Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 70

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ

Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 71

قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

Wakasema: Tunaabudu masa-namu, daima tunayanyenyekea



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 72

قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ

Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 73

أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ

Au yanakufaeni, au yanaku-dhuruni?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 74

قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ

Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 75

قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 76

أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ

Nyinyi na baba zenu wa zamani?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 77

فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 78

ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ

Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 79

وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 80

وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ

Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 81

وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 82

وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 83

رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّـٰلِحِينَ

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 84

وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 85

وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 86

وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 87

وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ

Wala usinihizi (usinifedheheshe) Siku watapo fufuliwa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 88

يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ

Siku ambayo kwamba mali hayatofaa kitu wala watoto



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 89

إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ

Isipokuwa mwenye kumjia Allah na moyo safi



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 16

وَإِبۡرَٰهِيمَ إِذۡ قَالَ لِقَوۡمِهِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُۖ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na Ibrahim pale alipo waambia watu wake: Muabuduni Allah, na mcheni Yeye. Hiyo ndiyo kheri yenu, ikiwa nyinyi mnajua



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 17

إِنَّمَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا وَتَخۡلُقُونَ إِفۡكًاۚ إِنَّ ٱلَّذِينَ تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَمۡلِكُونَ لَكُمۡ رِزۡقٗا فَٱبۡتَغُواْ عِندَ ٱللَّهِ ٱلرِّزۡقَ وَٱعۡبُدُوهُ وَٱشۡكُرُواْ لَهُۥٓۖ إِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Hakika nyinyi mnaabudu masanamu badala ya Allah, na mnazua uzushi. Hakika hao mnao waabudu badala ya Allah hawakumilikiini riziki yoyote. Takeni riziki kwa Allah, na mumuabudu Yeye, na mumshukuru Yeye. Kwake Yeye ndio mtarudishwa



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 18

وَإِن تُكَذِّبُواْ فَقَدۡ كَذَّبَ أُمَمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡۖ وَمَا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mkikadhibisha, basi kaumu kadhaa wa kadhaa za kabla yenu zilikwisha kadhibisha. Na si juu ya Mtume ila kufikisha Ujumbe waziwazi



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 24

فَمَا كَانَ جَوَابَ قَوۡمِهِۦٓ إِلَّآ أَن قَالُواْ ٱقۡتُلُوهُ أَوۡ حَرِّقُوهُ فَأَنجَىٰهُ ٱللَّهُ مِنَ ٱلنَّارِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ

Basi haikuwa jawabu ya watu wake ila ni kusema: Muuweni au mchomeni moto! Allah akamwokoa na moto. Hakika katika hayo zipo Ishara kwa watu wanaoamini



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 25

وَقَالَ إِنَّمَا ٱتَّخَذۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَوۡثَٰنٗا مَّوَدَّةَ بَيۡنِكُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يَكۡفُرُ بَعۡضُكُم بِبَعۡضٖ وَيَلۡعَنُ بَعۡضُكُم بَعۡضٗا وَمَأۡوَىٰكُمُ ٱلنَّارُ وَمَا لَكُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Na alisema: Hakika nyinyi mmeyashika masanamu badala ya Allah kwa mapenzi yaliyo baina yenu katika uhai wa duniani. Kisha Siku ya Kiyama mtakataana nyinyi kwa nyinyi, na mtalaaniana nyinyi kwa nyinyi. Na makaazi yenu ni Motoni. Wala hamtapata wa kukunusuruni



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 26

۞فَـَٔامَنَ لَهُۥ لُوطٞۘ وَقَالَ إِنِّي مُهَاجِرٌ إِلَىٰ رَبِّيٓۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Lutwi akamuamini, na akasema: Mimi nahamia kwa Mola wangu Mlezi. Hakika Yeye ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 27

وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَ وَجَعَلۡنَا فِي ذُرِّيَّتِهِ ٱلنُّبُوَّةَ وَٱلۡكِتَٰبَ وَءَاتَيۡنَٰهُ أَجۡرَهُۥ فِي ٱلدُّنۡيَاۖ وَإِنَّهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ لَمِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na tulimtunukia (Ibrahim) Is-haq na Yaa’qub. Na tukajaalia katika dhuriya zake Unabii na Kitabu, na tukampa ujira wake katika dunia; naye hakika katika Akhera bila ya shaka ni katika watu wema



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 31

وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُوٓاْ إِنَّا مُهۡلِكُوٓاْ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِۖ إِنَّ أَهۡلَهَا كَانُواْ ظَٰلِمِينَ

Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawaangamiza watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 32

قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطٗاۚ قَالُواْ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَن فِيهَاۖ لَنُنَجِّيَنَّهُۥ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Akasema: Hakika humo yumo Lutwi. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipokuwa mkewe aliye miongoni mwa wataokaa nyuma



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 83

۞وَإِنَّ مِن شِيعَتِهِۦ لَإِبۡرَٰهِيمَ

Na hakika Ibrahim alikuwa katika kundi lake,