Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 8

وَٱلۡوَزۡنُ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡحَقُّۚ فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Na mizani siku hiyo ni haki tu. Basi yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yakheri) utakuwa mzito (na kuelemea) basi hao ndio tu wenye kufaulu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 9

وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُم بِمَا كَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَظۡلِمُونَ

Na yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yake ya kheri) utakuwa hafifu, basi hao ndio waliozitia hasara nafsi zao kwa sababu ya walivyokuwa wanazifanyia dhulumu aya zetu (kwa kuzikataa na kuzipinga)



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 102

فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Ama wale ambao mizani zao zitakuwa nzito, hao ndio wenye kufanikiwa



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 103

وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فِي جَهَنَّمَ خَٰلِدُونَ

Na wale ambao mizani zao zitakuwa nyepesi, hao ndio walio zitia hasara nafsi zao, na katika Jahannamu watadumu



Sourate: AL-QAARIAH 

Verset : 6

فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,



Sourate: AL-QAARIAH 

Verset : 7

فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ

Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza



Sourate: AL-QAARIAH 

Verset : 8

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,



Sourate: AL-QAARIAH 

Verset : 9

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!