Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 39

وَمَا لَا تُبۡصِرُونَ

Na Naapa kwa yale msiyoyaona



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 40

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Kwa hakika hii (Qur’ani) ni kauli iliyo letwa na Mjumbe mwenye heshima



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 41

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَاعِرٖۚ قَلِيلٗا مَّا تُؤۡمِنُونَ

Wala si kauli ya mtunga mashairi. Ni machache sana mnayoyaamini



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 42

وَلَا بِقَوۡلِ كَاهِنٖۚ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Wala si kauli ya kuhani. Ni machache mnayo yakumbuka



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 43

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni Uteremsho Kutoka Kwa Mola Wa Viumbe Vyote



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 44

وَلَوۡ تَقَوَّلَ عَلَيۡنَا بَعۡضَ ٱلۡأَقَاوِيلِ

Na Kama (Mtume) Angelizua Juu Yetu Baadhi Ya Maneno tu,



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 45

لَأَخَذۡنَا مِنۡهُ بِٱلۡيَمِينِ

Bila ya shaka tungeli mshika kwa mkono wa kulia



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 46

ثُمَّ لَقَطَعۡنَا مِنۡهُ ٱلۡوَتِينَ

Kisha kwa hakika tungeli mkata mshipa mkubwa (wa moyo!)



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 47

فَمَا مِنكُم مِّنۡ أَحَدٍ عَنۡهُ حَٰجِزِينَ

Na hapana yeyote katika nyinyi ambaye angeli weza kutuzuia



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 48

وَإِنَّهُۥ لَتَذۡكِرَةٞ لِّلۡمُتَّقِينَ

Kwa hakika hii (Qur’ani) ni ukumbusho kwa wachamungu



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 49

وَإِنَّا لَنَعۡلَمُ أَنَّ مِنكُم مُّكَذِّبِينَ

Na hakika Sisi bila ya shaka tunajua kwamba miongoni mwenu wapo wanao kadhibisha



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 50

وَإِنَّهُۥ لَحَسۡرَةٌ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na hakika hii (Qur’ani) bila shaka itakuwa ni majuto makubwa juu ya makafiri



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 51

وَإِنَّهُۥ لَحَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Na hakika hii (Qur’an) ni haki ya yakini



Capítulo: ALHAAQQA 

Verso : 52

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litukuze jina la Mola Wako aliye Mkuu



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 1

سَأَلَ سَآئِلُۢ بِعَذَابٖ وَاقِعٖ

Muulizaji ameuliza kuhusu adhabu itakayotokea



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 2

لِّلۡكَٰفِرِينَ لَيۡسَ لَهُۥ دَافِعٞ

Kwa makafiri, hapana wa kuizuia



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 3

مِّنَ ٱللَّهِ ذِي ٱلۡمَعَارِجِ

Kutoka kwa Allah Mwenye madaraja ya juu (Mwenye mbingu za daraja)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 4

تَعۡرُجُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ إِلَيۡهِ فِي يَوۡمٖ كَانَ مِقۡدَارُهُۥ خَمۡسِينَ أَلۡفَ سَنَةٖ

Malaika na Roho (Jibrili) wanapanda kwenda kwake katika siku ambayo makadirio yake ni miaka hamsini elfu



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 5

فَٱصۡبِرۡ صَبۡرٗا جَمِيلًا

Basi subiri subira njema



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 6

إِنَّهُمۡ يَرَوۡنَهُۥ بَعِيدٗا

Hakika, wao wanaiona (siku hiyo) iko mbali



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 7

وَنَرَىٰهُ قَرِيبٗا

Nasi tunaiona iko karibu



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 8

يَوۡمَ تَكُونُ ٱلسَّمَآءُ كَٱلۡمُهۡلِ

Siku ambayo mbingu zitakuwa kama shaba iliyo yeyushwa



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 9

وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ

Na milima itakuwa kama sufi (iliyo chambuliwa)



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 10

وَلَا يَسۡـَٔلُ حَمِيمٌ حَمِيمٗا

Na rafiki hatomuuliza rafiki yake



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 11

يُبَصَّرُونَهُمۡۚ يَوَدُّ ٱلۡمُجۡرِمُ لَوۡ يَفۡتَدِي مِنۡ عَذَابِ يَوۡمِئِذِۭ بِبَنِيهِ

Watafanywa waonane. Mkosefu atatamani (kujikomboa) ajitolee fidia kutokana na adhabu Siku hiyo kwa kuwatoa watoto wake



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 12

وَصَٰحِبَتِهِۦ وَأَخِيهِ

Na mke wake na nduguye



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 13

وَفَصِيلَتِهِ ٱلَّتِي تُـٔۡوِيهِ

Na jamaa zake wa karibu ambao wanamlinda



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 14

وَمَن فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ يُنجِيهِ

Na (pia atatamani kutoa fidia kwa kulipa) vyote vilivyomo ardhini (duniani) kisha (ili) vimuokoe



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 15

كَلَّآۖ إِنَّهَا لَظَىٰ

Sio hivyo (Hayawezekani hayo). Kwa hakika, huo ni Moto mkali kabisa



Capítulo: ALMA’RIJ 

Verso : 16

نَزَّاعَةٗ لِّلشَّوَىٰ

Unaobabua kwa nguvu ngozi ya kichwani na mwilini