Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 25

كَذَّبَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَأَتَىٰهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Waliokuwa kabla yao walika-dhibisha, na ikawajia adhabu kutoka pahala wasipo patambua



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 26

فَأَذَاقَهُمُ ٱللَّهُ ٱلۡخِزۡيَ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Basi Allah akawaonjesha fedheha katika uhai wa duniani. Na bila ya shaka adhabu ya Akhera ni kubwa zaidi; laiti wangelijua!



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 27

وَلَقَدۡ ضَرَبۡنَا لِلنَّاسِ فِي هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانِ مِن كُلِّ مَثَلٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na bila ya shaka tumewapigia watu mifano ya kila namna katika hii Qur’ani ili wapate kukumbuka



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 28

قُرۡءَانًا عَرَبِيًّا غَيۡرَ ذِي عِوَجٖ لَّعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Qur’ani ya Kiarabu isiyo na upogo (isiyo na mashaka), ili wamche Mungu



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 29

ضَرَبَ ٱللَّهُ مَثَلٗا رَّجُلٗا فِيهِ شُرَكَآءُ مُتَشَٰكِسُونَ وَرَجُلٗا سَلَمٗا لِّرَجُلٍ هَلۡ يَسۡتَوِيَانِ مَثَلًاۚ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Allah amepiga mfano wa mtu mwenye mabwana washirika wanao gombana, na wa mtu mwengine aliye husika na bwana mmoja tu. Je! Wako sawa katika hali zao? Alhamdulillahi, Sifa njema zote ni za Allah! Lakini wengi wao hawajui



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 30

إِنَّكَ مَيِّتٞ وَإِنَّهُم مَّيِّتُونَ

Kwa hakika wewe utakufa, na wao watakufa



Capítulo: AZZUMAR 

Verso : 31

ثُمَّ إِنَّكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ عِندَ رَبِّكُمۡ تَخۡتَصِمُونَ

Kisha bila ya shaka mtagombana Siku ya Kiyama mbele ya Mola wenu Mlezi