ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُمۡتَرِينَ
Ni haki kutoka kwa Mola wako, basi usiwe miongoni mwa walio na shaka kabisa
كَانَ ٱلنَّاسُ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَبَعَثَ ٱللَّهُ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ فِيمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِۚ وَمَا ٱخۡتَلَفَ فِيهِ إِلَّا ٱلَّذِينَ أُوتُوهُ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۖ فَهَدَى ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لِمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ مِنَ ٱلۡحَقِّ بِإِذۡنِهِۦۗ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٍ
Watu walikuwa umma mmoja. Allah akatuma Mitume wakitoa habari njema na wakitoa maonyo na aliteremsha vitabu pamoja nao kwa haki ili ahukumu kati ya watu katika yale ambayo wametofatiana. Na hawakutofautiana katika hayo isipokuwa wale tu waliopewa vitabu hivyo, baada ya kuwafikia hoja za waziwazi kwa sababu tu ya uovu walionao. Basi Allah akawaongoza wale ambao wameamini kwenye haki kwa idhini yake na Allah anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyo nyooka
نَزَّلَ عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَأَنزَلَ ٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ
Amekuteremshia Kitabu kwa haki kikisadikisha yaliyokuwepo kabla yake. Na ameteremshaTaurati na Injili
يَـٰٓأَهۡلَ ٱلۡكِتَٰبِ لِمَ تَلۡبِسُونَ ٱلۡحَقَّ بِٱلۡبَٰطِلِ وَتَكۡتُمُونَ ٱلۡحَقَّ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Enyi Watu wa Kitabu, kwanini mnachanganya haki na batili na mnaificha haki na ilhali nyinyi mnajua (kuwa mnachofanya sio sahihi)?
تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱللَّهِ نَتۡلُوهَا عَلَيۡكَ بِٱلۡحَقِّۗ وَمَا ٱللَّهُ يُرِيدُ ظُلۡمٗا لِّلۡعَٰلَمِينَ
Hizo ni Aya za Allah tunakusomea kwa haki, na Allah hataki kuwadhulumu walimwengu
إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِتَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ بِمَآ أَرَىٰكَ ٱللَّهُۚ وَلَا تَكُن لِّلۡخَآئِنِينَ خَصِيمٗا
Hakika, sisi tumekuteremshia kitabu kwa haki ili uhukumu baina ya watu kwa kile ambacho Allah amekuonyesha (amekuelimisha). Na usiwe mtetezi wa wanaofanya khiana
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَنُدۡخِلُهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٗاۚ وَمَنۡ أَصۡدَقُ مِنَ ٱللَّهِ قِيلٗا
Na walioamini na wakatenda mema, tutawaingiza katika bustani zitiririkazo mito chini yake, watabaki humo milele. Ni ahadi ya Allah ya kweli, na ni nani mkweli zaidi wa kauli kuliko Allah?
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلرَّسُولُ بِٱلۡحَقِّ مِن رَّبِّكُمۡ فَـَٔامِنُواْ خَيۡرٗا لَّكُمۡۚ وَإِن تَكۡفُرُواْ فَإِنَّ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَكَانَ ٱللَّهُ عَلِيمًا حَكِيمٗا
Enyi watu, hakika amekujieni Mtume kwa haki kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi aminini, iwe kheri kwenu. Na mkikufuru basi hakika ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Na Allah ni Mjuzi sana, Mwenye hekima
وَأَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَمُهَيۡمِنًا عَلَيۡهِۖ فَٱحۡكُم بَيۡنَهُم بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۖ وَلَا تَتَّبِعۡ أَهۡوَآءَهُمۡ عَمَّا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡحَقِّۚ لِكُلّٖ جَعَلۡنَا مِنكُمۡ شِرۡعَةٗ وَمِنۡهَاجٗاۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَعَلَكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَلَٰكِن لِّيَبۡلُوَكُمۡ فِي مَآ ءَاتَىٰكُمۡۖ فَٱسۡتَبِقُواْ ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ
Na tumekuteremshia Kitabu kwa haki kikisadikisha vitabu vilivyokuwepo kabla yake na kikivitawala. Basi hukumu baina yao kwa (sheria) aliyokuteremshia Allah, na usifuate utashi wa nafsi zao ukaacha haki iliyokujia. Kila kundi katika nyinyi tumeliwekea sharia na njia. Na lau Allah angelitaka angekufanyeni (nyote) umma mmoja, lakini (amefanya hivyo) ili akujaribuni katika aliyokupeni. Basi shindaneni kwa mambo ya kheri. Kwa Allah tu ndio marejeo yenu nyote, na atakuambieni yale mliyokuwa mkitofautiana
وَإِذَا سَمِعُواْ مَآ أُنزِلَ إِلَى ٱلرَّسُولِ تَرَىٰٓ أَعۡيُنَهُمۡ تَفِيضُ مِنَ ٱلدَّمۡعِ مِمَّا عَرَفُواْ مِنَ ٱلۡحَقِّۖ يَقُولُونَ رَبَّنَآ ءَامَنَّا فَٱكۡتُبۡنَا مَعَ ٱلشَّـٰهِدِينَ
Na wanaposikia yaliyoteremshwa kwa Mtume utaona macho yao yanabubujika machozi kwasababu ya haki waliyoitambua. Wanasema: Ewe Mola wetu Mlezi, tumeamini; basi tuandike (tuwe) pamoja na wanaoshuhudia (Uungu wako, upekee wako na kuabudiwa kwako)
وَمَا لَنَا لَا نُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَمَا جَآءَنَا مِنَ ٱلۡحَقِّ وَنَطۡمَعُ أَن يُدۡخِلَنَا رَبُّنَا مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Na kwanini tusimuamini Allah na haki iliyotujia (Qur’an) Na hali tunatumai Mola wetu Mlezi atuingize pamoja na watu wema?
وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Na yeye ndiye aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na (kumbuka) siku (Allah) anaposema (kuliambia jambo): Kuwa, basi linakuwa. Kauli yake ni haki. Ni wake yeye tu ufalme siku litakapopulizwa baragumu. Ni mjuzi wa Ghaibu (yaliyofichika) na yaliyo bayana. Na yeye ni Mwenye hekima, Mjuzi wa habari (zote)
وَمِمَّنۡ خَلَقۡنَآ أُمَّةٞ يَهۡدُونَ بِٱلۡحَقِّ وَبِهِۦ يَعۡدِلُونَ
Na katika tuliowaumba upo umma unao ongoza kwa kutumia haki na kwa (haki) hiyo wanafanya uadilifu
يُرِيدُونَ أَن يُطۡفِـُٔواْ نُورَ ٱللَّهِ بِأَفۡوَٰهِهِمۡ وَيَأۡبَى ٱللَّهُ إِلَّآ أَن يُتِمَّ نُورَهُۥ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡكَٰفِرُونَ
(Makafiri) Wanataka kuizima Nuru ya Allah (Uislamu) kwa vinywa vyao, na Allah anakataa ila (ni lazima) aitimize Nuru yake (Dini yake na kumnusuru Nabii wake) na hata kama makafiri watachukia
هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُشۡرِكُونَ
Yeye (Allah) ndiye aliyemtuma Mtume wake kwa uwongofu (Qur’an) na Dini ya Haki ili ipate kuzishinda dini zote, na hata kama washirikina watachukia
إِلَيۡهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗاۖ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقًّاۚ إِنَّهُۥ يَبۡدَؤُاْ ٱلۡخَلۡقَ ثُمَّ يُعِيدُهُۥ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ بِٱلۡقِسۡطِۚ وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ
Kwake tu ndio marejeo yenu nyote. Hii ni ahadi ya kweli ya Allah. Hakika yeye (Allah) anaanza kuumba kisha anarudisha (kuumba) ili awalipe kwa uadilifu wale walioamini na wakatenda mema. Na wale waliokufuru watapata kinywaji cha maji ya moto sana na adhabu iumizayo mno kwa sababu ya ukafiri waliokuwa wakiufanya
هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ ٱلشَّمۡسَ ضِيَآءٗ وَٱلۡقَمَرَ نُورٗا وَقَدَّرَهُۥ مَنَازِلَ لِتَعۡلَمُواْ عَدَدَ ٱلسِّنِينَ وَٱلۡحِسَابَۚ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ يُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ
Ni yeye ambaye amelifanya jua lenye kuangaza na mwezi kuwa na nuru na ameuwekea (mwezi) vituo ili (kwa kutumia mwezi) mjue idadi ya miaka na hesabu. Allah hakuviumba hivyo isipokuwa kwa haki tu, anazifafanua Aya (zake) kwa watu wanaojua
فَلَمَّآ أَنجَىٰهُمۡ إِذَا هُمۡ يَبۡغُونَ فِي ٱلۡأَرۡضِ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۗ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنَّمَا بَغۡيُكُمۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِكُمۖ مَّتَٰعَ ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ ثُمَّ إِلَيۡنَا مَرۡجِعُكُمۡ فَنُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Basi (Allah) alipowaokoa, ghafla wakawa wanafanya uovu katika ardhi bila ya haki. Enyi watu, hakika uasi wenu ni hasara kwenu; ni anasa (fupi) za maisha ya duniani. Kisha kwetu tu ndio marejeo yenu, kwa hiyo tutakuambieni yote mliyokuwa mkiyafanya
قُلۡ هَلۡ مِن شُرَكَآئِكُم مَّن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّۚ قُلِ ٱللَّهُ يَهۡدِي لِلۡحَقِّۗ أَفَمَن يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلۡحَقِّ أَحَقُّ أَن يُتَّبَعَ أَمَّن لَّا يَهِدِّيٓ إِلَّآ أَن يُهۡدَىٰۖ فَمَا لَكُمۡ كَيۡفَ تَحۡكُمُونَ
Sema: Hivi katika washirika (Miungu) wenu (mnaowashirikisha na Allah), yupo anayeongoza kwenye haki? Sema: Allah pekee ndiye anayeongoza kwenye haki. Basi, hivi anayeongoza kwenye haki ana haki zaidi ya kufuatwa au (mwenye haki zaidi ya kufuatwa ni) yule asiyeweza kuongoza chochote isipokuwa aongozwe? Basi mnanini nyinyi? Mnahukumuje?
وَمَا يَتَّبِعُ أَكۡثَرُهُمۡ إِلَّا ظَنًّاۚ إِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـًٔاۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا يَفۡعَلُونَ
Na wengi wao hawafuati isipokuwa dhana tu. Hakika, dhana haifaidishi chochote kwenye haki. Hakika, Allah ni Mjuzi wa wanayoyatenda
۞وَيَسۡتَنۢبِـُٔونَكَ أَحَقٌّ هُوَۖ قُلۡ إِي وَرَبِّيٓ إِنَّهُۥ لَحَقّٞۖ وَمَآ أَنتُم بِمُعۡجِزِينَ
Na wanataka uwaeleze: Je, ni kweli hayo (unayowaambia)? Sema: Ndio! Ninaapa kwa Mola wangu Mlezi kwamba, kwa hakika kabisa, hayo ni kweli, na ninyi si wenye kushinda!
أَلَآ إِنَّ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ أَلَآ إِنَّ وَعۡدَ ٱللَّهِ حَقّٞ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Zindukeni: Bila ya shaka, ni vya Allah tu vyote vilivyomo mbinguni na ardhini. Zindukeni: Hakika, ahadi ya Allah ni kweli, na lakini wengi wao sana hawajui
فَإِن كُنتَ فِي شَكّٖ مِّمَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ فَسۡـَٔلِ ٱلَّذِينَ يَقۡرَءُونَ ٱلۡكِتَٰبَ مِن قَبۡلِكَۚ لَقَدۡ جَآءَكَ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمُمۡتَرِينَ
Basi kama una shaka katika yale tuliyokuteremshia, basi waulize wale wanaosoma kitabu (Taurati) kabla yako. Kwa yakini kabisa, haki imekwisha kukufikia kutoka kwa Mola wako Mlezi. Kwa hiyo, katu usiwe miongoni mwa watiao shaka
قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ قَدۡ جَآءَكُمُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكُمۡۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَإِنَّمَا يَهۡتَدِي لِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنَا۠ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ
Sema: Enyi watu, hakika imekujieni haki kutoka kwa Mola wenu Mlezi. Basi yeyote anayeongoka, anaongoka kwa faida ya nafsi yake, na anayepotea, basi kwa hakika anapotea kwa hasara ya nafsi yake. Na mimi si msaidizi kwenu
وَكُلّٗا نَّقُصُّ عَلَيۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلرُّسُلِ مَا نُثَبِّتُ بِهِۦ فُؤَادَكَۚ وَجَآءَكَ فِي هَٰذِهِ ٱلۡحَقُّ وَمَوۡعِظَةٞ وَذِكۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ
Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini
الٓمٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِۗ وَٱلَّذِيٓ أُنزِلَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَ ٱلۡحَقُّ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يُؤۡمِنُونَ
Alif Laam Miim Raa[1]. Hizo ni Aya za Kitabu. Na (hii Qur’an ni wahyi) ambayo umeteremshiwa kutoka kwa Mola wako Mlezi ni haki lakini watu wengi hawaamini
1- - Allah pekee ndiye anayejua maana ya herufi hizi mkato.
أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَسَالَتۡ أَوۡدِيَةُۢ بِقَدَرِهَا فَٱحۡتَمَلَ ٱلسَّيۡلُ زَبَدٗا رَّابِيٗاۖ وَمِمَّا يُوقِدُونَ عَلَيۡهِ فِي ٱلنَّارِ ٱبۡتِغَآءَ حِلۡيَةٍ أَوۡ مَتَٰعٖ زَبَدٞ مِّثۡلُهُۥۚ كَذَٰلِكَ يَضۡرِبُ ٱللَّهُ ٱلۡحَقَّ وَٱلۡبَٰطِلَۚ فَأَمَّا ٱلزَّبَدُ فَيَذۡهَبُ جُفَآءٗۖ وَأَمَّا مَا يَنفَعُ ٱلنَّاسَ فَيَمۡكُثُ فِي ٱلۡأَرۡضِۚ كَذَٰلِكَ يَضۡرِبُ ٱللَّهُ ٱلۡأَمۡثَالَ
(Allah) Ameteremsha maji kutoka mawinguni. Na mabonde yakatiririsha maji kwa kadiri yake. Na mafuriko yakachukua mapovu yaliyokusanyika juu yake. Na baadhi ya (madini) wanayo yayeyusha katika moto kwa kutaka mapambo au vyombo hutokea povu vile vile (wakati wa kuyayusha). Namna hiyo ndivyo Allah anavyopiga mifano ya haki na batili. Basi lile povu linapita kama takataka tu. Ama kinachowafaa watu hubakia kwenye ardhi. Hivi ndivyo Allah anavyopiga mifano
مَا نُنَزِّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّ وَمَا كَانُوٓاْ إِذٗا مُّنظَرِينَ
(Allah akawajibu washirikina) Sisi hatuwateremshi Malaika ila kwa haki, na hapo (watakapoteremshwa Malaika) hawatapewa muhula
وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ
Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika tu (wala hilo halina shaka). Basi (Ewe Mtume) samehe (watu wako) msamaha mzuri
خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ تَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Ameziumba mbingu na ardhi kwa haki. Ametukuka Allah na ametukuka (juu zaidi) ya vyote wanavyovishirikisha naye