Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 1

سَبَّحَ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۖ وَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Vimemtakasa Allah (viumbe) vyote vilivyomo katika mbingu na katika ardhi. Na Yeye ni Mwenye nguvu kubwa, Mwenye hekima sana



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 2

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لِمَ تَقُولُونَ مَا لَا تَفۡعَلُونَ

Enyi mlioamini, kwanini mnasema msiyoyafanya?



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 3

كَبُرَ مَقۡتًا عِندَ ٱللَّهِ أَن تَقُولُواْ مَا لَا تَفۡعَلُونَ

Imekuwa chukizo kubwa mno mbele ya Allah kwamba mnasema msiyoyafanya



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 4

إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلَّذِينَ يُقَٰتِلُونَ فِي سَبِيلِهِۦ صَفّٗا كَأَنَّهُم بُنۡيَٰنٞ مَّرۡصُوصٞ

Kwa hakika, Allah anawapenda wanaopigana katika njia yake wakiwa safu (moja) kama jengo liliokamatana



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 5

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ لِمَ تُؤۡذُونَنِي وَقَد تَّعۡلَمُونَ أَنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُمۡۖ فَلَمَّا زَاغُوٓاْ أَزَاغَ ٱللَّهُ قُلُوبَهُمۡۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Na (kumbuka Musa) Musa alipowaambia watu wake: Enyi watu wangu: Kwanini mnaniudhi, na ilhali mnajua kuwa hakika mimi ni Mtume wa Allah niliyetumwa kwenu? Basi walipo potoka, Allah aliziachia nyoyo zao zipotoke. Na Allah hawaongozi watu waovu



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 6

وَإِذۡ قَالَ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ يَٰبَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ إِنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُم مُّصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيَّ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَمُبَشِّرَۢا بِرَسُولٖ يَأۡتِي مِنۢ بَعۡدِي ٱسۡمُهُۥٓ أَحۡمَدُۖ فَلَمَّا جَآءَهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ قَالُواْ هَٰذَا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

Na (kumbuka Mtume) Isa, Mwana wa Mariamu aliposema: Enyi Wana wa Israili: Hakika, mimi ni Mtume wa Allah kwenu, nikithibitisha Taurati iliyokuwepo kabla yangu, na nikitoa bishara (habari njema) ya Mtume atakayekuja baada yangu; jina lake ni Ahmad. Lakini (Mtume huyo) alipowaletea hoja zilizo wazi, walisema: Huu ni uchawi ulio dhahiri



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 7

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَ وَهُوَ يُدۡعَىٰٓ إِلَى ٱلۡإِسۡلَٰمِۚ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ni nani mwenye kudhulumu zaidi kuliko yule anaye mzulia Allah uwongo, naye anaitwa kwenye Uislamu? Na Allah hawaongoi watu madhaalimu



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 8

يُرِيدُونَ لِيُطۡفِـُٔواْ نُورَ ٱللَّهِ بِأَفۡوَٰهِهِمۡ وَٱللَّهُ مُتِمُّ نُورِهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡكَٰفِرُونَ

Wanataka kuizima nuru ya Allah kwa vinywa vyao. Na Allah atakamilisha nuru yake ijapo kuwa makafiri watachukia



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 9

هُوَ ٱلَّذِيٓ أَرۡسَلَ رَسُولَهُۥ بِٱلۡهُدَىٰ وَدِينِ ٱلۡحَقِّ لِيُظۡهِرَهُۥ عَلَى ٱلدِّينِ كُلِّهِۦ وَلَوۡ كَرِهَ ٱلۡمُشۡرِكُونَ

Yeye ndiye aliye mtuma Mtume wake kwa uwongofu na Dini ya haki ili ipate kuzishinda dini zote, ijapo kuwa washirikina watachukia



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 10

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ هَلۡ أَدُلُّكُمۡ عَلَىٰ تِجَٰرَةٖ تُنجِيكُم مِّنۡ عَذَابٍ أَلِيمٖ

Enyi mlioamini! Nikujulisheni biashara itakayo kuokoeni na adhabu iliyo chungu (iumizayo)?



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 11

تُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَتُجَٰهِدُونَ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ بِأَمۡوَٰلِكُمۡ وَأَنفُسِكُمۡۚ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Muaminini Allah na Mtume wake, na piganeni Jihadi katika Njia ya Allah kwa mali zenu na nafsi zenu. Haya ni bora kwenu, ikiwa nyinyi mnajua



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 12

يَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡ وَيُدۡخِلۡكُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ وَمَسَٰكِنَ طَيِّبَةٗ فِي جَنَّـٰتِ عَدۡنٖۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Atakusameheni dhambi zenu, na atakutieni katika Mabustani yapitiwayo na mito kati yake, na maskani nzuri nzuri katika Bustani za milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 13

وَأُخۡرَىٰ تُحِبُّونَهَاۖ نَصۡرٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَفَتۡحٞ قَرِيبٞۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na kingine mkipendacho, nacho ni nusura itokayo kwa Allah, na ushindi ulio karibu! Na wabashirieni Waumini!



Capítulo: ASSWAFF 

Verso : 14

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُونُوٓاْ أَنصَارَ ٱللَّهِ كَمَا قَالَ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ لِلۡحَوَارِيِّـۧنَ مَنۡ أَنصَارِيٓ إِلَى ٱللَّهِۖ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ نَحۡنُ أَنصَارُ ٱللَّهِۖ فَـَٔامَنَت طَّآئِفَةٞ مِّنۢ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ وَكَفَرَت طَّآئِفَةٞۖ فَأَيَّدۡنَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ عَلَىٰ عَدُوِّهِمۡ فَأَصۡبَحُواْ ظَٰهِرِينَ

Enyi walioamini! Kuweni wenye kuinusuru (Dini ya) Allah kama alivyosema ‘Isa mwana wa Maryam kwa wafuasi wake (watiifu): Na ni wanusuruji wangu kwa ajili ya Allah? Wafuasi wake wakasema: Sisi ni wenye kuinusuru (Dini ya) Allah, Basi likaamini kundi miongoni mwa wana wa Israail na likakufuru kundi jingine. Tukawatia nguvu wale walioamini dhidi ya maadui zao, wakawa wenye kushinda