Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 10

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَغۡلُوبٞ فَٱنتَصِرۡ

Basi akamwita Mola wake mlezi kwamba: Hakika mimi nimeshindwa (nimezidiwa nguvu) basi ni Nusuru



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 11

فَفَتَحۡنَآ أَبۡوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٖ مُّنۡهَمِرٖ

Tukafungua milango ya mbingu kwa maji yanayofoka na kumiminika kwa nguvu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 12

وَفَجَّرۡنَا ٱلۡأَرۡضَ عُيُونٗا فَٱلۡتَقَى ٱلۡمَآءُ عَلَىٰٓ أَمۡرٖ قَدۡ قُدِرَ

Na tukaipasua ardhi yote kwa chemchem, na yakakutana maji kwa pamoja kwa jambo lililokadiriwa



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 13

وَحَمَلۡنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلۡوَٰحٖ وَدُسُرٖ

Na Tukambeba kwenye ile (jahazi) yenye mbao na misumari



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 14

تَجۡرِي بِأَعۡيُنِنَا جَزَآءٗ لِّمَن كَانَ كُفِرَ

Kikienda haraka tukikitazama kwa macho yetu ikiwa ni malipo kwa ambaye alikuwa amekufuru



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 15

وَلَقَد تَّرَكۡنَٰهَآ ءَايَةٗ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa yakini Tumeiacha iwe ni mazingatio, Je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 16

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 17

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 18

كَذَّبَتۡ عَادٞ فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Kina ‘Aad walikadhibisha, basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 19

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِيحٗا صَرۡصَرٗا فِي يَوۡمِ نَحۡسٖ مُّسۡتَمِرّٖ

Hakika Sisi Tumewapelekea upepo wa kimbunga wenye sauti kali na baridi kali katika siku korofi yenye kuendelea mfululizo



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 20

تَنزِعُ ٱلنَّاسَ كَأَنَّهُمۡ أَعۡجَازُ نَخۡلٖ مُّنقَعِرٖ

Unawang’oa watu kana kwamba vigogo vya mtende vilong’olewa



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 21

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi vipi ilikuwa adhabu Yangu na maonyo Yangu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 22

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 23

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ بِٱلنُّذُرِ

Kina Thamuwd waliwakadhibisha Waonyaji



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 24

فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٗا مِّنَّا وَٰحِدٗا نَّتَّبِعُهُۥٓ إِنَّآ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٍ

Wakasema: Ah! Tumfuate binaadamu miongoni mwetu? Hakika hapo sisi tutakuwa katika upotofu na wazimu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 25

أَءُلۡقِيَ ٱلذِّكۡرُ عَلَيۡهِ مِنۢ بَيۡنِنَا بَلۡ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٞ

Ah! Ameteremshiwa ukumbusho (Wahyi) baina yetu? Bali yeye ni muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 26

سَيَعۡلَمُونَ غَدٗا مَّنِ ٱلۡكَذَّابُ ٱلۡأَشِرُ

Watakuja kujua kesho nani muongo mkubwa mwenye kiburi mno



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 27

إِنَّا مُرۡسِلُواْ ٱلنَّاقَةِ فِتۡنَةٗ لَّهُمۡ فَٱرۡتَقِبۡهُمۡ وَٱصۡطَبِرۡ

Hakika Sisi Tutawapelekea ngamia jike awe jaribio kwao, basi (Ee Nabiy Swaalih) watazame na vuta subira



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 28

وَنَبِّئۡهُمۡ أَنَّ ٱلۡمَآءَ قِسۡمَةُۢ بَيۡنَهُمۡۖ كُلُّ شِرۡبٖ مُّحۡتَضَرٞ

Na wajulishe kwamba maji ni mgawanyo baina yao (ngamia na wao), kila sehemu ya maji itahudhuriwa (kwa zamu)



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 29

فَنَادَوۡاْ صَاحِبَهُمۡ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ

Wakamuita Mtu Wao Akajipa Ushujaa Na Kumchinja



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 30

فَكَيۡفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Vipi Ilikua Adhabu Yangu Na Maonyo yangu?



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 31

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَكَانُواْ كَهَشِيمِ ٱلۡمُحۡتَظِرِ

Hakika Sisi Tulipeleka Kwao Ukelele Moja tu, wakawa kama mabuwa yaliyokatika-katika ya mtengenezaji zizi



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 32

وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na Hakika Tumeirahisisha Qur’an Kwa Ajili Ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 33

كَذَّبَتۡ قَوۡمُ لُوطِۭ بِٱلنُّذُرِ

Wamekadhibisha Watu wa Luutwi Mitume waonyaji



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 34

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ حَاصِبًا إِلَّآ ءَالَ لُوطٖۖ نَّجَّيۡنَٰهُم بِسَحَرٖ

Hakika Sisi Tumewapelekea Upepo Uliyo Na Mchanga Ispokua Watu Wa Luutwi Waliyomuamini Tuliwaokoa Wakati Wa Theluthi Ya Mwisho Ya Usiku



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 35

نِّعۡمَةٗ مِّنۡ عِندِنَاۚ كَذَٰلِكَ نَجۡزِي مَن شَكَرَ

Neema kutoka Kwetu, hivyo ndivyo Tunavyomlipa ambaye ameshukuru



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 36

وَلَقَدۡ أَنذَرَهُم بَطۡشَتَنَا فَتَمَارَوۡاْ بِٱلنُّذُرِ

Na Hakika Aliwaonya Kuhusiana Na Adhabu Yetu Wakatia Shaka Na Maonyo Hayo



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 37

وَلَقَدۡ رَٰوَدُوهُ عَن ضَيۡفِهِۦ فَطَمَسۡنَآ أَعۡيُنَهُمۡ فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Na kwa yakini walimshawishi awape wageni wake, basi Tukawapofoa macho yao. Basi onjeni adhabu Yangu na maonyo Yangu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 38

وَلَقَدۡ صَبَّحَهُم بُكۡرَةً عَذَابٞ مُّسۡتَقِرّٞ

Hakika Iliwafika Wao Adhabu Yenye Kudumu Asubuhi Mapema



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 39

فَذُوقُواْ عَذَابِي وَنُذُرِ

Basi Onjeni Adhabu Yangu na Maonyo