۡسُهُۥۖ وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ

Na kwa yakini Tumemuumba Mtu na Tunajua yale inayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake



Sourate: QAAF 

Verset : 17

إِذۡ يَتَلَقَّى ٱلۡمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٞ

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni



Sourate: QAAF 

Verset : 18

مَّا يَلۡفِظُ مِن قَوۡلٍ إِلَّا لَدَيۡهِ رَقِيبٌ عَتِيدٞ

Hatamki kauli yoyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi)



Sourate: QAAF 

Verset : 19

وَجَآءَتۡ سَكۡرَةُ ٱلۡمَوۡتِ بِٱلۡحَقِّۖ ذَٰلِكَ مَا كُنتَ مِنۡهُ تَحِيدُ

Na uchungu wa mauti (wa kutoka roho) utakapomjia kwa haki. (Itasemwa): Hayo ndiyo yale uliyokuwa ukiyakimbia



Sourate: QAAF 

Verset : 20

وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡوَعِيدِ

Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndio Siku ya miadi. (makamiano)



Sourate: QAAF 

Verset : 21

وَجَآءَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّعَهَا سَآئِقٞ وَشَهِيدٞ

Na kila nafsi itakuja pamoja nayo mcungaji na shahidi



Sourate: QAAF 

Verset : 22

لَّقَدۡ كُنتَ فِي غَفۡلَةٖ مِّنۡ هَٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٞ

(Aambiwe): Kwa yakini ulikuwa umeghafilika na haya! Basi Tumekuondoshea kifuniko chako (pazia lako), basi kuona kwako leo ni kukali



Sourate: QAAF 

Verset : 23

وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌ

Na Malaika wake aliyepewa jukumu atasema: Hii (rekodi) iliyoko kwangu imeshatayarishwa



Sourate: QAAF 

Verset : 24

أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٖ

(Allaah Atasema): Mtupeni katika Jahannam kila kafiri, mkaidi!



Sourate: QAAF 

Verset : 25

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٖ مُّرِيبٍ

Mzuiaji wa kheri, mwenye kuruka mipaka, mwenye kutia shaka



Sourate: QAAF 

Verset : 26

ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Ambaye amefanya mwabudiwa mwengine pamoja na Allah, basi mtupeni katika adhabu kali



Sourate: QAAF 

Verset : 27

۞قَالَ قَرِينُهُۥ رَبَّنَا مَآ أَطۡغَيۡتُهُۥ وَلَٰكِن كَانَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٖ

Shatani mwenzake atasema: Ee Mola wetu mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotofu wa mbali. (na haki)



Sourate: QAAF 

Verset : 28

قَالَ لَا تَخۡتَصِمُواْ لَدَيَّ وَقَدۡ قَدَّمۡتُ إِلَيۡكُم بِٱلۡوَعِيدِ

(Allah) Atasema: Msigombane mbele yangu, na hali Nilikuleteeni onyo Langu!



Sourate: QAAF 

Verset : 29

مَا يُبَدَّلُ ٱلۡقَوۡلُ لَدَيَّ وَمَآ أَنَا۠ بِظَلَّـٰمٖ لِّلۡعَبِيدِ

Haibadilishwi kauli Kwangu, Nami si mwenye kudhulumu waja wangu



Sourate: QAAF 

Verset : 30

يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٖ

Siku Tutakapoiambia Jahannam: Je, umeshajaa? Nayo itasema: Je, kuna ziada yoyote?