Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 32

قَالَ إِنَّ فِيهَا لُوطٗاۚ قَالُواْ نَحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَن فِيهَاۖ لَنُنَجِّيَنَّهُۥ وَأَهۡلَهُۥٓ إِلَّا ٱمۡرَأَتَهُۥ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Akasema: Hakika humo yumo Lutwi. Wao wakasema: Sisi tunajua zaidi nani yumo humo. Hapana shaka tutamwokoa yeye na ahali zake, isipokuwa mkewe aliye miongoni mwa wataokaa nyuma



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 33

وَلَمَّآ أَن جَآءَتۡ رُسُلُنَا لُوطٗا سِيٓءَ بِهِمۡ وَضَاقَ بِهِمۡ ذَرۡعٗاۖ وَقَالُواْ لَا تَخَفۡ وَلَا تَحۡزَنۡ إِنَّا مُنَجُّوكَ وَأَهۡلَكَ إِلَّا ٱمۡرَأَتَكَ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ

Na wajumbe wetu walipo mfikia Lutwi, alihuzunika kwa ajili yao, na moyo uliona dhiki kwa ajili yao. Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongoni mwa wataokaa nyuma



Sourate: AL-ANKABUUT 

Verset : 34

إِنَّا مُنزِلُونَ عَلَىٰٓ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Kwa yakini sisi tutawateremshia watu wa mji huu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya uchafu wanao ufanya



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 133

وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Lutwi bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 134

إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tulipo mwokoa yeye na watu wake wote,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 135

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 136

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengineo



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 137

وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 138

وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 33

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطِۭ بِٱلنُّذُرِ

Wamekadhibisha Watu wa Luutwi Mitume waonyaji



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 34

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٖۖ نَّجَّيۡنَٰهُم بِسَحَرٖ

Hakika Sisi Tumewapelekea Upepo Uliyo Na Mchanga Ispokua Watu Wa Luutwi Waliyomuamini Tuliwaokoa Wakati Wa Theluthi Ya Mwisho Ya Usiku



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 35

نِّعۡمَةٗ مِّنۡ عِندِنَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي مَن شَكَرَ

Neema kutoka Kwetu, hivyo ndivyo Tunavyomlipa ambaye ameshukuru



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 36

وَلَقَدۡ أَنذَرَهُم بَطۡشَتَنَا فَتَمَارَوۡاْ بِٱلنُّذُرِ

Na Hakika Aliwaonya Kuhusiana Na Adhabu Yetu Wakatia Shaka Na Maonyo Hayo



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 37

وَلَقَدۡ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيۡفِهِۦ فَطَمَسۡنَآ أَعۡيُنَهُمۡ فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Na kwa yakini walimshawishi awape wageni wake, basi Tukawapofoa macho yao. Basi onjeni adhabu Yangu na maonyo Yangu



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 38

وَلَقَدۡ صَبَّحَهُم بُكۡرَةً عَذَابٞ مُّسۡتَقِرّٞ

Hakika Iliwafika Wao Adhabu Yenye Kudumu Asubuhi Mapema



Sourate: AL-QAMAR

Verset : 39

فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Onjeni Adhabu Yangu na Maonyo