فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ
Katika kizazi kilichoridhiwa mbele ya Mfalme aliye Muweza
Partager :
وَلِمَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ جَنَّتَانِ
Na kwa mwenye kukhofu kusi-mamishwa mbele ya Mola wake atapata bustani mbili
وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ
Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]
1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.
أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ
Hao ndio watakao kurubishwa
فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
katika pepo zenye neema
إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ عِندَ رَبِّهِمۡ جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ
Hakika wachamungu watapata Kwa Mola wao Bustani za neema
ٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ دَآئِمُونَ
Ambao wenye kudumisha Sala zao
وَٱلَّذِينَ فِيٓ أَمۡوَٰلِهِمۡ حَقّٞ مَّعۡلُومٞ
Na wale ambao katika Mali zao kuna haki maalumu
لِّلسَّآئِلِ وَٱلۡمَحۡرُومِ
Kwa (Masikini) mwenye kuomba na anaye jizuilia kuomba
وَٱلَّذِينَ يُصَدِّقُونَ بِيَوۡمِ ٱلدِّينِ
Na ambao wanasadikisha Siku ya Malipo, (siku ya Kiyama)
وَٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ عَذَابِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ
Na ambao wanaiogopa adhabu itokayo kwa Mola wao
إِنَّ عَذَابَ رَبِّهِمۡ غَيۡرُ مَأۡمُونٖ
Hakika adhabu ya Mola wao si ya kusalimika nayo
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِفُرُوجِهِمۡ حَٰفِظُونَ
Na ambao wanahifadhi tupu zao
إِلَّا عَلَىٰٓ أَزۡوَٰجِهِمۡ أَوۡ مَا مَلَكَتۡ أَيۡمَٰنُهُمۡ فَإِنَّهُمۡ غَيۡرُ مَلُومِينَ
Isipokuwa kwa wake zao, au wale iliyowamiliki mikono yao ya kuume, basi hao si wenye kulaumiwa
فَمَنِ ٱبۡتَغَىٰ وَرَآءَ ذَٰلِكَ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡعَادُونَ
Basi yeyote yule atakayetaka kinyume ya hayo, basi hao ndio warukao mipaka
وَٱلَّذِينَ هُمۡ لِأَمَٰنَٰتِهِمۡ وَعَهۡدِهِمۡ رَٰعُونَ
Na ambao amana zao na ahadi zao ni wenye kuzichunga (na kuzitimiza)
وَٱلَّذِينَ هُم بِشَهَٰدَٰتِهِمۡ قَآئِمُونَ
Na ambao wanasimama imara katika kutoa ushahidi wao,
وَٱلَّذِينَ هُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ
Na ambao kwenye Sala zao ni wenye kuzilinda
أُوْلَـٰٓئِكَ فِي جَنَّـٰتٖ مُّكۡرَمُونَ
Hao ndio watakao heshimiwa Peponi
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي ظِلَٰلٖ وَعُيُونٖ
Hakika wacha Mungu watakuwa katika vivuli na chemchem
وَفَوَٰكِهَ مِمَّا يَشۡتَهُونَ
Na matunda katika yale wanayoyatamani
كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
(Wataabiwa): Kuleni na kunyweni kwa furaha kwasababu ya yale mliyokuwa mkiyatenda
إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Hakika sisi ndio kama hivyo tunavyo walipa watendao mema
وَأَمَّا مَنۡ خَافَ مَقَامَ رَبِّهِۦ وَنَهَى ٱلنَّفۡسَ عَنِ ٱلۡهَوَىٰ
Ama yule anayeogopa kusimamishwa mbele ya Mola wake, na akaikataza nafsi yake na na matamanio
فَإِنَّ ٱلۡجَنَّةَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ
Basi huyo, Pepo itakuwa ndiyo makaazi yake!
إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ لَفِي نَعِيمٍ
Hakika watu wema bila ya shaka watakuwa katika neema
عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِ يَنظُرُونَ
Wakae juu ya viti vya enzi wakiangalia
تَعۡرِفُ فِي وُجُوهِهِمۡ نَضۡرَةَ ٱلنَّعِيمِ
Utatambua katika nyuso zao mng’aro wa neema,
إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡكَبِيرُ
Hakika walio amini na wakatenda mema watapata Bustani zenye mito ipitayo kati yake. Huko ndiko kufuzu kukubwa
يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ
Ewe nafsi iliyo tua!