Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Sourate: AL-HADIID

Verset : 21

سَابِقُوٓاْ إِلَىٰ مَغۡفِرَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ وَجَنَّةٍ عَرۡضُهَا كَعَرۡضِ ٱلسَّمَآءِ وَٱلۡأَرۡضِ أُعِدَّتۡ لِلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِٱللَّهِ وَرُسُلِهِۦۚ ذَٰلِكَ فَضۡلُ ٱللَّهِ يُؤۡتِيهِ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Kimbilieni kuomba msamaha kwa Mola wenu na Pepo (ambayo) upana wake ni kama upana wa mbingu na ardhi, imeandaliwa kwa wale walio muamini Allah na Mtume Wake. Hiyo ni fadhila ya Allah, Humpa Amtakaye. Na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Sourate: ALHAAQQA 

Verset : 22

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani (Pepo) Iliyo Juu,



Sourate: ALHAAQQA 

Verset : 23

قُطُوفُهَا دَانِيَةٞ

Vishada Vyake (vya matunda) Vitakuwa Karibu:



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 12

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُواْ جَنَّةٗ وَحَرِيرٗا

Na Atawalipa kwasababu ya kusubiri kwao, Pepo na nguo za hariri



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 13

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِۖ لَا يَرَوۡنَ فِيهَا شَمۡسٗا وَلَا زَمۡهَرِيرٗا

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona (hawatahisi) humo jua kali wala baridi kali.[1]


1- - Aya ni dalili kuwa Akhera kuna adhabu ya Baridi. Kama alivyopokea Imamu Bukhariy na Muslim- kutoka kwa Abuu Hurairah (Allah amuwiye radhh) amesema; amesema Mtume wa Allah (Rehema na amani ziwe juu yake):-


Sourate: AL-INSAAN

Verset : 14

وَدَانِيَةً عَلَيۡهِمۡ ظِلَٰلُهَا وَذُلِّلَتۡ قُطُوفُهَا تَذۡلِيلٗا

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning’inia mpaka chini



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 15

وَيُطَافُ عَلَيۡهِم بِـَٔانِيَةٖ مِّن فِضَّةٖ وَأَكۡوَابٖ كَانَتۡ قَوَارِيرَا۠

Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na bilauri zilokuwa za vigae



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 16

قَوَارِيرَاْ مِن فِضَّةٖ قَدَّرُوهَا تَقۡدِيرٗا

Vigae safi kutokana na fedha wamezipima kwa kipimo



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 17

وَيُسۡقَوۡنَ فِيهَا كَأۡسٗا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 18

عَيۡنٗا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلۡسَبِيلٗا

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 19

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيۡتَهُمۡ حَسِبۡتَهُمۡ لُؤۡلُؤٗا مَّنثُورٗا

Na watawazungukia wavulana wasio pevuka wakiwatumikia, ukiwaona utadhani ni lulu zilizo tawanywa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 20

وَإِذَا رَأَيۡتَ ثَمَّ رَأَيۡتَ نَعِيمٗا وَمُلۡكٗا كَبِيرًا

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 21

عَٰلِيَهُمۡ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضۡرٞ وَإِسۡتَبۡرَقٞۖ وَحُلُّوٓاْ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٖ وَسَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ شَرَابٗا طَهُورًا

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Sourate: ANNABAI 

Verset : 31

إِنَّ لِلۡمُتَّقِينَ مَفَازًا

Hakika wacha Mungu wanastahiki kufuzu



Sourate: ANNABAI 

Verset : 32

حَدَآئِقَ وَأَعۡنَٰبٗا

[watapata] Mabustani na mizabibu



Sourate: ANNABAI 

Verset : 33

وَكَوَاعِبَ أَتۡرَابٗا

Na wake wenye vifua vya kujaa, na walio lingana nao



Sourate: ANNABAI 

Verset : 34

وَكَأۡسٗا دِهَاقٗا

Na bilauri zilizo jaa,



Sourate: ANNABAI 

Verset : 35

لَّا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا كِذَّـٰبٗا

Hawatasikia humo upuuzi wala uongo



Sourate: ANNABAI 

Verset : 36

جَزَآءٗ مِّن رَّبِّكَ عَطَآءً حِسَابٗا

Hali yakuwa ni Malipo kutoka kwa Mola wako, ni kipawa cha kutosha



Sourate: AL-MUTWAFFIFIIN 

Verset : 25

يُسۡقَوۡنَ مِن رَّحِيقٖ مَّخۡتُومٍ

Watanyweshwa kinywaji safi kilichotiwa muhuri,



Sourate: AL-MUTWAFFIFIIN 

Verset : 26

خِتَٰمُهُۥ مِسۡكٞۚ وَفِي ذَٰلِكَ فَلۡيَتَنَافَسِ ٱلۡمُتَنَٰفِسُونَ

Muhuri wake ni miski. Na katika hayo washindanie wenye kushindana