Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 181

۞أَوۡفُواْ ٱلۡكَيۡلَ وَلَا تَكُونُواْ مِنَ ٱلۡمُخۡسِرِينَ

Timizeni kipimo sawa sawa, wala msiwe katika wanao punja



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 182

وَزِنُواْ بِٱلۡقِسۡطَاسِ ٱلۡمُسۡتَقِيمِ

Na pimeni kwa haki iliyo nyooka;



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 183

وَلَا تَبۡخَسُواْ ٱلنَّاسَ أَشۡيَآءَهُمۡ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ

Wala msiwapunje watu vitu vyao, wala msifanye jeuri kwa ufisadi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 184

وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ وَٱلۡجِبِلَّةَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na mcheni aliye kuumbeni nyinyi na vizazi vilivyo tangulia



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 185

قَالُوٓاْ إِنَّمَآ أَنتَ مِنَ ٱلۡمُسَحَّرِينَ

Wakasema: Hakika wewe ni katika walio rogwa



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 186

وَمَآ أَنتَ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَإِن نَّظُنُّكَ لَمِنَ ٱلۡكَٰذِبِينَ

Na wewe si chochote ila ni mtu tu kama sisi, na kwa yakini tunakuona wewe ni katika waongo



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 187

فَأَسۡقِطۡ عَلَيۡنَا كِسَفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ إِن كُنتَ مِنَ ٱلصَّـٰدِقِينَ

Hebu tuangushie vipande kutoka mbinguni ikiwa wewe ni miongoni mwa wasemao kweli



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 188

قَالَ رَبِّيٓ أَعۡلَمُ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Akasema: Mola wangu Mlezi anajua zaidi mnayo yatenda



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 189

فَكَذَّبُوهُ فَأَخَذَهُمۡ عَذَابُ يَوۡمِ ٱلظُّلَّةِۚ إِنَّهُۥ كَانَ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٍ

Basi walimkanusha, na ikawashika adhabu ya siku ya kivuli. Hakika hiyo ilikuwa adhabu ya siku kubwa



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 190

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo Ishara, lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 191

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi bila ya shaka ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 192

وَإِنَّهُۥ لَتَنزِيلُ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na bila ya shaka huu ni Uteremsho wa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 193

نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ

Ameuteremsha Roho mua-minifu,(jibril)



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 194

عَلَىٰ قَلۡبِكَ لِتَكُونَ مِنَ ٱلۡمُنذِرِينَ

Juu ya moyo wako, ili uwe katika Waonyaji,



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 195

بِلِسَانٍ عَرَبِيّٖ مُّبِينٖ

Kwa ulimi wa Kiarabu ulio wazi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 196

وَإِنَّهُۥ لَفِي زُبُرِ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na hakika bila ya shaka haya yamo katika Vitabu vya kale



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 197

أَوَلَمۡ يَكُن لَّهُمۡ ءَايَةً أَن يَعۡلَمَهُۥ عُلَمَـٰٓؤُاْ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ

Je! Haikuwa kwao ni Ishara kwamba wanayajua haya wanazuoni wa Wana wa Israili?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 198

وَلَوۡ نَزَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ بَعۡضِ ٱلۡأَعۡجَمِينَ

Na lau kuwa tungeli iteremsha juu ya mmoja wa wasio kuwa Waarabu,



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 199

فَقَرَأَهُۥ عَلَيۡهِم مَّا كَانُواْ بِهِۦ مُؤۡمِنِينَ

Na akawasomea, wasingeli kuwa wenye kuamini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 200

كَذَٰلِكَ سَلَكۡنَٰهُ فِي قُلُوبِ ٱلۡمُجۡرِمِينَ

Namna hivi tunaingiza katika nyoyo za wakosefu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 201

لَا يُؤۡمِنُونَ بِهِۦ حَتَّىٰ يَرَوُاْ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَلِيمَ

Hawataiamini mpaka waione adhabu chungu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 202

فَيَأۡتِيَهُم بَغۡتَةٗ وَهُمۡ لَا يَشۡعُرُونَ

Basi itawafikia kwa ghafla, na hali hawana khabari



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 203

فَيَقُولُواْ هَلۡ نَحۡنُ مُنظَرُونَ

Na watasema: Je, tutapewa muhula?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 204

أَفَبِعَذَابِنَا يَسۡتَعۡجِلُونَ

Basi, je, wanaihimiza adhabu yetu?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 205

أَفَرَءَيۡتَ إِن مَّتَّعۡنَٰهُمۡ سِنِينَ

Waonaje kama tukiwastarehesha kwa miaka



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 206

ثُمَّ جَآءَهُم مَّا كَانُواْ يُوعَدُونَ

Kisha yakawafikia waliyo kuwa wakiahidiwa,



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 207

مَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يُمَتَّعُونَ

Yatawafaa nini yale waliyo stareheshewa?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 208

وَمَآ أَهۡلَكۡنَا مِن قَرۡيَةٍ إِلَّا لَهَا مُنذِرُونَ

Wala hatukuangamiza mji wowote ila ulikuwa na waonyaji



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 209

ذِكۡرَىٰ وَمَا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Kuwa ni ukumbusho. Wala Sisi hatukuwa wenye kudhulumu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 210

وَمَا تَنَزَّلَتۡ بِهِ ٱلشَّيَٰطِينُ

Wala Mashet’ani hawakuteremka nayo,