Capítulo: HUUD 

Verso : 114

وَأَقِمِ ٱلصَّلَوٰةَ طَرَفَيِ ٱلنَّهَارِ وَزُلَفٗا مِّنَ ٱلَّيۡلِۚ إِنَّ ٱلۡحَسَنَٰتِ يُذۡهِبۡنَ ٱلسَّيِّـَٔاتِۚ ذَٰلِكَ ذِكۡرَىٰ لِلذَّـٰكِرِينَ

Na simamisha swala katika ncha mbili za mchana na nyakati za usiku. Hakika mema huondoa maovu. Huo ni ukumbusho kwa wale wanaokumbuka



Capítulo: HUUD 

Verso : 115

وَٱصۡبِرۡ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na subiri (kuwa mvumilivu), kwani Allah hapotezi ujira wa wafanyao wema



Capítulo: HUUD 

Verso : 116

فَلَوۡلَا كَانَ مِنَ ٱلۡقُرُونِ مِن قَبۡلِكُمۡ أُوْلُواْ بَقِيَّةٖ يَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡفَسَادِ فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا قَلِيلٗا مِّمَّنۡ أَنجَيۡنَا مِنۡهُمۡۗ وَٱتَّبَعَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مَآ أُتۡرِفُواْ فِيهِ وَكَانُواْ مُجۡرِمِينَ

Na lau ingekuwepo katika karine za kabla yenu masalia ya watu wa kheri wanakataza maovu ardhini, (lakini hawakuwepo miongoni mwa watu wa kheri) isipokuwa wachache tu. Miongoni mwa (walioamini) tuliowaokoa kutoka kwenye adhabu. Na wale waliodhulumu wakafuata starehe zao walizoneemeshwa, na wakawa waovu



Capítulo: HUUD 

Verso : 117

وَمَا كَانَ رَبُّكَ لِيُهۡلِكَ ٱلۡقُرَىٰ بِظُلۡمٖ وَأَهۡلُهَا مُصۡلِحُونَ

Na hakuwa Mola wako mlezi ni mwenye kuangamiza watu wa miji kwa dhulma tu na hali watu wake ni watenda mema



Capítulo: HUUD 

Verso : 118

وَلَوۡ شَآءَ رَبُّكَ لَجَعَلَ ٱلنَّاسَ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗۖ وَلَا يَزَالُونَ مُخۡتَلِفِينَ

Na lau angetaka Mola wako mlezi ange wafanya watu wote kuwa umma mmoja. Na hawaachi kukhitalifiana,



Capítulo: HUUD 

Verso : 119

إِلَّا مَن رَّحِمَ رَبُّكَۚ وَلِذَٰلِكَ خَلَقَهُمۡۗ وَتَمَّتۡ كَلِمَةُ رَبِّكَ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنَ ٱلۡجِنَّةِ وَٱلنَّاسِ أَجۡمَعِينَ

Isipokuwa tu wale Mola wako mlezi amewarehemu (wakaamini); na Allah amewaumba hivyo. Na neno la Mola wako mlezi litatimia: Kwe hakika nitaijaza Jahannam miongoni mwa majini na watu wote kwa pamoja



Capítulo: HUUD 

Verso : 120

وَكُلّٗا نَّقُصُّ عَلَيۡكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلرُّسُلِ مَا نُثَبِّتُ بِهِۦ فُؤَادَكَۚ وَجَآءَكَ فِي هَٰذِهِ ٱلۡحَقُّ وَمَوۡعِظَةٞ وَذِكۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Na yote haya tunakusimulia miongoni mwa habari za Mitume yale yanayoupa nguvu moyo wako. Na katika haya imekujia haki na mawaidha na ukumbusho kwa waumini



Capítulo: HUUD 

Verso : 121

وَقُل لِّلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ ٱعۡمَلُواْ عَلَىٰ مَكَانَتِكُمۡ إِنَّا عَٰمِلُونَ

Na waambie wale wasio amini: Fanyeni muwezavyo, nasi pia tunafanya (tuwezavyo)



Capítulo: HUUD 

Verso : 122

وَٱنتَظِرُوٓاْ إِنَّا مُنتَظِرُونَ

Na ngojeni, na sisi tunangoja



Capítulo: HUUD 

Verso : 123

وَلِلَّهِ غَيۡبُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَإِلَيۡهِ يُرۡجَعُ ٱلۡأَمۡرُ كُلُّهُۥ فَٱعۡبُدۡهُ وَتَوَكَّلۡ عَلَيۡهِۚ وَمَا رَبُّكَ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Na ni vya Allah tu vyote vilivyo fichikana mbinguni na ardhini, na mambo yote yatarudishwa kwake tu. Basi muabudu yeye na umtegemee yeye. Na Mola wako mlezi haghafiliki na yale mnayo yatenda



Capítulo: YUSUF 

Verso : 1

الٓرۚ تِلۡكَ ءَايَٰتُ ٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Alif Laam Raa[1]. Hizo ni Aya za Kitabu kinachobainisha


1- - Allah ndiye ajuaye zaidi maana ya herufi mkato hizi.


Capítulo: YUSUF 

Verso : 2

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ

Hakika, sisi tumeiteremsha Qur’ani kwa Kiarabu ili mpate kuelewa



Capítulo: YUSUF 

Verso : 3

نَحۡنُ نَقُصُّ عَلَيۡكَ أَحۡسَنَ ٱلۡقَصَصِ بِمَآ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانَ وَإِن كُنتَ مِن قَبۡلِهِۦ لَمِنَ ٱلۡغَٰفِلِينَ

Sisi tunakusimulia simulizi nzuri sana kwa (huu) Wahyi tuliokufunulia wa hii Qur’ani, na ingawa kabla yake ulikuwa miongoni mwa wasiojua



Capítulo: YUSUF 

Verso : 4

إِذۡ قَالَ يُوسُفُ لِأَبِيهِ يَـٰٓأَبَتِ إِنِّي رَأَيۡتُ أَحَدَ عَشَرَ كَوۡكَبٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ رَأَيۡتُهُمۡ لِي سَٰجِدِينَ

(Kumbuka) Wakati Yusuf alipomwambia baba yake (Yakubu kwamba): Ewe Baba yangu, hakika mimi niliona (usingizini) nyota kumi na moja na jua na mwezi; nimeziona zikinisujudia



Capítulo: YUSUF 

Verso : 5

قَالَ يَٰبُنَيَّ لَا تَقۡصُصۡ رُءۡيَاكَ عَلَىٰٓ إِخۡوَتِكَ فَيَكِيدُواْ لَكَ كَيۡدًاۖ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لِلۡإِنسَٰنِ عَدُوّٞ مُّبِينٞ

(Yakubu) Alisema: Ewe kijana wangu, usiwasimulie ndugu zako ndoto yako, wasije wakakufanyia hila (husuda). Hakika, shetani kwa mwanadamu ni adui wa wazi



Capítulo: YUSUF 

Verso : 6

وَكَذَٰلِكَ يَجۡتَبِيكَ رَبُّكَ وَيُعَلِّمُكَ مِن تَأۡوِيلِ ٱلۡأَحَادِيثِ وَيُتِمُّ نِعۡمَتَهُۥ عَلَيۡكَ وَعَلَىٰٓ ءَالِ يَعۡقُوبَ كَمَآ أَتَمَّهَا عَلَىٰٓ أَبَوَيۡكَ مِن قَبۡلُ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡحَٰقَۚ إِنَّ رَبَّكَ عَلِيمٌ حَكِيمٞ

Na kama hivyo anakuteua Mola wako Mlezi na akakufundisha tafsiri za matukio (ndoto) na anatimiza neema zake kwako na kwa familia ya Yakubu, kama alivyozitimizia (neema hizo) kwa Baba zako wawili hapo kabla; Ibrahimu na Is-haka[1]. Hakika, Mola wako Mlezi ni Mjuzi, Mwenye hekima


1- - Hawa ni mababu wa Nabii Yusuf. Katika lugha ya Qur’ani babu anahisabika ni baba.


Capítulo: YUSUF 

Verso : 7

۞لَّقَدۡ كَانَ فِي يُوسُفَ وَإِخۡوَتِهِۦٓ ءَايَٰتٞ لِّلسَّآئِلِينَ

Kwa yakini kabisa, katika (kisa cha) Yusuf na ndugu zake zipo ishara (nyingi) kwa wanaouliza



Capítulo: YUSUF 

Verso : 8

إِذۡ قَالُواْ لَيُوسُفُ وَأَخُوهُ أَحَبُّ إِلَىٰٓ أَبِينَا مِنَّا وَنَحۡنُ عُصۡبَةٌ إِنَّ أَبَانَا لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

(Kumbukeni) Wakati (ndugu wa Yusuf) waliposema: Kwa hakika kabisa, Yusuf na nduguye (wa mama mmoja) wanapendwa zaidi na baba yetu kuliko sisi, na ilihali sisi ni wengi. Hakika, Baba yetu yumo kwenye upotevu ulio wazi (anafanya kosa la wazi)



Capítulo: YUSUF 

Verso : 9

ٱقۡتُلُواْ يُوسُفَ أَوِ ٱطۡرَحُوهُ أَرۡضٗا يَخۡلُ لَكُمۡ وَجۡهُ أَبِيكُمۡ وَتَكُونُواْ مِنۢ بَعۡدِهِۦ قَوۡمٗا صَٰلِحِينَ

(Ndugu wa Yusuf walisema): Muueni Yusuf au mtupeni ardhi (ya mbali) ili uso (na upendo) wa Baba yenu utakuelekeeni nyinyi tena baada yake (baada ya kumuua Yusuf mtatubu dhambi hiyo na) mtakuwa watu wema



Capítulo: YUSUF 

Verso : 10

قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ لَا تَقۡتُلُواْ يُوسُفَ وَأَلۡقُوهُ فِي غَيَٰبَتِ ٱلۡجُبِّ يَلۡتَقِطۡهُ بَعۡضُ ٱلسَّيَّارَةِ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ

Alisema msemaji kati yao: Msimuue Yusuf (lakini) mtupeni kwenye kina cha kisima (kirefu) ataokotwa na baadhi ya wasafiri kama nyinyi mna azma ya kufanya (jambo la kumtenganisha na baba yake)



Capítulo: YUSUF 

Verso : 11

قَالُواْ يَـٰٓأَبَانَا مَا لَكَ لَا تَأۡمَ۬نَّا عَلَىٰ يُوسُفَ وَإِنَّا لَهُۥ لَنَٰصِحُونَ

(Nduguze baada ya kuafikiana) Walisema: Ewe Baba yetu, una nini hata hutuamini kwa Yusuf na ilihali sisi, kwa hakika, ni wenye kumtakia mema?



Capítulo: YUSUF 

Verso : 12

أَرۡسِلۡهُ مَعَنَا غَدٗا يَرۡتَعۡ وَيَلۡعَبۡ وَإِنَّا لَهُۥ لَحَٰفِظُونَ

Mruhusu kesho (atoke) pamoja nasi (kwenda malishoni) atakula na kucheza kwa furaha, nakwa yakini kabisa, sisi tutamlinda



Capítulo: YUSUF 

Verso : 13

قَالَ إِنِّي لَيَحۡزُنُنِيٓ أَن تَذۡهَبُواْ بِهِۦ وَأَخَافُ أَن يَأۡكُلَهُ ٱلذِّئۡبُ وَأَنتُمۡ عَنۡهُ غَٰفِلُونَ

(Yakubu) Alisema: Kwa hakika kabisa, inanihuzunisha nyinyi kwenda naye (na kuniacha peke yangu) na nachelea asije akaliwa na mbwa mwitu ilihali nyinyi mkiwa mmeghafilika



Capítulo: YUSUF 

Verso : 14

قَالُواْ لَئِنۡ أَكَلَهُ ٱلذِّئۡبُ وَنَحۡنُ عُصۡبَةٌ إِنَّآ إِذٗا لَّخَٰسِرُونَ

Walisema (kumwambia Baba yao): Iwapo ataliwa na mbwa mwitu na ilihali sisi ni wengi (kundi lenye nguvu), bila ya shaka sisi wakati huo tutakuwa hasarani (hatuna faida)



Capítulo: YUSUF 

Verso : 15

فَلَمَّا ذَهَبُواْ بِهِۦ وَأَجۡمَعُوٓاْ أَن يَجۡعَلُوهُ فِي غَيَٰبَتِ ٱلۡجُبِّۚ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡهِ لَتُنَبِّئَنَّهُم بِأَمۡرِهِمۡ هَٰذَا وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ

Basi walipokwenda naye na kukubaliana kumtumbukiza (kumtosa) katika kina cha kisima kirefu, na tulimfunulia Wahyi Yusuf (hapo kisimani kwamba): Hapana shaka yoyote utakuja kuwaambia (siku za usoni) kuhusu jambo lao hili, na wala wao hawatahisi (kama wewe ni Yusuf)



Capítulo: YUSUF 

Verso : 16

وَجَآءُوٓ أَبَاهُمۡ عِشَآءٗ يَبۡكُونَ

Walimjia Baba yao (wakati wa) usiku huku wakiangua kilio (cha uongo)



Capítulo: YUSUF 

Verso : 17

قَالُواْ يَـٰٓأَبَانَآ إِنَّا ذَهَبۡنَا نَسۡتَبِقُ وَتَرَكۡنَا يُوسُفَ عِندَ مَتَٰعِنَا فَأَكَلَهُ ٱلذِّئۡبُۖ وَمَآ أَنتَ بِمُؤۡمِنٖ لَّنَا وَلَوۡ كُنَّا صَٰدِقِينَ

Walisema: Ewe Baba yetu, hakika sisi tulikwenda kushindana na tulimuacha Yusuf kwenye vitu vyetu, basi akaliwa na mbwa mwitu (lakini wewe hutatuamini na hata kama tunasema kweli



Capítulo: YUSUF 

Verso : 18

وَجَآءُو عَلَىٰ قَمِيصِهِۦ بِدَمٖ كَذِبٖۚ قَالَ بَلۡ سَوَّلَتۡ لَكُمۡ أَنفُسُكُمۡ أَمۡرٗاۖ فَصَبۡرٞ جَمِيلٞۖ وَٱللَّهُ ٱلۡمُسۡتَعَانُ عَلَىٰ مَا تَصِفُونَ

Walikuja na kanzu yake huku ikiwa na damu ya uongo. (Yakubu alipobaini geresha yao) (Yakubu) Alisema: “Bali nafsi zenu zimekushawishini (kutenda) jambo (baya). Basi subira ni jambo zuri, na Allah ndiye wa kuombwa msaada kwa huu (uongo) mnaoueleza”



Capítulo: YUSUF 

Verso : 19

وَجَآءَتۡ سَيَّارَةٞ فَأَرۡسَلُواْ وَارِدَهُمۡ فَأَدۡلَىٰ دَلۡوَهُۥۖ قَالَ يَٰبُشۡرَىٰ هَٰذَا غُلَٰمٞۚ وَأَسَرُّوهُ بِضَٰعَةٗۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na uliwasili msafara, na ukamtuma mchota maji wao, naye akatumbukiza ndoo yake (ili kuchota maji). Alisema: Furaha iliyoje! Huyu hapa mvulana! Na walimficha akiwa (kama) bidhaa. Na Allah ni Mjuzi wa wanayoyatenda



Capítulo: YUSUF 

Verso : 20

وَشَرَوۡهُ بِثَمَنِۭ بَخۡسٖ دَرَٰهِمَ مَعۡدُودَةٖ وَكَانُواْ فِيهِ مِنَ ٱلزَّـٰهِدِينَ

Na (wale wasafiri) walimuuza (Yusuf) kwa thamani duni; pesa chache. Na hawakuwa na haja naye