Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 39

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na ambao wamekufuru na wakazikadhibisha Aya zetu, hao ni watu wa motoni, wataishi humo milele



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 86

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا بِٱلۡأٓخِرَةِۖ فَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Hao ndio walionunua uhai wa dunia kwa Akhera, kwahiyo hawatapunguziwa adhabu na wala hawatanusuriwa



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 161

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَمَاتُواْ وَهُمۡ كُفَّارٌ أُوْلَـٰٓئِكَ عَلَيۡهِمۡ لَعۡنَةُ ٱللَّهِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Hakika, waliokufuru na wakafa hali ni makafiri, hao wanastahiki laana ya Allah, na ya Malaika na (laana) ya watu wote



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 162

خَٰلِدِينَ فِيهَا لَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنظَرُونَ

Humo watakaa daima. Hawatapunguziwa adhabu na hawatapewa muda (wa kuomba radhi)



Sourate: ANNISAI 

Verset : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ يَأۡكُلُونَ أَمۡوَٰلَ ٱلۡيَتَٰمَىٰ ظُلۡمًا إِنَّمَا يَأۡكُلُونَ فِي بُطُونِهِمۡ نَارٗاۖ وَسَيَصۡلَوۡنَ سَعِيرٗا

Hakika wale wanaokula mali za Yatima kwa dhulma kwa hakika wanakula moto (kutia) matumboni mwao na watauingia Motoni



Sourate: ANNISAI 

Verset : 93

وَمَن يَقۡتُلۡ مُؤۡمِنٗا مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآؤُهُۥ جَهَنَّمُ خَٰلِدٗا فِيهَا وَغَضِبَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ وَلَعَنَهُۥ وَأَعَدَّ لَهُۥ عَذَابًا عَظِيمٗا

Na yeyote anayemuua Muumini (Muislamu) kwa kukusudia basi malipo yake ni Jahanamu, ataishi humo milele na Allah amemghadhibikia na amemlaani na amemuandalia adhabu kubwa kabisa



Sourate: ANNISAI 

Verset : 140

وَقَدۡ نَزَّلَ عَلَيۡكُمۡ فِي ٱلۡكِتَٰبِ أَنۡ إِذَا سَمِعۡتُمۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ يُكۡفَرُ بِهَا وَيُسۡتَهۡزَأُ بِهَا فَلَا تَقۡعُدُواْ مَعَهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦٓ إِنَّكُمۡ إِذٗا مِّثۡلُهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ جَامِعُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡكَٰفِرِينَ فِي جَهَنَّمَ جَمِيعًا

Na kwa hakika, (Allah) amekuteremshieni katika kitabu (Qur’ani) kwamba msikiapo Aya za Allah zinakanushwa na zinafanyiwa kejeli, basi msikae pamoja nao (hao wafanyao hivyo), mpaka waingie katika mazungumzo mengine[1]. Hakika, mkikaa nao nanyi mtakuwa kama wao. Hakika, Allah atawakusanya Wanafiki na Makafiri wote katika Jahanamu


1- - Allah ametaja suala hili katika Aya ya 68 ya Sura Al-an-aam (6) inayosema kwamba “Na ukiwaona wanaozisema vibaya Aya zetu usikae nao…”.


Sourate: ANNISAI 

Verset : 145

إِنَّ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ فِي ٱلدَّرۡكِ ٱلۡأَسۡفَلِ مِنَ ٱلنَّارِ وَلَن تَجِدَ لَهُمۡ نَصِيرًا

Hakika, wanafiki watakuwa katika tabaka la chini kabisa la Moto, na hutampata yeyote wa kuwanusuru



Sourate: AL-MAIDA 

Verset : 10

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ

Na waliokufuru na kuzikanusha Aya zetu (tulizoziteremsha kwa Mitume wetu), hao ndio watu wa Motoni



Sourate: AL-MAIDA 

Verset : 72

لَقَدۡ كَفَرَ ٱلَّذِينَ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ هُوَ ٱلۡمَسِيحُ ٱبۡنُ مَرۡيَمَۖ وَقَالَ ٱلۡمَسِيحُ يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبَّكُمۡۖ إِنَّهُۥ مَن يُشۡرِكۡ بِٱللَّهِ فَقَدۡ حَرَّمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِ ٱلۡجَنَّةَ وَمَأۡوَىٰهُ ٱلنَّارُۖ وَمَا لِلظَّـٰلِمِينَ مِنۡ أَنصَارٖ

Kwa hakika kabisa, wamekufuru waliosema: Hakika, Allah ni Masihi Mwana wa Mariamu. Na Masihi (mwenyewe) alisema: Enyi Wana wa Israili, muabuduni Allah, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Ilivyo ni kwamba, yeyote anayemfanyia ushirika Allah, hakika Allah amemharamishia Pepo, na makazi yake ni Motoni. Na madhalimu hawatakuwa na watetezi wowote



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 18

قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡهَا مَذۡءُومٗا مَّدۡحُورٗاۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Allah) Akasema (kumwambia Ibilisi kwamba): Toka humo (Peponi) ukiwa umechukiwa, umelaaniwa. Kwa yakini kabisa, yeyote atakayekufuata wewe miongoni mwao hakika nitaijaza Jahanamu kwa (kukutumbukizeni humo) nyinyi nyote



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 36

وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَٱسۡتَكۡبَرُواْ عَنۡهَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na wale waliokadhibisha Aya zetu na kuzifanyia kiburi hao ni watu wa motoni, watakaa humo milele



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 38

قَالَ ٱدۡخُلُواْ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ فِي ٱلنَّارِۖ كُلَّمَا دَخَلَتۡ أُمَّةٞ لَّعَنَتۡ أُخۡتَهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا ٱدَّارَكُواْ فِيهَا جَمِيعٗا قَالَتۡ أُخۡرَىٰهُمۡ لِأُولَىٰهُمۡ رَبَّنَا هَـٰٓؤُلَآءِ أَضَلُّونَا فَـَٔاتِهِمۡ عَذَابٗا ضِعۡفٗا مِّنَ ٱلنَّارِۖ قَالَ لِكُلّٖ ضِعۡفٞ وَلَٰكِن لَّا تَعۡلَمُونَ

(Allah) Atasema: Ingieni Motoni (nyinyi) pamoja na mataifa yaliyopita kabla yenu, ambao ni majini na watu. Kila umma unapoingia utawalaani (umma) ndugu yake (mwenzake) mpaka watakapokusanyika humo wote kwa pamoja, watasema wa mwisho wao (kuwashitaki) wa mwanzo wao (kwamba): “Ewe Mola wetu Mlezi, hawa ndio waliotupoteza, basi wape adhabu ya moto maradufu”. (Allah) Atasema: Kila mmoja wenu ana (adhabu) mara dufu na lakini hamjui



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 39

وَقَالَتۡ أُولَىٰهُمۡ لِأُخۡرَىٰهُمۡ فَمَا كَانَ لَكُمۡ عَلَيۡنَا مِن فَضۡلٖ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡسِبُونَ

Na watasema wa mwanzo wao kuwaambia wa mwisho wao (kwamba): Nyinyi hamkuwa na fadhila yoyote kwetu, basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyachuma



Sourate: ATTAUBA 

Verset : 63

أَلَمۡ يَعۡلَمُوٓاْ أَنَّهُۥ مَن يُحَادِدِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَأَنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدٗا فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡخِزۡيُ ٱلۡعَظِيمُ

Je, hawajui ya kwamba anayemfanyia uadui Allah na Mtume wake, basi huyo atapata Moto wa Jahanamu adumu humo? Hiyo ndiyo hasa hizaya kubwa kabisa



Sourate: ATTAUBA 

Verset : 68

وَعَدَ ٱللَّهُ ٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱلۡمُنَٰفِقَٰتِ وَٱلۡكُفَّارَ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ هِيَ حَسۡبُهُمۡۚ وَلَعَنَهُمُ ٱللَّهُۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ مُّقِيمٞ

Allah amewaahidi wanafiki wanaume na wanafiki wanawake na makafiri Moto wa Jahanamu wakidumu humo milele. Hilo ndilo linalowatosha, na Allah amewalaani na watapata adhabu ya kudumu



Sourate: HUUD 

Verset : 119

إِلَّا مَن رَّحِمَ رَبُّكَۚ وَلِذَٰلِكَ خَلَقَهُمۡۗ وَتَمَّتۡ كَلِمَةُ رَبِّكَ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Isipokuwa tu wale Mola wako mlezi amewarehemu (wakaamini); na Allah amewaumba hivyo. Na neno la Mola wako mlezi litatimia: Kwe hakika nitaijaza Jahannam miongoni mwa majini na watu wote kwa pamoja



Sourate: AL-ISRAA 

Verset : 18

مَّن كَانَ يُرِيدُ ٱلۡعَاجِلَةَ عَجَّلۡنَا لَهُۥ فِيهَا مَا نَشَآءُ لِمَن نُّرِيدُ ثُمَّ جَعَلۡنَا لَهُۥ جَهَنَّمَ يَصۡلَىٰهَا مَذۡمُومٗا مَّدۡحُورٗا

Anaye taka yapitayo upesi upesi, tutafanya haraka kumletea hapa hapa tunayo yataka kwa tumtakaye. Kisha tumemwekea Jahannamu; ataingia humo hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa na kufurushwa



Sourate: MARYAM 

Verset : 72

ثُمَّ نُنَجِّي ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْ وَّنَذَرُ ٱلظَّـٰلِمِينَ فِيهَا جِثِيّٗا

Kisha tutawaokoa wale walio mcha Allah; na tutawaacha mad-haalimu humo wamepiga magoti



Sourate: TWAHA 

Verset : 74

إِنَّهُۥ مَن يَأۡتِ رَبَّهُۥ مُجۡرِمٗا فَإِنَّ لَهُۥ جَهَنَّمَ لَا يَمُوتُ فِيهَا وَلَا يَحۡيَىٰ

Hakika atakayemjia Mola wake Mlezi naye ni muovu, basi kwa yakini, yake huyo ni Jahannamu. Hafi humo wala haishi



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 29

۞وَمَن يَقُلۡ مِنۡهُمۡ إِنِّيٓ إِلَٰهٞ مِّن دُونِهِۦ فَذَٰلِكَ نَجۡزِيهِ جَهَنَّمَۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na yeyote kati yao atakaye sema: Mimi ni mungu, badala yake, basi huyo tutamlipa malipo yake Jahannamu. Hivyo ndivyo tuwalipavyo wenye kudhulumu



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 98

إِنَّكُمۡ وَمَا تَعۡبُدُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ حَصَبُ جَهَنَّمَ أَنتُمۡ لَهَا وَٰرِدُونَ

Hakika nyinyi na hao mnao waabudu badala ya Allah ni kuni za Jahannamu; huko mtaingia tu



Sourate: AL-ANBIYAA 

Verset : 99

لَوۡ كَانَ هَـٰٓؤُلَآءِ ءَالِهَةٗ مَّا وَرَدُوهَاۖ وَكُلّٞ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wangekuwa hawa ni miungu, wasingeli ingia. Na wote watadumu humo



Sourate: AL-HAJJ 

Verset : 51

وَٱلَّذِينَ سَعَوۡاْ فِيٓ ءَايَٰتِنَا مُعَٰجِزِينَ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَحِيمِ

Na wanao jitahidi kuzipinga Aya zetu hao ndio watu wa Motoni



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 94

فَكُبۡكِبُواْ فِيهَا هُمۡ وَٱلۡغَاوُۥنَ

Basi watavurumizwa humo wao na hao wakosefu,



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 95

وَجُنُودُ إِبۡلِيسَ أَجۡمَعُونَ

Na majeshi ya Ibilisi yote



Sourate: AL-AHZAAB 

Verset : 64

إِنَّ ٱللَّهَ لَعَنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ وَأَعَدَّ لَهُمۡ سَعِيرًا

Hakika Allah amewalaani makafiri na amewaandalia Moto unao waka kwa nguvu



Sourate: AL-AHZAAB 

Verset : 65

خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ لَّا يَجِدُونَ وَلِيّٗا وَلَا نَصِيرٗا

Watadumu humo milele. Hawampati mlinzi wala wa kuwa-nusuru



Sourate: SWAAD 

Verset : 55

هَٰذَاۚ وَإِنَّ لِلطَّـٰغِينَ لَشَرَّ مَـَٔابٖ

Ndiyo hivi! Na hakika wenye kuasi bila ya shaka watapata marejeo mabaya kabisa;



Sourate: SWAAD 

Verset : 56

جَهَنَّمَ يَصۡلَوۡنَهَا فَبِئۡسَ ٱلۡمِهَادُ

Nayo ni Jahannamu! Wataingia humo. Nacho hicho ni kitanda kiovu mno cha kulalia