فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
Partager :
يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلسَّاعَةِ أَيَّانَ مُرۡسَىٰهَا
Wanakuuliza kuhusu Kiyama lini kufika kwake?
فِيمَ أَنتَ مِن ذِكۡرَىٰهَآ
Una nini wewe hata ukitaje hicho kiyama?
إِلَىٰ رَبِّكَ مُنتَهَىٰهَآ
Kwa Mola wako ndio mwisho wake
إِنَّمَآ أَنتَ مُنذِرُ مَن يَخۡشَىٰهَا
Kwa hakika wewe ni mwonyaji tu kwa mwenye kukiogopa hicho kiyama
كَأَنَّهُمۡ يَوۡمَ يَرَوۡنَهَا لَمۡ يَلۡبَثُوٓاْ إِلَّا عَشِيَّةً أَوۡ ضُحَىٰهَا
Siku watakapokiona, watakuwa kana kwamba hawakubaki (duniani) isipokuwa jioni moja au mchana wake
فَإِذَا جَآءَتِ ٱلصَّآخَّةُ
Basi utakapokuja ukelele mkali, (wenye kuumiza masikio)
يَوۡمَ يَفِرُّ ٱلۡمَرۡءُ مِنۡ أَخِيهِ
Siku ambayo, Mtu atakapomkimbia ndugu yake
وَأُمِّهِۦ وَأَبِيهِ
Na mama yake na baba yake
وَصَٰحِبَتِهِۦ وَبَنِيهِ
Na mkewe na wanae
لِكُلِّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ يَوۡمَئِذٖ شَأۡنٞ يُغۡنِيهِ
(Kwasababu) Kila mtu miongoni mwao siku hiyo atakuwa na lake la kumtosha yeye mwenyewe
وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ مُّسۡفِرَةٞ
Siku hiyo ziko nyuso zitakazo nawiri
ضَاحِكَةٞ مُّسۡتَبۡشِرَةٞ
Zikicheka na kufurahika, (na zitachangamka)
وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ عَلَيۡهَا غَبَرَةٞ
Na ziko nyuso siku hiyo zitakuwa na vumbi juu yake
تَرۡهَقُهَا قَتَرَةٌ
Zitafunikwa na giza zito
أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡكَفَرَةُ ٱلۡفَجَرَةُ
Hao ndio makafiri watenda maovu
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Na nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
ثُمَّ مَآ أَدۡرَىٰكَ مَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ
Tena nini kitakacho kujuulisha Siku ya Malipo ni siku gani?
يَوۡمَ لَا تَمۡلِكُ نَفۡسٞ لِّنَفۡسٖ شَيۡـٔٗاۖ وَٱلۡأَمۡرُ يَوۡمَئِذٖ لِّلَّهِ
(Ni) Siku ambayo nafsi haitakuwa na madaraka yoyote juu ya nafsi; na amri yote siku hiyo ni ya Mwenyezi Mungu tu
كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا
Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,
وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا
Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,
وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ
Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?
يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي
Atasema: Laiti ningeli jitangulizia (mema) katika uhai wangu!
فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ
Basi siku hiyo hataadhibu yeyote kama kuadhibu kwake
وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ
Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake
يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyo tua!
ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ
Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha
فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي
Basi ingia miongoni mwa waja wangu,
وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي
Na ingia katika Pepo yangu
إِذَا زُلۡزِلَتِ ٱلۡأَرۡضُ زِلۡزَالَهَا
Itakapo tetemeshwa ardhi kwa mtetemeko wake!