Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 96

وَلَتَجِدَنَّهُمۡ أَحۡرَصَ ٱلنَّاسِ عَلَىٰ حَيَوٰةٖ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْۚ يَوَدُّ أَحَدُهُمۡ لَوۡ يُعَمَّرُ أَلۡفَ سَنَةٖ وَمَا هُوَ بِمُزَحۡزِحِهِۦ مِنَ ٱلۡعَذَابِ أَن يُعَمَّرَۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na kwa hakika kabisa, utawakuta wao (Wayahudi) ndio wanaojali mno uhai[1] kuliko watu wote, na miongoni mwa washirikishaji (pia utakuta nao wako hivyo); anatamani mmoja wao angalau apewe umri wa miaka elfu moja. Na kupewa kwake umri mrefu hakutamuepushia adhabu, na Allah ni Mwenye kuyaona wanayoyatenda


1- - Katika maisha ya duniani


Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 137

فَإِنۡ ءَامَنُواْ بِمِثۡلِ مَآ ءَامَنتُم بِهِۦ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا هُمۡ فِي شِقَاقٖۖ فَسَيَكۡفِيكَهُمُ ٱللَّهُۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Endapo wataamini kama mlivyoamini, basi watakuwa wameongoka. Na endapo watakataa, basi elewa kuwa si vingine bali hao wako katika upinzani tu. Na Allah atakusalimisha nao. Na yeye ni Msikivu, Mwenye kujua sana



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 144

قَدۡ نَرَىٰ تَقَلُّبَ وَجۡهِكَ فِي ٱلسَّمَآءِۖ فَلَنُوَلِّيَنَّكَ قِبۡلَةٗ تَرۡضَىٰهَاۚ فَوَلِّ وَجۡهَكَ شَطۡرَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَحَيۡثُ مَا كُنتُمۡ فَوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ شَطۡرَهُۥۗ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَيَعۡلَمُونَ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّهِمۡۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا يَعۡمَلُونَ

Tunaona ukigeuzageuza uso wako mbinguni. Hakika tunakuelekeza Kibla unachokiridhia, Basi elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtukufu[1]. Na popote muwapo elekezeni nyuso zenu upande huo. Na hakika wale ambao wamepewa kitabu wanajua kwamba hiyo ni haki kutoka kwa Mola wao. Na Allah hakuwa mwenye kughafilika na wanayotenda


1- - Msikiti Mtukufu wa Makka


Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 20

فَإِنۡ حَآجُّوكَ فَقُلۡ أَسۡلَمۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّهِ وَمَنِ ٱتَّبَعَنِۗ وَقُل لِّلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡأُمِّيِّـۧنَ ءَأَسۡلَمۡتُمۡۚ فَإِنۡ أَسۡلَمُواْ فَقَدِ ٱهۡتَدَواْۖ وَّإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِٱلۡعِبَادِ

Na kama watakuletea hoja (yoyote), basi sema: Nimeukabidhi uso wangu (nimejisalimisha) kwa Allah; mimi na wale walionifuata. Na waambie waliopewa kitabu na wasio na elimu kwamba: Je, mmesilimu (Mmejisalimisha kwa Allah)? Kama wamesilimu basi hakika wameongoka, na kama wakikataa, basi wajibu wako ni kufikisha tu. Na Allah anawaona mno waja



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 38

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُۥۖ قَالَ رَبِّ هَبۡ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةٗ طَيِّبَةًۖ إِنَّكَ سَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Hapo, Zakaria alimuomba Mola wake. Alisema: “Ewe Mola wangu, nakuomba kizazi chema kutoka kwako, hakika wewe ni Mwingi wa kusikia maombi



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 156

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَقَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ إِذَا ضَرَبُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ كَانُواْ غُزّٗى لَّوۡ كَانُواْ عِندَنَا مَا مَاتُواْ وَمَا قُتِلُواْ لِيَجۡعَلَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ حَسۡرَةٗ فِي قُلُوبِهِمۡۗ وَٱللَّهُ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Enyi mlioamini msiwe kama wale waliokufuru na wakasema kuhusu ndugu zao waliposafiri ardhini au walipokuwa vitani; kama wangekuwa kwetu wasingekufa na wasingeuwawa ili Allah afanye hilo kuwa ni majuto katika nyoyo zao, na Allah anahuisha na anafisha na Allah kwa munayoyatenda ni Mwenye kuyaona mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 163

هُمۡ دَرَجَٰتٌ عِندَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Hao wana vyeo mbalimbali kwa Allah, na Allah ni mwenye kuyaona yote wayatendayo



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 181

لَّقَدۡ سَمِعَ ٱللَّهُ قَوۡلَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ فَقِيرٞ وَنَحۡنُ أَغۡنِيَآءُۘ سَنَكۡتُبُ مَا قَالُواْ وَقَتۡلَهُمُ ٱلۡأَنۢبِيَآءَ بِغَيۡرِ حَقّٖ وَنَقُولُ ذُوقُواْ عَذَابَ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika Allah amesikia kauli ya wale waliosema: Hakika Allah ni fukara na sisi ndio matajiri, tutakisajili walichokisema, na kuwaua kwao manabii bila ya haki, na siku ya Kiama tutawaambia: onjeni adhabu ya Moto wenye kuunguza



Sourate: ANNISAI 

Verset : 58

۞إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تُؤَدُّواْ ٱلۡأَمَٰنَٰتِ إِلَىٰٓ أَهۡلِهَا وَإِذَا حَكَمۡتُم بَيۡنَ ٱلنَّاسِ أَن تَحۡكُمُواْ بِٱلۡعَدۡلِۚ إِنَّ ٱللَّهَ نِعِمَّا يَعِظُكُم بِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ سَمِيعَۢا بَصِيرٗا

Hakika, Allah anakuamrisheni kurudisha amana kwa wenyewe, na mnapo hukumu baina ya watu mhukumu kwa uadilifu. Hakika, mazuri mno anayokuwaidhini Allah ni hayo. HakikaAllah ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kuona



Sourate: ANNISAI 

Verset : 148

۞لَّا يُحِبُّ ٱللَّهُ ٱلۡجَهۡرَ بِٱلسُّوٓءِ مِنَ ٱلۡقَوۡلِ إِلَّا مَن ظُلِمَۚ وَكَانَ ٱللَّهُ سَمِيعًا عَلِيمًا

Allah hapendi kudhihirisha kauli ovu isipokuwa kwa mwenye kudhulumiwa. Na Allah ni Mwenye kusikia sana, Mjuzi sana.[1]


1- - Aya inamkataza Muislamu kuwa na hulka na tabia ya kutoa kauli zisizofaa na zisizokuwa na staha. Lakini mbele ya mamlaka au mbele ya vyombo vya sheria na maamuzi, Muislamu ambaye amedhulumiwa haki yake anaruhusiwa kuwasilisha madai na, ikibidi kutamka maneno halisi ili madai yake yaeleweke, hata kama maneno ni makali. Anaruhusiwa kufanya hivyo ili apate haki yake na ili dhalimu aadhibiwe kwa kupewa adhabu anayostahiki.


Sourate: AL-AN’AAM 

Verset : 103

لَّا تُدۡرِكُهُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَهُوَ يُدۡرِكُ ٱلۡأَبۡصَٰرَۖ وَهُوَ ٱللَّطِيفُ ٱلۡخَبِيرُ

Macho hayamuoni (hapa duniani) na yeye anayaona macho[1]. Na yeye ni Mpole sana, Mwenye habari (za kila kitu)


1- - Itikadi ya Watu wa Suna na Jamaa (Suni) ni kwamba, Allah haonekani hapa duniani kwa mujibu wa Aya hii na pia kwa mujibu wa: 1) Nukuu ya Mama Aisha mke wa Mtume aliyenukuliwa akisema kuwa: “Anayedai kuwa Muhammad alimuona Mola wake hakika amesema uongo”. 2) Aya ya 143 ya Sura Al-aaraaf (7) ambapo Mtume Musa alimuomba Mola wake amuwezeshe kumuona na ikashindikana. Ama Akhera Allah ataonekana kwa mujibu wa: 1) Aya ya 23 ya Sura Alqiyama (75). 2) Aya ya 15 ya Sura Almutwaffifiin (83) inayoeleza kuwa makafiri Siku ya Kiama watazuiwa kumuona Mola wao. Amesema Imamu Shaafii katika kuitafsiri Aya hii kwamba, hii inaonesha kuwa Waumini hawatazuiwa kumuona Mola wao.


Sourate: AN-FAL 

Verset : 61

۞وَإِن جَنَحُواْ لِلسَّلۡمِ فَٱجۡنَحۡ لَهَا وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na (makafiri) wakielekea kutaka amani (na suluhu), basi na wewe elekea kwenye amani (na suluhu) hiyo na mtegemee Allah. Hakika, yeye (Allah) ndiye Mwenye kusikia, Mwenye kujua



Sourate: ATTAUBA 

Verset : 105

وَقُلِ ٱعۡمَلُواْ فَسَيَرَى ٱللَّهُ عَمَلَكُمۡ وَرَسُولُهُۥ وَٱلۡمُؤۡمِنُونَۖ وَسَتُرَدُّونَ إِلَىٰ عَٰلِمِ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na sema (uwaambie wanaotubu na wengineo): Tendeni amali (kwa ikhlasi). Allah, na Mtume wake, na Waumini wataziona amali zenu. Na mtarudishwa kwa (Allah) Mwenye kujua siri na dhahiri; Naye atakuambieni yote mliyokuwa mnayatenda



Sourate: HUUD 

Verset : 112

فَٱسۡتَقِمۡ كَمَآ أُمِرۡتَ وَمَن تَابَ مَعَكَ وَلَا تَطۡغَوۡاْۚ إِنَّهُۥ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Basi, simama imara kama ulivyo amrishwa, na wale waliotubu pamoja na wewe, na msichupe mipaka. Hakika Yeye anayaona yote myatendayo



Sourate: AL-ISRAA 

Verset : 96

قُلۡ كَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ إِنَّهُۥ كَانَ بِعِبَادِهِۦ خَبِيرَۢا بَصِيرٗا

Sema: Allah anatosha kuwa Shahidi baina yangu na nyinyi. Hakika Yeye anawajua vyema waja wake na anawaona



Sourate: AL-KAHF 

Verset : 26

قُلِ ٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا لَبِثُواْۖ لَهُۥ غَيۡبُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ أَبۡصِرۡ بِهِۦ وَأَسۡمِعۡۚ مَا لَهُم مِّن دُونِهِۦ مِن وَلِيّٖ وَلَا يُشۡرِكُ فِي حُكۡمِهِۦٓ أَحَدٗا

Sema: Allah anajua zaidi muda walio kaa. Ni zake tu siri za mbingu na ardhi. Kuona kulioje na kusikia kwake! Hawana mlinzi isipo kuwa Yeye, wala hamshirikishi yeyote katika hukumu yake



Sourate: TWAHA 

Verset : 46

قَالَ لَا تَخَافَآۖ إِنَّنِي مَعَكُمَآ أَسۡمَعُ وَأَرَىٰ

Akasema: Msiogope! Hakika Mimi nipo pamoja nanyi. Nasikia na ninaona



Sourate: AL-HAJJ 

Verset : 75

ٱللَّهُ يَصۡطَفِي مِنَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ رُسُلٗا وَمِنَ ٱلنَّاسِۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعُۢ بَصِيرٞ

Allah huteuwa Wajumbe mion-goni mwa Malaika na miongoni mwa watu. Hakika Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona



Sourate: ALFURQAAN 

Verset : 20

وَمَآ أَرۡسَلۡنَا قَبۡلَكَ مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ إِلَّآ إِنَّهُمۡ لَيَأۡكُلُونَ ٱلطَّعَامَ وَيَمۡشُونَ فِي ٱلۡأَسۡوَاقِۗ وَجَعَلۡنَا بَعۡضَكُمۡ لِبَعۡضٖ فِتۡنَةً أَتَصۡبِرُونَۗ وَكَانَ رَبُّكَ بَصِيرٗا

Na hatukuwatuma kabla yako Mitume wowote ila kwa hakika na yakini walikuwa wakila chakula, na wakaenda masokoni. Na tumewajaalia baadhi yenu wawe ni majaribio kwa wengine; je! Mtasubiri? Na Mola wako Mlezi ni Mwenye kuona



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 217

وَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

Na umtegemee Mtukufu Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 218

ٱلَّذِي يَرَىٰكَ حِينَ تَقُومُ

Ambaye anakuona unapo simama,



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 219

وَتَقَلُّبَكَ فِي ٱلسَّـٰجِدِينَ

Na mageuko yako kati ya wanao sujudu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 220

إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Yeye ndiye Mwenye kusikia Mwenye kujua



Sourate: FAATWIR 

Verset : 31

وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ هُوَ ٱلۡحَقُّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ بِعِبَادِهِۦ لَخَبِيرُۢ بَصِيرٞ

Na hayo tuliyo kufunulia kutoka Kitabuni ni Kweli yenye kusadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Hakika Allah kwa waja wake ni Mwenye khabari na Mwenye kuona



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 40

إِنَّ ٱلَّذِينَ يُلۡحِدُونَ فِيٓ ءَايَٰتِنَا لَا يَخۡفَوۡنَ عَلَيۡنَآۗ أَفَمَن يُلۡقَىٰ فِي ٱلنَّارِ خَيۡرٌ أَم مَّن يَأۡتِيٓ ءَامِنٗا يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ ٱعۡمَلُواْ مَا شِئۡتُمۡ إِنَّهُۥ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٌ

Hakika wale wanao upotoa ukweli uliomo katika Ishara zetu hawatufichikii Sisi. Je! Atakaye tupwa Motoni ni bora au atakaye kuja kwa amani Siku ya Kiyama? Tendeni mpendavyo, kwa hakika Yeye anayaona mnayo yatenda



Sourate: ASH-SHUURAA 

Verset : 11

فَاطِرُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ جَعَلَ لَكُم مِّنۡ أَنفُسِكُمۡ أَزۡوَٰجٗا وَمِنَ ٱلۡأَنۡعَٰمِ أَزۡوَٰجٗا يَذۡرَؤُكُمۡ فِيهِۚ لَيۡسَ كَمِثۡلِهِۦ شَيۡءٞۖ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡبَصِيرُ

Yeye ndiye Muumba mbingu na ardhi, amekujaalieni mke na mume katika nafsi zenu, na katika wanyama hoa (wa kufugwa) dume na jike, anakuzidishieni namna hii. Hakuna chochote mfano wake. Naye ni Mwenye kusikia Mwenye kuona



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 80

أَمۡ يَحۡسَبُونَ أَنَّا لَا نَسۡمَعُ سِرَّهُمۡ وَنَجۡوَىٰهُمۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيۡهِمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong’ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika



Sourate: AL-HUJURAAT 

Verset : 18

إِنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ غَيۡبَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Hakika Allah anavijua visivyoonekana mbingni na ardhini, na Allah anayaona yote mnayofanya



Sourate: AL-MUJAADILA 

Verset : 1

قَدۡ سَمِعَ ٱللَّهُ قَوۡلَ ٱلَّتِي تُجَٰدِلُكَ فِي زَوۡجِهَا وَتَشۡتَكِيٓ إِلَى ٱللَّهِ وَٱللَّهُ يَسۡمَعُ تَحَاوُرَكُمَآۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعُۢ بَصِيرٌ

Hakika, Allah amekwishasikia kauli ya yule mwanamke anayejadiliana nawe (ewe Muhammad) kuhusu mumewe, na anamshitakia Allah, na Allah anayasikia majibizano yenu. Hakika, Allah ni Mwenye kusikia yote, Mwenye kuona yote



Sourate: AL-MULK 

Verset : 19

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ إِلَى ٱلطَّيۡرِ فَوۡقَهُمۡ صَـٰٓفَّـٰتٖ وَيَقۡبِضۡنَۚ مَا يُمۡسِكُهُنَّ إِلَّا ٱلرَّحۡمَٰنُۚ إِنَّهُۥ بِكُلِّ شَيۡءِۭ بَصِيرٌ

Je, hawawaoni ndege juu yao, wakiwa wakikunjua na kukunja (mbawa zao) hakuna anayewashikilia isipokuwa Allah mwingi wa Rehema, hakika Yeye ni Mwenye kuona kila kitu