Sourate: HUUD 

Verset : 43

قَالَ سَـَٔاوِيٓ إِلَىٰ جَبَلٖ يَعۡصِمُنِي مِنَ ٱلۡمَآءِۚ قَالَ لَا عَاصِمَ ٱلۡيَوۡمَ مِنۡ أَمۡرِ ٱللَّهِ إِلَّا مَن رَّحِمَۚ وَحَالَ بَيۡنَهُمَا ٱلۡمَوۡجُ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُغۡرَقِينَ

(Mtoto yule alimjibu baba yake): Nitakimbilia katika Jabali litanikinga na maji, (Nuhu) akasema: Leo hakuna wa kuikinga amri ya Allah ispokuwa yule tu (Allah) atamrehemu, na wimbi likaingia kati yao na akawa miongoni mwa waliogharikishwa



Sourate: HUUD 

Verset : 44

وَقِيلَ يَـٰٓأَرۡضُ ٱبۡلَعِي مَآءَكِ وَيَٰسَمَآءُ أَقۡلِعِي وَغِيضَ ٱلۡمَآءُ وَقُضِيَ ٱلۡأَمۡرُ وَٱسۡتَوَتۡ عَلَى ٱلۡجُودِيِّۖ وَقِيلَ بُعۡدٗا لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na pakasemwa: Ewe ardhi! Meza maji yako, na ewe mbingu jizuie, na maji yakazama, na jambo likamalizwa (kwa kuangamizwa watu wa Nuhu), na jahazi likasimama juu ya mlima judy. Na pakasemwa: Kuangamia kuwe kwa watu madhalimu



Sourate: HUUD 

Verset : 45

وَنَادَىٰ نُوحٞ رَّبَّهُۥ فَقَالَ رَبِّ إِنَّ ٱبۡنِي مِنۡ أَهۡلِي وَإِنَّ وَعۡدَكَ ٱلۡحَقُّ وَأَنتَ أَحۡكَمُ ٱلۡحَٰكِمِينَ

Na (hapo) Nuhu akamwita Mola wake mlezi akasema: Ee Mola wangu mlezi!(umeniahidi utaniokoa mimi na watu wangu), Hakika mwanangu ni katika watu wangu, na hakika ahadi yako ni haki (huendi kinyume na uliloahidi), nawe ni Hakimu uliye zaidi ya Mahakimu (Muadilifu wao)



Sourate: HUUD 

Verset : 46

قَالَ يَٰنُوحُ إِنَّهُۥ لَيۡسَ مِنۡ أَهۡلِكَۖ إِنَّهُۥ عَمَلٌ غَيۡرُ صَٰلِحٖۖ فَلَا تَسۡـَٔلۡنِ مَا لَيۡسَ لَكَ بِهِۦ عِلۡمٌۖ إِنِّيٓ أَعِظُكَ أَن تَكُونَ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

(Allah) akasema: Ewe Nuhu, hakika huyo si miongoni mwa watu wako (niliokuahidi kuwaokoa kwa sababu ya ukafiri wake); hakika ana matendo yasio mazuri. Basi usiniombe mambo usiyoyajua undani wake. Hakika mimi nakuwaidhi usije ukawa miongoni mwa wajinga



Sourate: HUUD 

Verset : 47

قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَعُوذُ بِكَ أَنۡ أَسۡـَٔلَكَ مَا لَيۡسَ لِي بِهِۦ عِلۡمٞۖ وَإِلَّا تَغۡفِرۡ لِي وَتَرۡحَمۡنِيٓ أَكُن مِّنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

(Nuhu) akasema: Ee Mola wangu, mlezi hakika ninajikinga kwako kukuomba jambo nisilolijua undani wake; Na endapo hutanisamehe na kunirehemu, nitakuwa miongoni mwa waliopata hasara



Sourate: HUUD 

Verset : 48

قِيلَ يَٰنُوحُ ٱهۡبِطۡ بِسَلَٰمٖ مِّنَّا وَبَرَكَٰتٍ عَلَيۡكَ وَعَلَىٰٓ أُمَمٖ مِّمَّن مَّعَكَۚ وَأُمَمٞ سَنُمَتِّعُهُمۡ ثُمَّ يَمَسُّهُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Pakasemwa: ewe Nuhu, teremka kwa salama (amani) itokayo kwetu, na baraka nyingi ziwe kwako na kwa watu walio pamoja nawe. Na hivi punde zitakuwepo kaumu nyingi za watu waovu tutawapa starehe, kisha itawashika kutoka kwetu adhabu iumizayo mno



Sourate: HUUD 

Verset : 49

تِلۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهَآ إِلَيۡكَۖ مَا كُنتَ تَعۡلَمُهَآ أَنتَ وَلَا قَوۡمُكَ مِن قَبۡلِ هَٰذَاۖ فَٱصۡبِرۡۖ إِنَّ ٱلۡعَٰقِبَةَ لِلۡمُتَّقِينَ

Hizo ni sehemu tu ya habari za ghaibu tunakufunulia. Hukuwa unazijua kabla ya hapa, sio wewe wala watu wako, Basi subiri, hakika mwisho (mwema) ni kwa wamchao Allah



Sourate: AL-ISRAA 

Verset : 3

ذُرِّيَّةَ مَنۡ حَمَلۡنَا مَعَ نُوحٍۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَبۡدٗا شَكُورٗا

Enyi kizazi tuliowachukua pamoja na Nuhu! Hakika yeye alikuwa mja mwenye shukrani



Sourate: MARYAM 

Verset : 58

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مِن ذُرِّيَّةِ ءَادَمَ وَمِمَّنۡ حَمَلۡنَا مَعَ نُوحٖ وَمِن ذُرِّيَّةِ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡرَـٰٓءِيلَ وَمِمَّنۡ هَدَيۡنَا وَٱجۡتَبَيۡنَآۚ إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُ ٱلرَّحۡمَٰنِ خَرُّواْۤ سُجَّدٗاۤ وَبُكِيّٗا۩

Hao ndio alio waneemesha Allah miongoni mwa Manabii katika uzao wa Adam, na katika uzao wa wale tulio wapandisha pamoja na Nuhu, na katika uzao wa Ibrahim na Israil, na katika wale tulio waongoa na tukawateuwa. Wanapo somewa Aya za Mwingi wa Rehema huanguka kusujudu na kulia



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 76

وَنُوحًا إِذۡ نَادَىٰ مِن قَبۡلُ فَٱسۡتَجَبۡنَا لَهُۥ فَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ

Na Nuhu alipo ita zamani, nasi tukamuitikia, na tukamuokoa yeye na watu wake kutokana na shida kubwa



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 77

وَنَصَرۡنَٰهُ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمَ سَوۡءٖ فَأَغۡرَقۡنَٰهُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na tukamnusuru kutokana na watu walio zikanusha Ishara zetu. Hakika hao walikuwa watu wabaya. Basi tukawazamisha wote



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 23

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ فَقَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ

Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu! Muabuduni Allah. Nyinyi hamna mungu asiye kuwa Yeye. Basi je! Hamuogopi?



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 24

فَقَالَ ٱلۡمَلَؤُاْ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَوۡمِهِۦ مَا هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُكُمۡ يُرِيدُ أَن يَتَفَضَّلَ عَلَيۡكُمۡ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَأَنزَلَ مَلَـٰٓئِكَةٗ مَّا سَمِعۡنَا بِهَٰذَا فِيٓ ءَابَآئِنَا ٱلۡأَوَّلِينَ

Walisema wale wakuu walio kufuru katika watu wake: Huyu si chochote ila ni mtu tu kama nyinyi. Anataka kujipa ubora juu yenu. Na lau kuwa Allah amependa basi angeli teremsha Malaika. Hatukusikia haya kwa baba zetu wa zamani



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 25

إِنۡ هُوَ إِلَّا رَجُلُۢ بِهِۦ جِنَّةٞ فَتَرَبَّصُواْ بِهِۦ حَتَّىٰ حِينٖ

Huyu si lolote ila ni mtu mwenye wazimu. Basi mngojeeni tu kwa muda



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 26

قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي بِمَا كَذَّبُونِ

Akasema (Nuhu): Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwa kuwa wamenikanusha



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 27

فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡهِ أَنِ ٱصۡنَعِ ٱلۡفُلۡكَ بِأَعۡيُنِنَا وَوَحۡيِنَا فَإِذَا جَآءَ أَمۡرُنَا وَفَارَ ٱلتَّنُّورُ فَٱسۡلُكۡ فِيهَا مِن كُلّٖ زَوۡجَيۡنِ ٱثۡنَيۡنِ وَأَهۡلَكَ إِلَّا مَن سَبَقَ عَلَيۡهِ ٱلۡقَوۡلُ مِنۡهُمۡۖ وَلَا تُخَٰطِبۡنِي فِي ٱلَّذِينَ ظَلَمُوٓاْ إِنَّهُم مُّغۡرَقُونَ

Tukampa ufunuo (wahyi tukamwambia: Unda jahazi chini ya uangalizi wetu na amri yetu na usaidizi wetu! Basi itakapo fika amri yetu na ikafurika tanuri, hapo waingize ndani yake wa kila namna dume na jike, na ahali zako, isipo kuwa yule ambaye katika wao juu yake imekwisha tangulia kauli. Wala usinitajie hao walio dhulumu. Kwani hao bila ya shaka watazamishwa



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 28

فَإِذَا ٱسۡتَوَيۡتَ أَنتَ وَمَن مَّعَكَ عَلَى ٱلۡفُلۡكِ فَقُلِ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي نَجَّىٰنَا مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Basi utakapo tulia wewe na walio pamoja nawe humo marikebuni, sema: Alhamdulillahi Sifa zote njema ni za Allah, aliye tuokoa na watu madhaalimu!



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 29

وَقُل رَّبِّ أَنزِلۡنِي مُنزَلٗا مُّبَارَكٗا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلۡمُنزِلِينَ

Na sema: Mola wangu Mlezi! Niteremshe mteremsho wenye baraka, na Wewe ni Mbora wa wateremshaji



Sourate: ALMUUMINUUN 

Verset : 30

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ وَإِن كُنَّا لَمُبۡتَلِينَ

Hakika katika hayo yapo mazingatio. Na kwa yakini Sisi ni wenye kuwafanyia mtihani



Sourate: ALFURQAAN 

Verset : 37

وَقَوۡمَ نُوحٖ لَّمَّا كَذَّبُواْ ٱلرُّسُلَ أَغۡرَقۡنَٰهُمۡ وَجَعَلۡنَٰهُمۡ لِلنَّاسِ ءَايَةٗۖ وَأَعۡتَدۡنَا لِلظَّـٰلِمِينَ عَذَابًا أَلِيمٗا

Na watu wa Nuhu, walipo wakanusha Mitume, tuliwazamisha, na tukawafanya ni Ishara kwa watu. Na tumewaandalia wenye kudhulumu adhabu chungu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 105

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ نُوحٍ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kaumu ya Nuhu waliwakadhibisha Mitume



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 106

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ نُوحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipowaambia ndugu yao, Nuhu: Je! Hamumuogopi Allah?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 107

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 108

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Allah, na nitiini mimi



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 109

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na sikutakini juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 110

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi Mcheni Allah, na nitiini mimi



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 111

۞قَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لَكَ وَٱتَّبَعَكَ ٱلۡأَرۡذَلُونَ

Wakasema: Je! Tukuamini wewe, hali wanaokufuata ni watu wa chini?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 112

قَالَ وَمَا عِلۡمِي بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Akasema: Nayajuaje waliyo kuwa wakiyafanya?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 113

إِنۡ حِسَابُهُمۡ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّيۖ لَوۡ تَشۡعُرُونَ

Hesabu yao haiko ila kwa Mola wao Mlezi, laiti mngeli tambua!



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 114

وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wala mimi si wa kuwafukuza Waumini