Capítulo: HUUD 

Verso : 1

الٓرۚ كِتَٰبٌ أُحۡكِمَتۡ ءَايَٰتُهُۥ ثُمَّ فُصِّلَتۡ مِن لَّدُنۡ حَكِيمٍ خَبِيرٍ

Alif, laam, raa (hizi ni herufi za mkato na Allah ndiye anayejua maana yake). Hiki ni kitabu (ambacho) zimetengenezwa vyema Aya zake kisha zimefafanuliwa kutoka kwa aliye na Hekima, Mwenye habari nyingi



Capítulo: HUUD 

Verso : 2

أَلَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَۚ إِنَّنِي لَكُم مِّنۡهُ نَذِيرٞ وَبَشِيرٞ

(Kwamba) Msiabudu chochote ispokuwa Allah tu. Hakika mimi ninatoka kwake (nikiwa) Muonyaji na Mwenye kutoa habari njema



Capítulo: HUUD 

Verso : 3

وَأَنِ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ ثُمَّ تُوبُوٓاْ إِلَيۡهِ يُمَتِّعۡكُم مَّتَٰعًا حَسَنًا إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى وَيُؤۡتِ كُلَّ ذِي فَضۡلٖ فَضۡلَهُۥۖ وَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٖ كَبِيرٍ

Na muombeni msamaha Mola wenu Mlezi kisha rejeeni kwake atawastarehesheni starehe nzuri mpaka muda uliotajwa, na atampa kila mwenye fadhila fadhila zake na kama watakengeuka kwa hakika mimi ninaogopea kwenu (kupata) adhabu ya Siku kubwa



Capítulo: HUUD 

Verso : 4

إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Kwa Allah tu ndio marejeo yenu na Yeye kwa kila kitu ni Muweza



Capítulo: HUUD 

Verso : 5

أَلَآ إِنَّهُمۡ يَثۡنُونَ صُدُورَهُمۡ لِيَسۡتَخۡفُواْ مِنۡهُۚ أَلَا حِينَ يَسۡتَغۡشُونَ ثِيَابَهُمۡ يَعۡلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعۡلِنُونَۚ إِنَّهُۥ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Ehee!Kwa hakika wao wanaficha vifuani mwao (ukafiri,) ili wajifiche kwake. Ehee!Wakati wanajifunika nguo zao (wasionekane) kwamba Allah anajua yote wanayoyaficha na wanayoyadhihirisha kwa hakika Yeye ni Mjuzi wa yaliomo vifuani



Capítulo: HUUD 

Verso : 6

۞وَمَا مِن دَآبَّةٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِ رِزۡقُهَا وَيَعۡلَمُ مُسۡتَقَرَّهَا وَمُسۡتَوۡدَعَهَاۚ كُلّٞ فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ

Na hakuna chochote kitem-beacho ardhini ispokuwa rizki yake ni kwa Allah pekee, na anayajua makazi yake (hapa duniani na baada ya kufa kwake) na sehemu atakapokufa. Hayo yote yapo katika kitabu kinacho bainisha



Capítulo: HUUD 

Verso : 7

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ وَكَانَ عَرۡشُهُۥ عَلَى ٱلۡمَآءِ لِيَبۡلُوَكُمۡ أَيُّكُمۡ أَحۡسَنُ عَمَلٗاۗ وَلَئِن قُلۡتَ إِنَّكُم مَّبۡعُوثُونَ مِنۢ بَعۡدِ ٱلۡمَوۡتِ لَيَقُولَنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

Na ni Yeye ambaye ameziumba mbingu na ardhi katika siku sita, na Arshi yake ilikuwa juu ya maji (kabla ya kuumbwa mbingu na ardhi), ili awatahini (ajue) ni nani miongoni mwenu aliye mzuri sana wa matendo. Na endapo utawaambia: Hakika nyinyi mtafufuliwa baada ya kufa, watasema wale waliokufuru: Hii Qur’ani sichochote ispokuwa ni uchawi tu ulio wazi



Capítulo: HUUD 

Verso : 8

وَلَئِنۡ أَخَّرۡنَا عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابَ إِلَىٰٓ أُمَّةٖ مَّعۡدُودَةٖ لَّيَقُولُنَّ مَا يَحۡبِسُهُۥٓۗ أَلَا يَوۡمَ يَأۡتِيهِمۡ لَيۡسَ مَصۡرُوفًا عَنۡهُمۡ وَحَاقَ بِهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Na kwa hakika endapo tutawa-cheleweshea adhabu mpaka muda (maalumu) uliohesabiwa, kwa yakini watasema ni kipi kinachoifunga adhabu hiyo (kama ni kweli ipo)? Ehee siku itakapowajia haitawakosa wao na yatawazunguka yale waliyokuwa wanayafanyia mzaha



Capítulo: HUUD 

Verso : 9

وَلَئِنۡ أَذَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِنَّا رَحۡمَةٗ ثُمَّ نَزَعۡنَٰهَا مِنۡهُ إِنَّهُۥ لَيَـُٔوسٞ كَفُورٞ

Na kama mwanadamu tutam-uonjesha kutoka kwetu rehema yoyote kisha tukaiondoa kwake rehema hiyo, kwa hakika yeye hukata tamaa akakufuru



Capítulo: HUUD 

Verso : 10

وَلَئِنۡ أَذَقۡنَٰهُ نَعۡمَآءَ بَعۡدَ ضَرَّآءَ مَسَّتۡهُ لَيَقُولَنَّ ذَهَبَ ٱلسَّيِّـَٔاتُ عَنِّيٓۚ إِنَّهُۥ لَفَرِحٞ فَخُورٌ

Na iwapo tutamuonjesha neema nyingi baada ya madhara (matatizo) yaliyompata, kwa hakika atasema yameniondokea matatizo, kwa hakika yeye anakuwa mwenye furaha sana mwenye kujigamba mno



Capítulo: HUUD 

Verso : 11

إِلَّا ٱلَّذِينَ صَبَرُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُم مَّغۡفِرَةٞ وَأَجۡرٞ كَبِيرٞ

Isipokuwa tu wale walio subiri na wakatenda mema, hao wanamsamaha (kutoka kwa Mola wao mlezi) na wanamalipo makubwa



Capítulo: HUUD 

Verso : 12

فَلَعَلَّكَ تَارِكُۢ بَعۡضَ مَا يُوحَىٰٓ إِلَيۡكَ وَضَآئِقُۢ بِهِۦ صَدۡرُكَ أَن يَقُولُواْ لَوۡلَآ أُنزِلَ عَلَيۡهِ كَنزٌ أَوۡ جَآءَ مَعَهُۥ مَلَكٌۚ إِنَّمَآ أَنتَ نَذِيرٞۚ وَٱللَّهُ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٌ

Huenda wewe ni mwenye kuacha baadhi ya yale yaliyofunuliwa kwako, na kifua chako kinabana wanaposema kuwa: Kwanini asingeteremshiwa hazina au angekuja Malaika pamoja naye? Hakika sivingine wewe ni muhofishaji tu na Allah ni msimamizi wa kila kitu



Capítulo: HUUD 

Verso : 13

أَمۡ يَقُولُونَ ٱفۡتَرَىٰهُۖ قُلۡ فَأۡتُواْ بِعَشۡرِ سُوَرٖ مِّثۡلِهِۦ مُفۡتَرَيَٰتٖ وَٱدۡعُواْ مَنِ ٱسۡتَطَعۡتُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Au wanasema hii Qur’ani ameizua? Sema: Leteni Sura kumi zilizozushwa mfano wake na muiteni mtakayeweza (kumuita) badala ya Allah kama mkiwa wa kweli (katika madai yenu)



Capítulo: HUUD 

Verso : 14

فَإِلَّمۡ يَسۡتَجِيبُواْ لَكُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَآ أُنزِلَ بِعِلۡمِ ٱللَّهِ وَأَن لَّآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ فَهَلۡ أَنتُم مُّسۡلِمُونَ

Na kama hawakukujibuni hilo basi juweni kwamba, sivinginevyo (Qur’ani imeteremshwa kwa elimu ya Allah na hakuna Mola anayestahiki kuabudiwa ispokuwa Yeye tu je nyinyi mmesilimu?



Capítulo: HUUD 

Verso : 15

مَن كَانَ يُرِيدُ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا وَزِينَتَهَا نُوَفِّ إِلَيۡهِمۡ أَعۡمَٰلَهُمۡ فِيهَا وَهُمۡ فِيهَا لَا يُبۡخَسُونَ

Wale wanaotaka (katika matendo yao wanayofanya wapate) maisha ya kidunia na mapambo yake (kama dhahabu, fedha, watoto nafasi, wanawake nk), tutawalipa (thawabu hizo) kikamilifu hapa duniani na hawatapunguziwa chochote



Capítulo: HUUD 

Verso : 16

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ لَيۡسَ لَهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ إِلَّا ٱلنَّارُۖ وَحَبِطَ مَا صَنَعُواْ فِيهَا وَبَٰطِلٞ مَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Hao ndio wale ambao Akhera hawana chochote isipokuwa Moto tu, na yataharibika matendo yao yote na ni batili yote waliyokuwa wakiyatenda



Capítulo: HUUD 

Verso : 17

أَفَمَن كَانَ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّهِۦ وَيَتۡلُوهُ شَاهِدٞ مِّنۡهُ وَمِن قَبۡلِهِۦ كِتَٰبُ مُوسَىٰٓ إِمَامٗا وَرَحۡمَةًۚ أُوْلَـٰٓئِكَ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۚ وَمَن يَكۡفُرۡ بِهِۦ مِنَ ٱلۡأَحۡزَابِ فَٱلنَّارُ مَوۡعِدُهُۥۚ فَلَا تَكُ فِي مِرۡيَةٖ مِّنۡهُۚ إِنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَ ٱلنَّاسِ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hivi yule aliye na hoja kutoka kwa Mola wake mlezi na akaifuata (hoja hiyo) shahidi kutoka kwake (Jibrili) na kabla yake palikuwepo kitabu (cha taurati kilichoteremshwa kwa Nabii) Musa juu yake amani, kikiwa ni kiongozi na rehema, hao wanaiamini Qur ani, na yeyote anaeikufuru miongoni mwa makundi, basi Moto ni mahali pake alipoahidiwa, basi usiwe katika shaka yoyote, hii Qur’ani ni haki kutoka kwa bwana wako, lakini watu wengi hawaamini



Capítulo: HUUD 

Verso : 18

وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًاۚ أُوْلَـٰٓئِكَ يُعۡرَضُونَ عَلَىٰ رَبِّهِمۡ وَيَقُولُ ٱلۡأَشۡهَٰدُ هَـٰٓؤُلَآءِ ٱلَّذِينَ كَذَبُواْ عَلَىٰ رَبِّهِمۡۚ أَلَا لَعۡنَةُ ٱللَّهِ عَلَى ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ni nani aliye dhalimu zaidi (katika kuzua) kuliko yule aliyemzulia Allah uongo? Hao watahudhurishwa kwa Mola wao mlezi na mashahidi watasema: Hawa ndiyo wale waliyomzulia uongo Mola wao mlezi, ehee laana ya Allah iwe kwa Madhalimu



Capítulo: HUUD 

Verso : 19

ٱلَّذِينَ يَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَيَبۡغُونَهَا عِوَجٗا وَهُم بِٱلۡأٓخِرَةِ هُمۡ كَٰفِرُونَ

(Madhalimu) ambao wanawazuia watu (kuifuata) njia ya Allah na wanaitaka njia iende kombo (iwe sawa na matamanio yao) ilhali wao Akhera wanaikataa



Capítulo: HUUD 

Verso : 20

أُوْلَـٰٓئِكَ لَمۡ يَكُونُواْ مُعۡجِزِينَ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَمَا كَانَ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِنۡ أَوۡلِيَآءَۘ يُضَٰعَفُ لَهُمُ ٱلۡعَذَابُۚ مَا كَانُواْ يَسۡتَطِيعُونَ ٱلسَّمۡعَ وَمَا كَانُواْ يُبۡصِرُونَ

Hao hawakuwa wenye kushin-dikana katika ardhi na hawakuwa na wakuwanusuru badala ya Allah, adhabu itazidishwa kwa watu hao, hawakuwa wanaweza kusikia (Qur’ani) na hawakuwa wanaona (miujiza na kunufaika nayo)



Capítulo: HUUD 

Verso : 21

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Hao ndio ambao wamezitia hasara nafsi zao na yamewapotea yote waliyokuwa wanayazua



Capítulo: HUUD 

Verso : 22

لَا جَرَمَ أَنَّهُمۡ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ هُمُ ٱلۡأَخۡسَرُونَ

Ni hakika kwamba wao Akhera, ndiyo wenye hasara kubwa sana



Capítulo: HUUD 

Verso : 23

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ وَأَخۡبَتُوٓاْ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Hakika wale walioamini na wakatenda mema na wakanyenyekea kwa Mola wao mlezi, hao ni watu wa Peponi wao humo wataishi milele



Capítulo: HUUD 

Verso : 24

۞مَثَلُ ٱلۡفَرِيقَيۡنِ كَٱلۡأَعۡمَىٰ وَٱلۡأَصَمِّ وَٱلۡبَصِيرِ وَٱلسَّمِيعِۚ هَلۡ يَسۡتَوِيَانِ مَثَلًاۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Mfano wa makundi mawili hayo ni kama kipofu na kiziwi na (kama) aliye na uoni sana na anayesikia mno hivi nikweli makundi mawili hayo yanalingana? Kwanini ham-kumbuki?



Capítulo: HUUD 

Verso : 25

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

Na kwa hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake (akawaambia watu wake kuwa) hakika mimi kwenu ni muonyaji ninaye bainisha



Capítulo: HUUD 

Verso : 26

أَن لَّا تَعۡبُدُوٓاْ إِلَّا ٱللَّهَۖ إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ أَلِيمٖ

(Kwamba) musimuabudu yeyote ispokuwa Allah kwa hakika mimi ninaogopea kwenu adhabu ya siku yenye kuumiza mno



Capítulo: HUUD 

Verso : 27

فَقَالَ ٱلۡمَلَأُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَوۡمِهِۦ مَا نَرَىٰكَ إِلَّا بَشَرٗا مِّثۡلَنَا وَمَا نَرَىٰكَ ٱتَّبَعَكَ إِلَّا ٱلَّذِينَ هُمۡ أَرَاذِلُنَا بَادِيَ ٱلرَّأۡيِ وَمَا نَرَىٰ لَكُمۡ عَلَيۡنَا مِن فَضۡلِۭ بَلۡ نَظُنُّكُمۡ كَٰذِبِينَ

Wakasema waheshimiwa ambao wamekufuru katika watu wake: Wewe hatukuoni (chochote) ispokuwa tu ni mtu mfano wetu (sio Malaika) na hatuoni wafuasi wako ispokuwa tu ni wale ambao ni wanyonge wetu wenye mawazo duni, na hatuwaoni kuwa mnaubora wowote kwetu bali tuna hakika kuwa ni waongo



Capítulo: HUUD 

Verso : 28

قَالَ يَٰقَوۡمِ أَرَءَيۡتُمۡ إِن كُنتُ عَلَىٰ بَيِّنَةٖ مِّن رَّبِّي وَءَاتَىٰنِي رَحۡمَةٗ مِّنۡ عِندِهِۦ فَعُمِّيَتۡ عَلَيۡكُمۡ أَنُلۡزِمُكُمُوهَا وَأَنتُمۡ لَهَا كَٰرِهُونَ

Akasema enyi jamaa zangu hivi mwaonaje nikiwa nina hoja kutoka kwa Mola wangu mlezi na amenipa rehema kutoka kwake na ikafichwa kwenu, hivi tuwalazimishe kukubali na ilhali nyinyi mnaichukia?



Capítulo: HUUD 

Verso : 29

وَيَٰقَوۡمِ لَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مَالًاۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَى ٱللَّهِۚ وَمَآ أَنَا۠ بِطَارِدِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْۚ إِنَّهُم مُّلَٰقُواْ رَبِّهِمۡ وَلَٰكِنِّيٓ أَرَىٰكُمۡ قَوۡمٗا تَجۡهَلُونَ

Na enyi jamaa zangu siwaombi mali (malipo kama ujira wa kazi ya kuwafikishia daawa) hakuna wakunilipa ispokuwa Allah tu, nami si mwenye kuwafukuza wale walioamini (kwa unyonge wao), kwa hakika wao watakutana na Mola wao mlezi lakini mimi ninakuoneni ni watu wajinga



Capítulo: HUUD 

Verso : 30

وَيَٰقَوۡمِ مَن يَنصُرُنِي مِنَ ٱللَّهِ إِن طَرَدتُّهُمۡۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Na enyi jama zangu ninani atakaeninusuru kutokana na (adhabu ya) Allah iwapo nitawafukuza? Hivi hamuonyeki?