Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 27

ٱلَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهۡدَ ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مِيثَٰقِهِۦ وَيَقۡطَعُونَ مَآ أَمَرَ ٱللَّهُ بِهِۦٓ أَن يُوصَلَ وَيُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Ambao wana vunja ahadi za Allah baada ya kuwekwa, na wanakataa alichoamuru Allah kiungwe, na wanafanya uharibifu ardhini. Hao tu ndio wenye hasara



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 77

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَشۡتَرُونَ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ وَأَيۡمَٰنِهِمۡ ثَمَنٗا قَلِيلًا أُوْلَـٰٓئِكَ لَا خَلَٰقَ لَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ ٱللَّهُ وَلَا يَنظُرُ إِلَيۡهِمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika, wale wanaouza ahadi ya Allah na viapo vyao kwa thamani ndogo, hao hawatakuwa na fungu (la kheri yoyote) Akhera, na Allah hatazungumza nao (mazungumzo ya huruma) na hatawaangalia (kwa huruma) Siku ya Kiama na hatowatakasa (kwa kusamehe dhambi zao) na watapata adhabu kali mno



Sourate: AN-FAL 

Verset : 55

إِنَّ شَرَّ ٱلدَّوَآبِّ عِندَ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hakika viumbe waovu mno mbele ya Allah ni wale waliokufuru, kwasababu hawaamini (upekee wa Allah na uweza wake)



Sourate: AN-FAL 

Verset : 56

ٱلَّذِينَ عَٰهَدتَّ مِنۡهُمۡ ثُمَّ يَنقُضُونَ عَهۡدَهُمۡ فِي كُلِّ مَرَّةٖ وَهُمۡ لَا يَتَّقُونَ

Ambao miongoni mwao umeingia[1] nao maafikiano (mikataba) kwamba wasiwasaidie makafiri), kisha wanavunja maafikiano yao kila mara, na hawaogopi (wala hawajali)


1- - Wayahudi wa kabila la Quraidha


Sourate: AN-FAL 

Verset : 57

فَإِمَّا تَثۡقَفَنَّهُمۡ فِي ٱلۡحَرۡبِ فَشَرِّدۡ بِهِم مَّنۡ خَلۡفَهُمۡ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Basi ukiwakuta vitani wafurushe (kisawa sawa ili uwaogopeshe (makafiri wengine) walioko nyuma yao ili wapate kukumbuka (wasithubutu tena kukuchezea na kuuchezea Uislamu)



Sourate: AN-FAL 

Verset : 58

وَإِمَّا تَخَافَنَّ مِن قَوۡمٍ خِيَانَةٗ فَٱنۢبِذۡ إِلَيۡهِمۡ عَلَىٰ سَوَآءٍۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡخَآئِنِينَ

Na ukihofu (ukibaini) khiyana kwa watu wowote, basi watupie (mbali) ahadi yao (na wapige ili wewe na wao) muwe sawa (katika kuvunja ahadi). Hakika, Allah hawapendi wafanyao khiyana



Sourate: ATTAUBA 

Verset : 3

وَأَذَٰنٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦٓ إِلَى ٱلنَّاسِ يَوۡمَ ٱلۡحَجِّ ٱلۡأَكۡبَرِ أَنَّ ٱللَّهَ بَرِيٓءٞ مِّنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ وَرَسُولُهُۥۚ فَإِن تُبۡتُمۡ فَهُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡۖ وَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّكُمۡ غَيۡرُ مُعۡجِزِي ٱللَّهِۗ وَبَشِّرِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِعَذَابٍ أَلِيمٍ

Na (hili) ni tangazo kutoka kwa Allah na Mtume wake kwenda kwa watu (wote) Siku Kubwa ya Hija kwamba, Allah na Mtume wake, wamejiweka kando (kwenye makubaliano) na washirikina (makafiri). Basi iwapo (nyinyi makafiri) mtatubu hiyo itakuwa heri kwenu, na mkikengeuka (mkaipinga haki) basi jueni kuwa nyinyi hamuwezi kumshinda (kumtoroka) Allah. Na wabashirie (waonye) makafiri kuwa watapata adhabu iumizayo mno



Sourate: AR-RA’D 

Verset : 25

وَٱلَّذِينَ يَنقُضُونَ عَهۡدَ ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مِيثَٰقِهِۦ وَيَقۡطَعُونَ مَآ أَمَرَ ٱللَّهُ بِهِۦٓ أَن يُوصَلَ وَيُفۡسِدُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱللَّعۡنَةُ وَلَهُمۡ سُوٓءُ ٱلدَّارِ

Na wale wanaovunja ahadi za Allah baada ya kuzifunga, na wanakata aliyoamrisha Allah yaungwe, na wanafanya uharibifu katika nchi: hao ndio watakaopata laana, na watapata nyumba mbaya



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 95

وَلَا تَشۡتَرُواْ بِعَهۡدِ ٱللَّهِ ثَمَنٗا قَلِيلًاۚ إِنَّمَا عِندَ ٱللَّهِ هُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Na msiuze ahadi ya Allah kwa thamani ndogo. Hakika si vingine (kilicho) kwa Allah ni bora kwenu ikiwa mnajua (hayo)