فَتَلَقَّىٰٓ ءَادَمُ مِن رَّبِّهِۦ كَلِمَٰتٖ فَتَابَ عَلَيۡهِۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ
Adamu akapokea maneno (ya toba) kutoka kwa Mola wake (akatubu) na (Allah) akamkubalia toba yake. Hakika yeye (Allah) ni Mwingi wa kupokea toba, Mwingi wa rehema
ثُمَّ عَفَوۡنَا عَنكُم مِّنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Kisha tukakusameheni baada ya hapo ili mpate kushukuru
وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ إِنَّكُمۡ ظَلَمۡتُمۡ أَنفُسَكُم بِٱتِّخَاذِكُمُ ٱلۡعِجۡلَ فَتُوبُوٓاْ إِلَىٰ بَارِئِكُمۡ فَٱقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ عِندَ بَارِئِكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ
Na (kumbukeni) Musa alip-owaambia watu wake (kuwa): Enyi watu wangu, kwa hakika nyinyi mmezidhulumu nafsi zenu kwa kumfanya kwenu ndama Mungu. Basi tubieni kwa Mola wenu na uaneni. Hilo ni bora kwenu mbeleya Muumba wenu. Allah akakubali toba yenu. Kwa hakika, yeye ni Mwingi wa kukubali toba, Mwingi wa rehema
إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ وَأَصۡلَحُواْ وَبَيَّنُواْ فَأُوْلَـٰٓئِكَ أَتُوبُ عَلَيۡهِمۡ وَأَنَا ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ
Isipokuwa waliotubu na wakare-kebisha na wakabainisha. Basi hao nitakubali tobayao, na mimi tu ndiye Mwingi wa kukubali toba, Mwingi wa kurehemu
إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةَ وَٱلدَّمَ وَلَحۡمَ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ بِهِۦ لِغَيۡرِ ٱللَّهِۖ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَلَآ إِثۡمَ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ
Yeye tu amekuharamishieni mzoga na damu na nyama ya nguruwe na kilichochinjwa kwa kutaja jina lisiliokuwa la Allah. Lakini, aliyefikwa na dharura bila ya kutamani wala kupitiliza kiasi, hana dhambi[1]. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
1- - Kula katika hivyo vilivyo haramishwa.
لَّا يُؤَاخِذُكُمُ ٱللَّهُ بِٱللَّغۡوِ فِيٓ أَيۡمَٰنِكُمۡ وَلَٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا كَسَبَتۡ قُلُوبُكُمۡۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Allah hatakuchukulieni hatua kwa viapo vyenu vya kipuuzi. Lakini atakuchukulieni hatua kwa yale yaliyo nuiwa na nyoyo zenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno
وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا عَرَّضۡتُم بِهِۦ مِنۡ خِطۡبَةِ ٱلنِّسَآءِ أَوۡ أَكۡنَنتُمۡ فِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ سَتَذۡكُرُونَهُنَّ وَلَٰكِن لَّا تُوَاعِدُوهُنَّ سِرًّا إِلَّآ أَن تَقُولُواْ قَوۡلٗا مَّعۡرُوفٗاۚ وَلَا تَعۡزِمُواْ عُقۡدَةَ ٱلنِّكَاحِ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡكِتَٰبُ أَجَلَهُۥۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ فَٱحۡذَرُوهُۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Na si vibaya kwenu posa za fumbo mlizowafumbia au mlicho-kificha kwenye nafsi zenu. Allah amejua kuwa nyinyi mtawakumbuka hao, Na lakini msiwaahidi (ndoa) kwa siri isipokuwa mseme maneno mema. Na msiazimie kufunga nao ndoa mpaka Eda ifike mwisho wake. Na jueni kwamba Allah anajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi jihadharini naye, najueni kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno
لِّلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ وَإِن تُبۡدُواْ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ أَوۡ تُخۡفُوهُ يُحَاسِبۡكُم بِهِ ٱللَّهُۖ فَيَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ
Ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Na kama mkidhihirisha yaliyomo katika nyoyo zenu, au mkiyaficha, Allah atakuhojini kwayo; kwahiyo atamsamehe amtakaye, na atamuadhibu amtakaye. Na Allah ni Mwenye uweza mno wa kila kitu
قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allah, basi nifuateni, Allah atakupendeni na atakusameheni madhambi yenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۚ يَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Ana msamehe amtakaye na anamuadhibu amtakaye. Na Allah ni Msamehevu sana, Mwenye rehema nyingi
وَٱلَّذِينَ إِذَا فَعَلُواْ فَٰحِشَةً أَوۡ ظَلَمُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ ذَكَرُواْ ٱللَّهَ فَٱسۡتَغۡفَرُواْ لِذُنُوبِهِمۡ وَمَن يَغۡفِرُ ٱلذُّنُوبَ إِلَّا ٱللَّهُ وَلَمۡ يُصِرُّواْ عَلَىٰ مَا فَعَلُواْ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ
Na ambao wafanyapo uovu (wamadhambi makubwa) au wakazidhulumu nafsi zao (kwa kufanya madhambi madogo) wanamkumbuka Allah na kuomba msamaha kwa dhambi zao (hizo) na hakuna anayesamehe dhambi isipokuwa Allah tu, na hawaendelei kufanya (madhambi) waliyoyafanya na ilhali wanajua
إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَلَّوۡاْ مِنكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِ إِنَّمَا ٱسۡتَزَلَّهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ بِبَعۡضِ مَا كَسَبُواْۖ وَلَقَدۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Hakika Wale waliorudi miongoni mwenu siku ambayo majeshi mawili yalipokutana, hakika shetani (ndiye) aliyewatelezesha kwa sababu ya baadhi ya makosa waliyoyafanya, na kwa hakika Allah amewasamehe. Hakika Allah ni Msamehevu sana Mpole Mno
إِنَّمَا ٱلتَّوۡبَةُ عَلَى ٱللَّهِ لِلَّذِينَ يَعۡمَلُونَ ٱلسُّوٓءَ بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ يَتُوبُونَ مِن قَرِيبٖ فَأُوْلَـٰٓئِكَ يَتُوبُ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡۗ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Hakika wanaomrudia Allah kwa toba ya kweli ni wale tu wanaofanya baya bila kujua kisha wanatubu muda mchache kabla ya kufa, basi Allah hao anawapokelea toba zao, na Allah ni Mjuzi saana mwenye Hekima
يُرِيدُ ٱللَّهُ لِيُبَيِّنَ لَكُمۡ وَيَهۡدِيَكُمۡ سُنَنَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ وَيَتُوبَ عَلَيۡكُمۡۗ وَٱللَّهُ عَلِيمٌ حَكِيمٞ
Allah anataka kukubainishieni na kukuongozeni katika njia za wale waliokuwepo kabla yenu, na kukusameheni. Na Allah ni Mjuzi mno, Mwenye hekima
وَٱللَّهُ يُرِيدُ أَن يَتُوبَ عَلَيۡكُمۡ وَيُرِيدُ ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلشَّهَوَٰتِ أَن تَمِيلُواْ مَيۡلًا عَظِيمٗا
Na Allah anataka kukusameheni, na wale wanaofuata matamanio ya nafsi (zao) wanataka mpotee upoteaji mkubwa sana
إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَغۡفِرُ أَن يُشۡرَكَ بِهِۦ وَيَغۡفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَآءُۚ وَمَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدِ ٱفۡتَرَىٰٓ إِثۡمًا عَظِيمًا
Hakika, Allah hatoi msamaha (wa dhambi ya) kushirikishwa na anasamehe (dhambi) isiyokuwa hiyo kwa amtakaye. Na yeyote amshirikishaye Allah basi hakika amezua dhambi kubwa kabisa
دَرَجَٰتٖ مِّنۡهُ وَمَغۡفِرَةٗ وَرَحۡمَةٗۚ وَكَانَ ٱللَّهُ غَفُورٗا رَّحِيمًا
Ni daraja nyingi kutoka kwake na msamaha na rehema. Na Allah amekuwa Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu
فَأُوْلَـٰٓئِكَ عَسَى ٱللَّهُ أَن يَعۡفُوَ عَنۡهُمۡۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَفُوًّا غَفُورٗا
Basi hao huenda Allah akawasamehe, na Allah ni Msamehevu sana, Mwingi wa kufuta dhambi
وَمَن يَعۡمَلۡ سُوٓءًا أَوۡ يَظۡلِمۡ نَفۡسَهُۥ ثُمَّ يَسۡتَغۡفِرِ ٱللَّهَ يَجِدِ ٱللَّهَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na yeyote mwenye kutenda baya au kudhulumu nafsi yake, kisha akamuomba msamaha Allah, atamkuta Allah ni Msamehevu sana, Mwenye kurehem
إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَغۡفِرُ أَن يُشۡرَكَ بِهِۦ وَيَغۡفِرُ مَا دُونَ ذَٰلِكَ لِمَن يَشَآءُۚ وَمَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدۡ ضَلَّ ضَلَٰلَۢا بَعِيدًا
Hakika, Allah hatoi msamaha (wa dhambi ya) kushirikishwa, na anasamehe (dhambi) zilizo chini ya hiyo kwa amtakaye. Na yeyote anayemfanyia ushirika Allah kwa hakika amepotea upotevu ulio mbali kabisa (na haki)
وَلَن تَسۡتَطِيعُوٓاْ أَن تَعۡدِلُواْ بَيۡنَ ٱلنِّسَآءِ وَلَوۡ حَرَصۡتُمۡۖ فَلَا تَمِيلُواْ كُلَّ ٱلۡمَيۡلِ فَتَذَرُوهَا كَٱلۡمُعَلَّقَةِۚ وَإِن تُصۡلِحُواْ وَتَتَّقُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا
Na hamtaweza kufanya uadilifu baina ya wanawake (wake zenu) hata kama mtafanya jitihada. Basi (pamoja na hayo) msimili (msielemee) moja kwa moja (kwa mke mmoja), mkamuacha mwingine kama aliyetundikwa (aliyening’inizwa).[1] Na kama mtafanya usuluhishi na mkamcha Allah, hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehem
1- - Waume wanakatazwa kutofanya uadilifu baina ya wake zao kwa kutotoa huduma stahiki kwa usawa au kwa kutelekeza baadhi. Hili halihusu mume mwenye wake zaidi ya mmoja tu, lakini linamhusu hata mume mwenye mke mmoja. Mume mwenye mke mmoja pia haruhusiwi kutomtendea uadilifu mkewe kwa kutompa haki zake au kwa kumtelekeza na kumuweka katika mazingira ya kutojitambua kwamba ni mke au sio mke. Uadilifu unaokusudia na sheria ni uadilifu wa huduma na sio hisia za mvuto, mahaba na mapenzi ya moyoni.
وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٌ عَظِيمٞ
Allah amewaahidi walioamini na kutenda mema (kwamba) watapata msamaha na malipo makubwa sana
وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ وَٱلنَّصَٰرَىٰ نَحۡنُ أَبۡنَـٰٓؤُاْ ٱللَّهِ وَأَحِبَّـٰٓؤُهُۥۚ قُلۡ فَلِمَ يُعَذِّبُكُم بِذُنُوبِكُمۖ بَلۡ أَنتُم بَشَرٞ مِّمَّنۡ خَلَقَۚ يَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُ وَيُعَذِّبُ مَن يَشَآءُۚ وَلِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَاۖ وَإِلَيۡهِ ٱلۡمَصِيرُ
Na Wayahudi na Wanaswara (Wakristo) walisema: “Sisi ni Wana wa Allah (Mungu) na vipenzi vyake”. Sema: “Basi ni kwa nini anakuadhibuni kwa dhambi zenu? Bali nyinyi ni watu (tu) miongoni mwa (watu wengine) aliowaumba. (Allah) Anamsamehe amtakaye (anapotubu) na anamuadhibu amtakaye (asipotubu). Na ni wa Allah tu ufalme wa mbinguni na ardhini na vilivyomo baina yake, na marejeo ni kwake tu
إِلَّا ٱلَّذِينَ تَابُواْ مِن قَبۡلِ أَن تَقۡدِرُواْ عَلَيۡهِمۡۖ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Isipokuwa wale waliotubu kabla hamjawatia nguvuni. Basi jueni kwamba, kwa hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu
فَمَن تَابَ مِنۢ بَعۡدِ ظُلۡمِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَإِنَّ ٱللَّهَ يَتُوبُ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ
Basi mwenye kutubu baada ya kudhulumu kwake na akatengeneza (akarekebisha tabia zake), basi Allah hupokea toba yake. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu
أَلَمۡ تَعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ يُعَذِّبُ مَن يَشَآءُ وَيَغۡفِرُ لِمَن يَشَآءُۗ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Hivi hujui ya kwamba, ni wa Allah tu ufalme wa mbinguni na ardhini? Anamuadhibu amtakaye na anamsamehe amtakaye. Na Allah ni Muweza wa kila kitu
أَفَلَا يَتُوبُونَ إِلَى ٱللَّهِ وَيَسۡتَغۡفِرُونَهُۥۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Hivi, ni kwanini hawatubu kwa Allah na kumuomba msamaha? Na Allah ni Mwingi wa kusamehe mwenye kurehemu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡتُلُواْ ٱلصَّيۡدَ وَأَنتُمۡ حُرُمٞۚ وَمَن قَتَلَهُۥ مِنكُم مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآءٞ مِّثۡلُ مَا قَتَلَ مِنَ ٱلنَّعَمِ يَحۡكُمُ بِهِۦ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ هَدۡيَۢا بَٰلِغَ ٱلۡكَعۡبَةِ أَوۡ كَفَّـٰرَةٞ طَعَامُ مَسَٰكِينَ أَوۡ عَدۡلُ ذَٰلِكَ صِيَامٗا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمۡرِهِۦۗ عَفَا ٱللَّهُ عَمَّا سَلَفَۚ وَمَنۡ عَادَ فَيَنتَقِمُ ٱللَّهُ مِنۡهُۚ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ
Enyi mlioamini, msiue wanya-mapori na hali mmeharimia (mmo ndani ya ibada ya Hija au Umra). Na yeyote miongoni mwenu atakayemuua mnyama huyo kwa makusudi, basi malipo (yake) ni (kuchinja) mnyama wa kufuga mfano wa aliyemuua. Watahukumu hayo waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama (huyo) apelekwe Al-Kaaba (Makkah ili achinjwe huko na nyama yake kugaiwa sadaka kwa maskini wa huko) au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini au badala ya hayo ni kufunga ili (aliyefanya kosa hilo la kuwinda) aonje ubaya wa jambo lake (baya alilolifanya). Allah amekwishafuta yaliyopita (lakini) atakayerudia (kufanya tena kosa hilo) Allah atamuadhibu. Na Allah ni Mwenye nguvu sana, Mwenye kutesa
ٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ وَأَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Jueni kwamba, Allah ni Mkali wa kuadhibu, na kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَسۡـَٔلُواْ عَنۡ أَشۡيَآءَ إِن تُبۡدَ لَكُمۡ تَسُؤۡكُمۡ وَإِن تَسۡـَٔلُواْ عَنۡهَا حِينَ يُنَزَّلُ ٱلۡقُرۡءَانُ تُبۡدَ لَكُمۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهَاۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ
Enyi mlioamini, msiulize mambo (ambayo) mkidhihirishiwa yanakuchukizeni. Na mkiyauliza wakati Qur’ani inateremshwa mtadhihirishiwa. (Msirudie) Allah ameshayasamehe hayo (mliyokwishauliza). Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno