Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 31

وَمَآءٖ مَّسۡكُوبٖ

Na maji yenye kumiminwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 32

وَفَٰكِهَةٖ كَثِيرَةٖ

Na matunda mengi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 33

لَّا مَقۡطُوعَةٖ وَلَا مَمۡنُوعَةٖ

Hayana kikomo na wala hayakatazwi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 34

وَفُرُشٖ مَّرۡفُوعَةٍ

Na matandiko ya kupumzikia yaliyoinuliwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 35

إِنَّآ أَنشَأۡنَٰهُنَّ إِنشَآءٗ

Hakika Sisi Tutawaumba (Mahurulaini) upya



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 36

فَجَعَلۡنَٰهُنَّ أَبۡكَارًا

Na tukawafanya kuwa bikra



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 37

عُرُبًا أَتۡرَابٗا

Wenye mahaba kwa waume zao, na wana umri unaolingana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 38

لِّأَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ni kwaajili ya watu wa kuliani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 39

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika watu wa mwanzo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 40

وَثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na kundi kubwa katika watu wa mwishoni



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo