Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 12

قَالَ رَبِّ إِنِّيٓ أَخَافُ أَن يُكَذِّبُونِ

Akasema: Hakika mimi nachelea wasinikanushe



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 13

وَيَضِيقُ صَدۡرِي وَلَا يَنطَلِقُ لِسَانِي فَأَرۡسِلۡ إِلَىٰ هَٰرُونَ

Na kifua changu kina dhiki, na ulimi wangu haukunjuki vyema. Basi mtumie ujumbe Harun



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 14

وَلَهُمۡ عَلَيَّ ذَنۢبٞ فَأَخَافُ أَن يَقۡتُلُونِ

Na wao wana kisasi juu yangu, kwahivyo naogopa wasije kuniuwa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 15

قَالَ كَلَّاۖ فَٱذۡهَبَا بِـَٔايَٰتِنَآۖ إِنَّا مَعَكُم مُّسۡتَمِعُونَ

Akasema: Siyo hivyo kabisa! Nendeni na miujiza yetu. Hakika Sisi tu pamoja nanyi, tunasikiliza



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 16

فَأۡتِيَا فِرۡعَوۡنَ فَقُولَآ إِنَّا رَسُولُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi mfikieni Firauni na mwambieni: Hakika sisi ni Mitume wa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 17

أَنۡ أَرۡسِلۡ مَعَنَا بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Waachilie Wana wa Israili waende nasi



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 18

قَالَ أَلَمۡ نُرَبِّكَ فِينَا وَلِيدٗا وَلَبِثۡتَ فِينَا مِنۡ عُمُرِكَ سِنِينَ

(Firauni) akasema: Sisi hatukukulea wewe utotoni, na ukakaa kwetu katika umri wako miaka mingi?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 19

وَفَعَلۡتَ فَعۡلَتَكَ ٱلَّتِي فَعَلۡتَ وَأَنتَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na ukatenda kitendo chako ulicho tenda, nawe ukawa miongoni mwa wasio na shukrani?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 20

قَالَ فَعَلۡتُهَآ إِذٗا وَأَنَا۠ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

(Mussa) akasema: Nilitenda hayo hapo nilipo kuwa miongoni mwa wale walio potea



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 21

فَفَرَرۡتُ مِنكُمۡ لَمَّا خِفۡتُكُمۡ فَوَهَبَ لِي رَبِّي حُكۡمٗا وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Basi nikakumbieni nilipokuo-gopeni tena Mola wangu mlezi akanitunukia hukumu, na akanijaalia niwe miongoni mwa mitume



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 22

وَتِلۡكَ نِعۡمَةٞ تَمُنُّهَا عَلَيَّ أَنۡ عَبَّدتَّ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Na hiyo ndiyo neema ya kuni-sumbulia, na wewe umewatia utumwani Wana wa Israili?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 23

قَالَ فِرۡعَوۡنُ وَمَا رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Firauni akasema: Ni nani huyo Mola Mlezi wa walimwengu wote?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 24

قَالَ رَبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Akasema: Ndiye Mola Mlezi wa mbingu na ardhi, na vilivyomo baina yao, ikiwa nyinyi ni wenye yakini



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 25

قَالَ لِمَنۡ حَوۡلَهُۥٓ أَلَا تَسۡتَمِعُونَ

(Firauni) akawaambia walio mzunguka: Hamsikilizi?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 26

قَالَ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

(Mussa) akasema: Ndiye Mola wenu Mlezi, na Mola Mlezi wa baba zenu wa kwanza



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 27

قَالَ إِنَّ رَسُولَكُمُ ٱلَّذِيٓ أُرۡسِلَ إِلَيۡكُمۡ لَمَجۡنُونٞ

(Firauni) akasema: Hakika huyu Mtume wenu aliye tumwa kwenu ni mwendawazimu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 28

قَالَ رَبُّ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡقِلُونَ

(Mussa) akasema: Ndiye Mola Mlezi wa Mashariki na Magharibi na vilivyomo baina yao, ikiwa nyinyi mnatia akilini



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 29

قَالَ لَئِنِ ٱتَّخَذۡتَ إِلَٰهًا غَيۡرِي لَأَجۡعَلَنَّكَ مِنَ ٱلۡمَسۡجُونِينَ

(Firauni) akasema: Ukimfuata mungu mwengine asiye kuwa mimi, basi bila ya shaka nitakufunga gerezani



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 30

قَالَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكَ بِشَيۡءٖ مُّبِينٖ

Akasema: Je! Ijapokuwa nitakuletea kitu cha kubainisha wazi?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 31

قَالَ فَأۡتِ بِهِۦٓ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Akasema: Kilete basi, kama wewe ni katika wasemao kweli



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 32

فَأَلۡقَىٰ عَصَاهُ فَإِذَا هِيَ ثُعۡبَانٞ مُّبِينٞ

Basi akaitupa fimbo yake, mara ikawa nyoka wa kuonekana dhaahiri



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 33

وَنَزَعَ يَدَهُۥ فَإِذَا هِيَ بَيۡضَآءُ لِلنَّـٰظِرِينَ

Na akautoa mkono wake, na mara ukawa mweupe kwa watazamao



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 34

قَالَ لِلۡمَلَإِ حَوۡلَهُۥٓ إِنَّ هَٰذَا لَسَٰحِرٌ عَلِيمٞ

(Firauni) akawaambia waheshimiwa walio mzunguka: Hakika huyu ni mchawi mtaalamu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 35

يُرِيدُ أَن يُخۡرِجَكُم مِّنۡ أَرۡضِكُم بِسِحۡرِهِۦ فَمَاذَا تَأۡمُرُونَ

Anataka kukutoeni katika nchi yenu kwa uchawi wake. Basi mna shauri gani?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 36

قَالُوٓاْ أَرۡجِهۡ وَأَخَاهُ وَٱبۡعَثۡ فِي ٱلۡمَدَآئِنِ حَٰشِرِينَ

Wakasema: Mpe muda yeye na nduguye na uwatume mijini wapigao mbiu ya mgambo



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 37

يَأۡتُوكَ بِكُلِّ سَحَّارٍ عَلِيمٖ

Wakuletee kila mchawi bingwa mtaalamu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 38

فَجُمِعَ ٱلسَّحَرَةُ لِمِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ

Basi wakakusanywa wachawi wakati na siku maalumu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 39

وَقِيلَ لِلنَّاسِ هَلۡ أَنتُم مُّجۡتَمِعُونَ

Na watu wakaambiwa: Je! Mtakusanyika?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 40

لَعَلَّنَا نَتَّبِعُ ٱلسَّحَرَةَ إِن كَانُواْ هُمُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Huenda tutawafuata wachawi wakiwa wao ndio watakao shinda



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 41

فَلَمَّا جَآءَ ٱلسَّحَرَةُ قَالُواْ لِفِرۡعَوۡنَ أَئِنَّ لَنَا لَأَجۡرًا إِن كُنَّا نَحۡنُ ٱلۡغَٰلِبِينَ

Basi walipo kuja wachawi wakamwambia Firauni: Je! Tutapata ujira tukiwa sisi ndio tulio shinda?