Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 73

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi Tumeufanya kuwa ni ukumbusho na manufaa kwa wasafiri



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 74

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliyetukuka



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 75

۞فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 76

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Hakika hicho ni kiapo kikubwa lau mnaelewa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 77

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika ya hiyo ni Kurani tukufu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 78

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa (Walio twahara)



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 80

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 81

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Hivi kwa maneno haya nyinyi mnapuuza na kuikanusha?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 82

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na mnafanya (badala ya kushu-kuru) kwa riziki mnayopata, nyinyi ndio mnakad hibisha



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 83

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Itakuaje basi pale roho itaka-pofika kwenye koo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 84

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama tu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 85

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Nasi Tuko karibu naye zaidi kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuoni



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 86

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hammo katika mamlaka yangu.[1]


1- - Basi kama lau kusingekua na kufufuliwa.


Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 87

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho (mwilini mwake), mkiwa ni wakweli?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 88

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa (mwenye roho hiyo) ni miongoni mwa waliokurubishwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 89

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na mabustani zenye kila aina ya neema



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 90

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa watu wa kuliani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 91

فَسَلَٰمٞ لَّكَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Basi itaambiwa amani iwe juu yako uliye katika watu kuliani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 92

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُكَذِّبِينَ ٱلضَّآلِّينَ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa wakadhibisha waliyopotea



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 93

فَنُزُلٞ مِّنۡ حَمِيمٖ

Basi mapokezi na mafikio yake ni maji ya moto yachemkayo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 94

وَتَصۡلِيَةُ جَحِيمٍ

Na kuingizwa kwenye Moto wa jahimu, (uwakao vikali mno)



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 95

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ حَقُّ ٱلۡيَقِينِ

Hakika hii bila shaka ni haki yenye yakini.[1]


1- - Hakika haya yaliotajwa katika Sura hii tukufu bila shaka ni kiini cha yakini ilio thabiti, isiyo ingiliwa na shaka hata kidogo.


Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 96

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliye Mtukufu



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 1

سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Vimemsabihi (vimemtakasa) Allah na kumtukuza vyote vilivyomo katika mbingu na ardhi na yeye tu ndiye Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 2

لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Ni Wake pekee ufalme wa mbingu na ardhi. Anahuisha na anafisha. Na yeye Muweza wa kila kitu



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 3

هُوَ ٱلۡأَوَّلُ وَٱلۡأٓخِرُ وَٱلظَّـٰهِرُ وَٱلۡبَاطِنُۖ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Yeye ndiye wa mwanzo na ndiye wa mwisho na mjuzi wa mambo ya dhahiri na ya siri na yeye ni Mjuzi sana wa kila kitu



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 4

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يَعۡلَمُ مَا يَلِجُ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا يَخۡرُجُ مِنۡهَا وَمَا يَنزِلُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا يَعۡرُجُ فِيهَاۖ وَهُوَ مَعَكُمۡ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Yeye Ndiye Aliyeumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha Akawa juu (Istawaa)[1] ya ‘Arsh, Anajua yale yanayoingia ardhini, na yale yatokayo humo, na yale yanayoteremka kutoka mbinguni, na yale yanayopanda humo, Naye Yu Pamoja nanyi popote mlipo. Na Allah ni Mwenye kuona yote myatendayo


1- - Faida: Maana ya Istawaa: Yuko juu kabisa kwa namna inayolingana na Utukufu Wake Yeye Mwenyewe Allaah. {Rejea Tanbihi (2: 29)}.


Capítulo: AL-HADIID

Verso : 5

لَّهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۚ وَإِلَى ٱللَّهِ تُرۡجَعُ ٱلۡأُمُورُ

Ni Wake Pekee ufalme wa mbingu na ardhi, kwa Allah Pekee yanarejeshwa mambo yote



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 6

يُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَيُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِۚ وَهُوَ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Anauingiza usiku katika mchana, na Anaingiza mchana katika usiku, Naye ni Mjuzi wa yaliyomo vifuani