Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 40

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’ani kwaajili ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka.?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 41

وَلَقَدۡ جَآءَ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ ٱلنُّذُرُ

Hakika yaliwajia watu wafiraun maonyo



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 42

كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذۡنَٰهُمۡ أَخۡذَ عَزِيزٖ مُّقۡتَدِرٍ

Na kwa yakini watu wa Fir’awn walifikiwa na waonyaji



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 43

أَكُفَّارُكُمۡ خَيۡرٞ مِّنۡ أُوْلَـٰٓئِكُمۡ أَمۡ لَكُم بَرَآءَةٞ فِي ٱلزُّبُرِ

Je, makafiri wenu (enyi Maquraysh) ni bora kuliko hao (ummah) wa awali? Au mna msamaha katika Maandiko Tukufu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 44

أَمۡ يَقُولُونَ نَحۡنُ جَمِيعٞ مُّنتَصِرٞ

Au wanasema: Sisi ni wengi (kundi) tutashinda tu.?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 45

سَيُهۡزَمُ ٱلۡجَمۡعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ

Litashindwa kundi hilo na watakimbia



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 46

بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوۡعِدُهُمۡ وَٱلسَّاعَةُ أَدۡهَىٰ وَأَمَرُّ

Bali Kiyama Ndio Ahadi Yao Na Adhabu Ya Kiyama Kubwa Na Chungu Zaidi



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 47

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ

Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 48

يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ

Siku watakayoburutwa motoni kifudi fudi, Waambiwe: Onjeni mguso wa moto mkali mno



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 49

إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ

Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa Qadar (makadirio)



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 50

وَمَآ أَمۡرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٞ كَلَمۡحِۭ بِٱلۡبَصَرِ

Na amri Yetu haiwi ila ni moja tu, kama upepeso wa jicho



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 51

وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَآ أَشۡيَاعَكُمۡ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa yakini Tumewaangamiza wenzenu, je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 52

وَكُلُّ شَيۡءٖ فَعَلُوهُ فِي ٱلزُّبُرِ

Na yote waliyoyafanya yamehi-fadhiwa kwenye vitabu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 53

وَكُلُّ صَغِيرٖ وَكَبِيرٖ مُّسۡتَطَرٌ

Na kila kidogo na kikubwa kime-andikwa



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 54

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَهَرٖ

Hakika Waliomcha Allah watakua kwenye mabustani Na Mito



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 55

فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ

Katika kizazi kilichoridhiwa mbele ya Mfalme aliye Muweza



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 1

ٱلرَّحۡمَٰنُ

(Allah) Mwingi wa rehma



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 2

عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ

Amefundisha Qur’ani



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 3

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ

Amemumba mwanadamu



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 4

عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ

Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 5

ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ

Jua na mwezi (vinatembea) kwa hesabu (na mpangilio maalum)



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 6

وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ

Na nyota na miti vinasujudu



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 7

وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ

Na mbingu ameinyanyua na ameweka mizani (kuthibitisha uadilifu na usawa)



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 8

أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ

(Ameweka mizani) Ili msifanye dhulma katika upimaji



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 9

وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ

Na simamisheni mzani kwa uadilifu na msipunguze mizani



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 10

وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ

Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 11

فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ

Humo mna matunda na mitende yenye makole



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 12

وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ

Na punje (nafaka ) zenye majani (makapi) na harufu nzuri



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 13

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ

Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?



Capítulo: ARRAHMAAN 

Verso : 14

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ

Amemuumba mwanadamu kutokana na udongo utowao sauti kama vyombo vya udongo vilivyochomwa