Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 30

وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّي جَاعِلٞ فِي ٱلۡأَرۡضِ خَلِيفَةٗۖ قَالُوٓاْ أَتَجۡعَلُ فِيهَا مَن يُفۡسِدُ فِيهَا وَيَسۡفِكُ ٱلدِّمَآءَ وَنَحۡنُ نُسَبِّحُ بِحَمۡدِكَ وَنُقَدِّسُ لَكَۖ قَالَ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na (kumbuka) Mola wako alipowaambia Malaika kuwa: Kwa yakini, mimi nitamuweka Khalifa ardhini. Wakasema: Hivi unamuweka humo atakayefanya uharibifu humo na kumwaga damu, na wakati sisi tunakutakasa kwa kukusifu? (Allah) Akasema: Mimi ninajua msichokijua



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 31

وَعَلَّمَ ءَادَمَ ٱلۡأَسۡمَآءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمۡ عَلَى ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ فَقَالَ أَنۢبِـُٔونِي بِأَسۡمَآءِ هَـٰٓؤُلَآءِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na akamfundisha Adamu majina yote, kisha akawaleta wenye majina hayo mbele ya malaika. Akawaambia: Nitajieni majina ya hawa kama ninyi ni wa kweli



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 32

قَالُواْ سُبۡحَٰنَكَ لَا عِلۡمَ لَنَآ إِلَّا مَا عَلَّمۡتَنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَلِيمُ ٱلۡحَكِيمُ

Wakasema: Utakatifu ni wako. Hakuna tunachokijua ila tu ulichotujulisha. Hakika, wewe tu ndiye Mjuzi, Mwenye hekima



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 33

قَالَ يَـٰٓـَٔادَمُ أَنۢبِئۡهُم بِأَسۡمَآئِهِمۡۖ فَلَمَّآ أَنۢبَأَهُم بِأَسۡمَآئِهِمۡ قَالَ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ غَيۡبَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَأَعۡلَمُ مَا تُبۡدُونَ وَمَا كُنتُمۡ تَكۡتُمُونَ

Akasema: Ewe Adamu, waambie majina yao. Basi alipowaambia majina yao, (Allah) akasema: Je, si nilikuambieni kuwa mimi ninajua visivyoonekana mbinguni na ardhini? Na ninayajua mno mnayo yadhihirisha na mnayoyaficha



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 34

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰ وَٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na (kumbuka) tulipowaambia Malaika (kuwa): Msujudieni Adamu. Wakasujudu, isipokuwa Ibilisi alikataa na kuleta kiburi na akawa miongoni mwa makafiri



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 97

قُلۡ مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّـجِبۡرِيلَ فَإِنَّهُۥ نَزَّلَهُۥ عَلَىٰ قَلۡبِكَ بِإِذۡنِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَهُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Sema: Mwenye kuwa adui wa Jibrili, basi (ajue kuwa) yeye ndiye aliyeuteremsha Wahyi (Qur’an) moyoni mwako kwa idhini ya Allah, unaosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake na ni muongozo na bishara kwa waumini



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 98

مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّلَّهِ وَمَلَـٰٓئِكَتِهِۦ وَرُسُلِهِۦ وَجِبۡرِيلَ وَمِيكَىٰلَ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَدُوّٞ لِّلۡكَٰفِرِينَ

Mwenye kuwa adui wa Allah na Malaika wake na Mitume wake na Jibrilina Mikaili, basi hakika, Allah ni adui wa makafiri wote



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 102

وَٱتَّبَعُواْ مَا تَتۡلُواْ ٱلشَّيَٰطِينُ عَلَىٰ مُلۡكِ سُلَيۡمَٰنَۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيۡمَٰنُ وَلَٰكِنَّ ٱلشَّيَٰطِينَ كَفَرُواْ يُعَلِّمُونَ ٱلنَّاسَ ٱلسِّحۡرَ وَمَآ أُنزِلَ عَلَى ٱلۡمَلَكَيۡنِ بِبَابِلَ هَٰرُوتَ وَمَٰرُوتَۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنۡ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَآ إِنَّمَا نَحۡنُ فِتۡنَةٞ فَلَا تَكۡفُرۡۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنۡهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِۦ بَيۡنَ ٱلۡمَرۡءِ وَزَوۡجِهِۦۚ وَمَا هُم بِضَآرِّينَ بِهِۦ مِنۡ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡۚ وَلَقَدۡ عَلِمُواْ لَمَنِ ٱشۡتَرَىٰهُ مَا لَهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنۡ خَلَٰقٖۚ وَلَبِئۡسَ مَا شَرَوۡاْ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمۡۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Na wamefuata yale yanayoso-mwa na Mashetani katika (wakati wa) ufalme wa Suleimani. Na Suleimani hakukufuru, lakini Mashetani ndio waliokufuru; (kwa sababu) wanawafundisha watu uchawi na yaliyoteremshwa kwa Malaika wawili Haruta na Maruta katika mji wa Babil. Na wala hawamfundishi yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru. Basi wakajifunza kwao yale yawezayo kumfarakanisha mtu na mkewe. Na wala wao hawana uwezo wa kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Allah tu. Na wanajifunza yale yanayowadhuru na wala hayawanufaishi. Na kwa yakini wamejua kwamba aliyechagua haya hatakuwa na fungu lolote Akhera. Na nikibaya mnokilewalichozichagulianafsizao laiti wangekuwa wanajua



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 80

وَلَا يَأۡمُرَكُمۡ أَن تَتَّخِذُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ أَرۡبَابًاۚ أَيَأۡمُرُكُم بِٱلۡكُفۡرِ بَعۡدَ إِذۡ أَنتُم مُّسۡلِمُونَ

Na (pia haiwi kwa yeyote ambaye Allah amempa Kitabu, elimu, mamlaka na Utume) akuamrisheni muwafanye Malaika na Manabii kuwa Miungu. Hivi (inawezekana) akuamrisheni ukafiri baada ya kuwa nyinyi ni Waislamu?



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 124

إِذۡ تَقُولُ لِلۡمُؤۡمِنِينَ أَلَن يَكۡفِيَكُمۡ أَن يُمِدَّكُمۡ رَبُّكُم بِثَلَٰثَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ مُنزَلِينَ

Na (kumbuka) ulipowaambia Waumini: Hivi haitakutosheni Mola wenu kukuleteeni Malaika elfu tatu walioteremshwa?



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 125

بَلَىٰٓۚ إِن تَصۡبِرُواْ وَتَتَّقُواْ وَيَأۡتُوكُم مِّن فَوۡرِهِمۡ هَٰذَا يُمۡدِدۡكُمۡ رَبُّكُم بِخَمۡسَةِ ءَالَٰفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ مُسَوِّمِينَ

Ni kweli kabisa; ikiwa mtakuwa na subira na mkamcha Allah na maadui wakakujieni kwa ghafla, basi hapo Mola wenu Mlezi atakuleteeni msaada wa Malaika elfu tano wenye kujiweka alama maalum



Sourate: ANNISAI 

Verset : 97

إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَفَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ ظَالِمِيٓ أَنفُسِهِمۡ قَالُواْ فِيمَ كُنتُمۡۖ قَالُواْ كُنَّا مُسۡتَضۡعَفِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ قَالُوٓاْ أَلَمۡ تَكُنۡ أَرۡضُ ٱللَّهِ وَٰسِعَةٗ فَتُهَاجِرُواْ فِيهَاۚ فَأُوْلَـٰٓئِكَ مَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَسَآءَتۡ مَصِيرًا

Hakika, wale ambao Malaika wamewafisha (wamewatoa roho) ilhali wamezidhulumu nafsi zao, (Malaika) watawauliza: Je, mlikuwa na nini nyinyi? Watasema: Tulikuwa wayonge katika ardhi (duniani). (Malaika) Watawaambia: Hivi Ardhi ya Allah haikuwa yenye wasaa mkahama humo? Basi hao makazi yao ni Jahanamu, na marejeo mabaya mno ni hayo.[1]


1- - Aya hii inawataka Waislamu kutoridhika na mazingira ambayo sio rafiki katika kutekeleza majukumu ya dini yao na pia mambo yao ya kimaendeleo. Wanatakiwa kupambana na ikishindikana wahame na kwenda eneo jingine lenye mazingira rafiki.


Sourate: AL-AN’AAM 

Verset : 93

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ قَالَ أُوحِيَ إِلَيَّ وَلَمۡ يُوحَ إِلَيۡهِ شَيۡءٞ وَمَن قَالَ سَأُنزِلُ مِثۡلَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۗ وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلظَّـٰلِمُونَ فِي غَمَرَٰتِ ٱلۡمَوۡتِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ بَاسِطُوٓاْ أَيۡدِيهِمۡ أَخۡرِجُوٓاْ أَنفُسَكُمُۖ ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ عَذَابَ ٱلۡهُونِ بِمَا كُنتُمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَكُنتُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهِۦ تَسۡتَكۡبِرُونَ

Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia Allah uongo (kuwa amempa Utume) au aliyesema kuwa: Nimeletewa Wahyi na ilhali hakuletewa Wahyi wowote? Na (ni nani dhalimu zaidi kuliko) yule aliyesema kuwa: Nitateremsha mfano wa aliyoteremsha Allah? Na lau ungeona wakati madhalimu wamo katika mahangaiko ya mauti na Malaika wamenyoosha mikono yao (wakiwa tayari kuchukua roho zao wakiwaambia): Zitoeni (ziokoeni) roho zenu (kutoka mikononi mwetu kama mnaweza kwa sababu) leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya yale yasiyokuwa ya haki mliyomsingizia Allah, na mlikuwa mnazifanyia kiburi Aya zake



Sourate: AN-FAL 

Verset : 9

إِذۡ تَسۡتَغِيثُونَ رَبَّكُمۡ فَٱسۡتَجَابَ لَكُمۡ أَنِّي مُمِدُّكُم بِأَلۡفٖ مِّنَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ مُرۡدِفِينَ

(Kumbukeni) Wakati mna-muomba msaada Mola wenu Mlezi akuokoeni (dhidi ya maadui zenu), akakujibuni kuwa: Kwa yakini Mimi nitakusaidieni kwa (kuleta vikosi vya) Malaika elfu moja wanaofuatana mfululizo



Sourate: AN-FAL 

Verset : 12

إِذۡ يُوحِي رَبُّكَ إِلَى ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ أَنِّي مَعَكُمۡ فَثَبِّتُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۚ سَأُلۡقِي فِي قُلُوبِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلرُّعۡبَ فَٱضۡرِبُواْ فَوۡقَ ٱلۡأَعۡنَاقِ وَٱضۡرِبُواْ مِنۡهُمۡ كُلَّ بَنَانٖ

(Kumbuka) Wakati Mola wako Mlezi alipowapa Wahyi (vikosi vya) Malaika kwamba: Hakika Mimi nipo pamoja nanyi (kwa kukusaidieni na kukupeni ushindi), basi watieni nguvu walioamini (kwa kuwapa bishara njema). Nitatia woga kwenye nyoyo za waliokufuru (hadi washindwe). Basi wapigeni juu ya shingo (vichwani) na wapigeni kwenye kila ncha za vidole (vya mikono na miguu)



Sourate: AN-FAL 

Verset : 50

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ يَتَوَفَّى ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَضۡرِبُونَ وُجُوهَهُمۡ وَأَدۡبَٰرَهُمۡ وَذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ

Na laiti (ewe Muhammad ungekuwa) unaona wakati Malaika wanawaua makafiri huku wakizipiga nyuso zao na migongo yao na (kuwaambia): Onjeni adhabu ya kuungua (ungeona jambo kubwa la kutisha)



Sourate: AN-FAL 

Verset : 51

ذَٰلِكَ بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيكُمۡ وَأَنَّ ٱللَّهَ لَيۡسَ بِظَلَّـٰمٖ لِّلۡعَبِيدِ

Hilo (la kuwafanyia hivyo makafiri kwenye vita vya Badri) ni kwasababu ya yale yaliyotangulizwa (yaliyofanywa) na mikono yenu (nyinyi makafiri kwa kuwanyanyasa Waislamu), na hakika Allah kamwe si Mwenye kuwadhulumu waja



Sourate: HUUD 

Verset : 69

وَلَقَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞۖ فَمَا لَبِثَ أَن جَآءَ بِعِجۡلٍ حَنِيذٖ

Na hakika walikuja wajumbe wetu kwa Ibrahimu kwa bishara njema, wakasema: Salama! Naye akasema: salama! Haukupita muda akaleta ndama wa kuchoma



Sourate: AR-RA’D 

Verset : 11

لَهُۥ مُعَقِّبَٰتٞ مِّنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَمِنۡ خَلۡفِهِۦ يَحۡفَظُونَهُۥ مِنۡ أَمۡرِ ٱللَّهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُغَيِّرُ مَا بِقَوۡمٍ حَتَّىٰ يُغَيِّرُواْ مَا بِأَنفُسِهِمۡۗ وَإِذَآ أَرَادَ ٱللَّهُ بِقَوۡمٖ سُوٓءٗا فَلَا مَرَدَّ لَهُۥۚ وَمَا لَهُم مِّن دُونِهِۦ مِن وَالٍ

Kila mtu anao (Malaika) wafuatiliaji mbele yake na nyuma yake wanaomhifadhi[1] kwa amri ya Allah. Hakika, Allah habadili yaliyopo kwa watu mpaka (wao wenyewe) wabadili yaliyomo nafsini mwao. Na Allah anapotaka kuwafikishia jambo baya watu hakuna wa kulizuia na (watu) hawana mlinzi yeyote badala yake


1- - Mwanadamu kila alipo ana Malaika wanaomfuatilia kwa maelekezo ya Allah; wanaomhifadhi yeye na pia kuhifadhi na kutunza kumbukumbu za mambo yote anayoyafanya na pia kauli zote anazozitamka kama ilivyotajwa katika Aya ya 18 ya Sura Qaf (50) na Aya ya 10 mpaka 12 za Sura Al-infitaar (82).


Sourate: AR-RA’D 

Verset : 13

وَيُسَبِّحُ ٱلرَّعۡدُ بِحَمۡدِهِۦ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ مِنۡ خِيفَتِهِۦ وَيُرۡسِلُ ٱلصَّوَٰعِقَ فَيُصِيبُ بِهَا مَن يَشَآءُ وَهُمۡ يُجَٰدِلُونَ فِي ٱللَّهِ وَهُوَ شَدِيدُ ٱلۡمِحَالِ

Na Radi inamtakasa Allah kwa kumuhimidi na Malaika pia (wanamsabihi Allah) kwa kumuogopa. Na (Allah) anapeleka vimondo (vya umeme wa radi) na kumlengeshea (vimondo hivyo) amtakaye. Nao wanabishana kuhusu Allah hali ya kuwa Yeye ni Mkali wa kuadhibu



Sourate: AR-RA’D 

Verset : 23

جَنَّـٰتُ عَدۡنٖ يَدۡخُلُونَهَا وَمَن صَلَحَ مِنۡ ءَابَآئِهِمۡ وَأَزۡوَٰجِهِمۡ وَذُرِّيَّـٰتِهِمۡۖ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَدۡخُلُونَ عَلَيۡهِم مِّن كُلِّ بَابٖ

Nazo ni Bustani za milele, wataingia wao na waliyo wema miongoni mwa Baba zao, na wake zao, na vizazi vyao (hata kama hawakufikia daraja za ucha Mungu). Na Malaika wanaingia kwao wao katika kila mlango



Sourate: AR-RA’D 

Verset : 24

سَلَٰمٌ عَلَيۡكُم بِمَا صَبَرۡتُمۡۚ فَنِعۡمَ عُقۡبَى ٱلدَّارِ

(Wakiwaambia) Assalamu Alaikum, Amani iwe kwenu, kwasababu ya mlivyo subiri, basi ni mema mno malipo ya nyumba ya Akhera



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 7

لَّوۡمَا تَأۡتِينَا بِٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

(Kama ni mkweli) Si utuletee Malaika (waje watuthibitishie Utume wako) ikiwa wewe ni miongoni mwa wanaosema kweli?



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 8

مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذٗا مُّنظَرِينَ

(Allah akawajibu washirikina) Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa haki, na hapo (watakapoteremshwa Malaika) hawatapewa muhula



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 28

وَإِذۡ قَالَ رَبُّكَ لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ إِنِّي خَٰلِقُۢ بَشَرٗا مِّن صَلۡصَٰلٖ مِّنۡ حَمَإٖ مَّسۡنُونٖ

Na (kumbuka) Mola wako Mlezi alipowaambia Malaika: Hakika Mimi nitamuumba mtu kwa udongo unaotoa sauti, unaotokana na matope yaliyovunda



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 29

فَإِذَا سَوَّيۡتُهُۥ وَنَفَخۡتُ فِيهِ مِن رُّوحِي فَقَعُواْ لَهُۥ سَٰجِدِينَ

Basi nitakapomkamilisha na kumpulizia roho yangu, basi mumuangukie kwa kumsujudia



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 30

فَسَجَدَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ كُلُّهُمۡ أَجۡمَعُونَ

Basi Malaika wote kwa pamoja walimsujudia



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 51

وَنَبِّئۡهُمۡ عَن ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ

(Ewe Mtume) Na wape (waja wangu) habari za wageni wa Ibrahim



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 52

إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗا قَالَ إِنَّا مِنكُمۡ وَجِلُونَ

Walipoingia kwake na walisema: Salama! Yeye alisema (kwa kuingia kwenu bila kubisha hodi): Hakika sisi tunakuogopeni



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 53

قَالُواْ لَا تَوۡجَلۡ إِنَّا نُبَشِّرُكَ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ

Walisema (kumwambia): Usiogope. Sisi tunakubashiria kijana mwenye ujuzi mno (Naye ni Is-haka)