Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 11

فَوَقَىٰهُمُ ٱللَّهُ شَرَّ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمِ وَلَقَّىٰهُمۡ نَضۡرَةٗ وَسُرُورٗا

Basi Allah Atawakinga na shari ya siku hiyo, na Atawapa nuru na kuwakutanisha na uchangamfu na furaha



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 12

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُواْ جَنَّةٗ وَحَرِيرٗا

Na Atawalipa kwasababu ya kusubiri kwao, Pepo na nguo za hariri



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 13

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِۖ لَا يَرَوۡنَ فِيهَا شَمۡسٗا وَلَا زَمۡهَرِيرٗا

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona (hawatahisi) humo jua kali wala baridi kali.[1]


1- - Aya ni dalili kuwa Akhera kuna adhabu ya Baridi. Kama alivyopokea Imamu Bukhariy na Muslim- kutoka kwa Abuu Hurairah (Allah amuwiye radhh) amesema; amesema Mtume wa Allah (Rehema na amani ziwe juu yake):-


Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 14

وَدَانِيَةً عَلَيۡهِمۡ ظِلَٰلُهَا وَذُلِّلَتۡ قُطُوفُهَا تَذۡلِيلٗا

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning’inia mpaka chini



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 15

وَيُطَافُ عَلَيۡهِم بِـَٔانِيَةٖ مِّن فِضَّةٖ وَأَكۡوَابٖ كَانَتۡ قَوَارِيرَا۠

Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na bilauri zilokuwa za vigae



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 16

قَوَارِيرَاْ مِن فِضَّةٖ قَدَّرُوهَا تَقۡدِيرٗا

Vigae safi kutokana na fedha wamezipima kwa kipimo



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 17

وَيُسۡقَوۡنَ فِيهَا كَأۡسٗا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 18

عَيۡنٗا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلۡسَبِيلٗا

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 19

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيۡتَهُمۡ حَسِبۡتَهُمۡ لُؤۡلُؤٗا مَّنثُورٗا

Na watawazungukia wavulana wasio pevuka wakiwatumikia, ukiwaona utadhani ni lulu zilizo tawanywa



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 20

وَإِذَا رَأَيۡتَ ثَمَّ رَأَيۡتَ نَعِيمٗا وَمُلۡكٗا كَبِيرًا

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 21

عَٰلِيَهُمۡ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضۡرٞ وَإِسۡتَبۡرَقٞۖ وَحُلُّوٓاْ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٖ وَسَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ شَرَابٗا طَهُورًا

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 23

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ تَنزِيلٗا

Hakika Sisi tumekuteremshia Qur’ani kidogo kidogo (hatua kwa hatua)



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 24

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعۡ مِنۡهُمۡ ءَاثِمًا أَوۡ كَفُورٗا

Basi ngojea hukumu ya Mola wako wala usimtii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kukufuru



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 25

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلٗا

Na litaje jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 26

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَٱسۡجُدۡ لَهُۥ وَسَبِّحۡهُ لَيۡلٗا طَوِيلًا

Na usiku msujudie Yeye, na umtakase, (usali kwaajili yake) usiku, wakati mrefu



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 27

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ يُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَآءَهُمۡ يَوۡمٗا ثَقِيلٗا

Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito, (ya Kiyama)



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 28

نَّحۡنُ خَلَقۡنَٰهُمۡ وَشَدَدۡنَآ أَسۡرَهُمۡۖ وَإِذَا شِئۡنَا بَدَّلۡنَآ أَمۡثَٰلَهُمۡ تَبۡدِيلًا

Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 29

إِنَّ هَٰذِهِۦ تَذۡكِرَةٞۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلٗا

Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 30

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Wala hamuwezi kutaka ila atakapo Allah. Hakika Allah ni Mwenye elimu, Mwenye hekima



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 31

يُدۡخِلُ مَن يَشَآءُ فِي رَحۡمَتِهِۦۚ وَٱلظَّـٰلِمِينَ أَعَدَّ لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمَۢا

Humuingiza amtakaye katika rehema zake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iumizayo



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 1

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا

Nina apa kwa pepo zitumwazo kwa mfuatano



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 2

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا

Kisha zinazovuma kwa kasi!



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 3

وَٱلنَّـٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا

Na kwa pepo zinazotawanya (mawingu na mvua)



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 4

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا

Kisha Nina apa kwa (Malaika) wanaopambanua haki na batili



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 5

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا

Kisha kwa (Malaika) wanaopeleka Wahyi (kwa Mtume)



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 6

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا

Kwa ajili ya kuondosha udhuru au kwa ajili ya kuonya



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 7

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatatokea tu!



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 8

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ

Basi pale nyota zitakapofutiliwa mbali mwanga wake



Capítulo: ALMURSALAAT 

Verso : 9

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ

Na mbingu zitakapo pasuliwa, (au zitakapo funguliwa)