Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 10

لَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكُمۡ كِتَٰبٗا فِيهِ ذِكۡرُكُمۡۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na hakika tumekuteremshieni Kitabu ambacho ndani yake umo ukumbusho wenu. Je! Hamzingatii?



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 50

وَهَٰذَا ذِكۡرٞ مُّبَارَكٌ أَنزَلۡنَٰهُۚ أَفَأَنتُمۡ لَهُۥ مُنكِرُونَ

Na huu ni ukumbusho ulio barikiwa, tulio uteremsha. Basi je! Mnaukataa?



Sourate: AL-HAJJ 

Verset : 16

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلۡنَٰهُ ءَايَٰتِۭ بَيِّنَٰتٖ وَأَنَّ ٱللَّهَ يَهۡدِي مَن يُرِيدُ

Na namna hivi tumeiteremsha (Qur’ani) kuwa ni Aya zilizo wazi, na hakika Allah humwongoa amtakaye



Sourate: ANNUUR 

Verset : 34

وَلَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكُمۡ ءَايَٰتٖ مُّبَيِّنَٰتٖ وَمَثَلٗا مِّنَ ٱلَّذِينَ خَلَوۡاْ مِن قَبۡلِكُمۡ وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ

Na kwa yakini tumekute-remshieni Ishara zilizo wazi na mifano kutokana na walio tangulia kabla yenu na mawaidha kwa wacha Mungu



Sourate: ANNUUR 

Verset : 46

لَّقَدۡ أَنزَلۡنَآ ءَايَٰتٖ مُّبَيِّنَٰتٖۚ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Kwa yakini tumeteremsha Ishara zinazo bainisha. Na Allah hummwongoa amtakaye kwenye Njia Iliyo Nyooka



Sourate: ALFURQAAN 

Verset : 6

قُلۡ أَنزَلَهُ ٱلَّذِي يَعۡلَمُ ٱلسِّرَّ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ إِنَّهُۥ كَانَ غَفُورٗا رَّحِيمٗا

Sema: Ameyateremsha haya ajuaye siri za katika mbingu na ardhi. Hakika Yeye ni Mwenye kusamehe Mwenye kurehemu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 192

وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na bila ya shaka huu ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 193

نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ

Ameuteremsha Roho mua-minifu,(jibril)



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 194

عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ

Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 195

بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ

Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi



Sourate: AL-QASWAS 

Verset : 86

وَمَا كُنتَ تَرۡجُوٓاْ أَن يُلۡقَىٰٓ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبُ إِلَّا رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۖ فَلَا تَكُونَنَّ ظَهِيرٗا لِّلۡكَٰفِرِينَ

Nawe hukuwa unataraji kuletewa Kitabu; lakini ni rehema tu ya Mola wako Mlezi. Basi usiwe msaidizi wa makafiri



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 51

أَوَلَمۡ يَكۡفِهِمۡ أَنَّآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ يُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَرَحۡمَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ

Je! Kwani hayakuwatosha ya kwamba tumekuteremshia Kitabu hiki wanacho somewa? Hakika katika hayo zipo rehema na mawaidha kwa watu wanao amini



Sourate: ASSAJDAH 

Verset : 2

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ لَا رَيۡبَ فِيهِ مِن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kisichokuwa na shaka yoyote kutoka kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: FAATWIR 

Verset : 31

وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ هُوَ ٱلۡحَقُّ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ بِعِبَادِهِۦ لَخَبِيرُۢ بَصِيرٞ

Na hayo tuliyo kufunulia kutoka Kitabuni ni Kweli yenye kusadikisha yaliyo kuwa kabla yake. Hakika Allah kwa waja wake ni Mwenye khabari na Mwenye kuona



Sourate: YAASIIN 

Verset : 5

تَنزِيلَ ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

(Ni) Uteremsho wa (Allah) Mwenye nguvu kubwa, Mwenye kurehemu sana



Sourate: SWAAD 

Verset : 29

كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ إِلَيۡكَ مُبَٰرَكٞ لِّيَدَّبَّرُوٓاْ ءَايَٰتِهِۦ وَلِيَتَذَكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Na hiki Kitabu, tumekuteremshia wewe, chenye baraka, ili wazizingatie Aya zake, na wawaidhike wenye akili



Sourate: AZZUMAR 

Verset : 1

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ مِنَ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡحَكِيمِ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allah, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Sourate: AZZUMAR 

Verset : 2

إِنَّآ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ فَٱعۡبُدِ ٱللَّهَ مُخۡلِصٗا لَّهُ ٱلدِّينَ

Hakika, sisi tumekuteremshia Kitabu (hiki) kwa haki. Basi muabudu Allah ukimsafia Dini Yeye tu



Sourate: AZZUMAR 

Verset : 23

ٱللَّهُ نَزَّلَ أَحۡسَنَ ٱلۡحَدِيثِ كِتَٰبٗا مُّتَشَٰبِهٗا مَّثَانِيَ تَقۡشَعِرُّ مِنۡهُ جُلُودُ ٱلَّذِينَ يَخۡشَوۡنَ رَبَّهُمۡ ثُمَّ تَلِينُ جُلُودُهُمۡ وَقُلُوبُهُمۡ إِلَىٰ ذِكۡرِ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ هُدَى ٱللَّهِ يَهۡدِي بِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَمَا لَهُۥ مِنۡ هَادٍ

Allah ameteremsha hadithi nzuri kabisa, Kitabu chenye kufanana na kukaririwa; husisimua ngozi za wenye kumkhofu Mola wao Mlezi. Kisha ngozi zao na nyoyo zao hulainika kwa kumkumbuka Allah. Huo ndio mwongozo wa Allah, na kwa huo humwongoa amtakaye. Na ambaye ameachwa na Allah kupotea, basi hapana wa kumwongoa



Sourate: AZZUMAR 

Verset : 41

إِنَّآ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡكِتَٰبَ لِلنَّاسِ بِٱلۡحَقِّۖ فَمَنِ ٱهۡتَدَىٰ فَلِنَفۡسِهِۦۖ وَمَن ضَلَّ فَإِنَّمَا يَضِلُّ عَلَيۡهَاۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِوَكِيلٍ

Hakika Sisi tumekuteremshia Kitabu kwa ajili ya watu wote kwa Haki. Basi mwenye kuongoka ni kwa nafsi yake, na mwenye kupotoka bila ya shaka amepotoka kwa hasara yake. Na wewe si mlinzi juu yao



Sourate: GHAAFIR 

Verset : 2

تَنزِيلُ ٱلۡكِتَٰبِ مِنَ ٱللَّهِ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡعَلِيمِ

(Huu) Ni uteremsho wa Kitabu kutoka kwa Allah, Mwenye nguvu kubwa, Mwenye kujua



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 2

تَنزِيلٞ مِّنَ ٱلرَّحۡمَٰنِ ٱلرَّحِيمِ

(Huu) Ni uteremsho utokao kwa (Allah) Mwingi wa rehema, Mwenye kurehemu



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 3

كِتَٰبٞ فُصِّلَتۡ ءَايَٰتُهُۥ قُرۡءَانًا عَرَبِيّٗا لِّقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

(Hiki) Ni Kitabu kilicho fafanu-liwa Aya zake, kikiwa (ni) Qur’ani, cha (lugha ya) Kiarabu kwa ajili ya watu wanaojua (wenye elimu)



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 4

بَشِيرٗا وَنَذِيرٗا فَأَعۡرَضَ أَكۡثَرُهُمۡ فَهُمۡ لَا يَسۡمَعُونَ

Kitoacho habari njema na chenye kuonya. Basi wengi wao wamepuuza; kwa hivyo hawasikii



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 41

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِٱلذِّكۡرِ لَمَّا جَآءَهُمۡۖ وَإِنَّهُۥ لَكِتَٰبٌ عَزِيزٞ

Kwa hakika wanaoyakataa mawaidha haya yanapo wajia (wataangamia), na hakika bila ya shaka ni Kitabu chenye nguvu na utukufu



Sourate: FUSSWILAT 

Verset : 42

لَّا يَأۡتِيهِ ٱلۡبَٰطِلُ مِنۢ بَيۡنِ يَدَيۡهِ وَلَا مِنۡ خَلۡفِهِۦۖ تَنزِيلٞ مِّنۡ حَكِيمٍ حَمِيدٖ

Hautakifikia upotovu mbele yake wala nyuma yake. Kimeteremshwa na Mwenye hekima, Msifiwa



Sourate: ASH-SHUURAA 

Verset : 17

ٱللَّهُ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ وَٱلۡمِيزَانَۗ وَمَا يُدۡرِيكَ لَعَلَّ ٱلسَّاعَةَ قَرِيبٞ

Allah ndiye aliye teremsha Kitabu kwa Haki, na Mizani. Na nini kitakacho kujuulisha ya kwamba pengine Saa ya Kiyama ipo karibu?



Sourate: ASH-SHUURAA 

Verset : 52

وَكَذَٰلِكَ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ رُوحٗا مِّنۡ أَمۡرِنَاۚ مَا كُنتَ تَدۡرِي مَا ٱلۡكِتَٰبُ وَلَا ٱلۡإِيمَٰنُ وَلَٰكِن جَعَلۡنَٰهُ نُورٗا نَّهۡدِي بِهِۦ مَن نَّشَآءُ مِنۡ عِبَادِنَاۚ وَإِنَّكَ لَتَهۡدِيٓ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Na namna hivi tumekufunulia Qur’ani kwa amri yetu. Ulikuwa hujui Kitabu ni nini, wala Imani. Lakini tumekifanya kuwa ni Nuru ambayo kwayo tunamwongoa tumtakaye katika waja wetu. Na hakika wewe unaongoa kwenye Njia Iliyo Nyooka



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 1

حمٓ

Haamiim



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 2

وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Nina apa kwa Kitabu kinacho-bainisha