Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 121

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo ishara, lakini si wengi wao waliokuwa waumini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 122

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 123

كَذَّبَتۡ عَادٌ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kina A’d waliwakanusha Mitume



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 124

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ هُودٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao, Hud: Je! Hamumchi Allah?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 125

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 126

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini mimi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 127

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala sikutakeni juu yake ujira, kwani ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 128

أَتَبۡنُونَ بِكُلِّ رِيعٍ ءَايَةٗ تَعۡبَثُونَ

Je! Mnajenga juu ya kila mnyanyuko kumbusho la kufanyia upuuzi?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 129

وَتَتَّخِذُونَ مَصَانِعَ لَعَلَّكُمۡ تَخۡلُدُونَ

Na mnajenga majengo ya fakhari kama kwamba mtaishi milele!



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 130

وَإِذَا بَطَشۡتُم بَطَشۡتُمۡ جَبَّارِينَ

Na mnapotumia nguvu mnatumia nguvu kwa ujabari



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 131

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 132

وَٱتَّقُواْ ٱلَّذِيٓ أَمَدَّكُم بِمَا تَعۡلَمُونَ

Na mcheni aliye kupeni haya mnayo yajua



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 133

أَمَدَّكُم بِأَنۡعَٰمٖ وَبَنِينَ

Amekupeni wanyama wa kufuga na watoto



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 134

وَجَنَّـٰتٖ وَعُيُونٍ

Na mabustani na chemchem



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 135

إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ

Hakika mimi ninakukhofieni adhabu ya Siku kubwa



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 136

قَالُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡنَآ أَوَعَظۡتَ أَمۡ لَمۡ تَكُن مِّنَ ٱلۡوَٰعِظِينَ

Wakasema: Ni sawasawa kwetu, ukitupa mawaidha au hukuwa miongoni mwa watoao mawaidha



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 137

إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا خُلُقُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Haya si chochote ila ni mtindo wa watu wa tokea zamani



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 138

وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ

Wala sisi hatutaadhibiwa



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 139

فَكَذَّبُوهُ فَأَهۡلَكۡنَٰهُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Wakamkanusha; nasi tukawaan-gamiza. Hakika bila ya shaka katika haya ipo Ishara. Lakini hawakuwa wengi wao wenye kuamini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 140

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 141

كَذَّبَتۡ ثَمُودُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kina Thamud waliwakanusha Mitume



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 142

إِذۡ قَالَ لَهُمۡ أَخُوهُمۡ صَٰلِحٌ أَلَا تَتَّقُونَ

Alipo waambia ndugu yao Saleh: Je! Hamumchi Allah?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 143

إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Hakika mimi kwenu ni Mtume muaminifu



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 144

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 145

وَمَآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ مِنۡ أَجۡرٍۖ إِنۡ أَجۡرِيَ إِلَّا عَلَىٰ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala sikutakini ujira juu yake. Ujira wangu hauko ila kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 146

أَتُتۡرَكُونَ فِي مَا هَٰهُنَآ ءَامِنِينَ

Je! Mtaachwa salama usalimina katika haya yaliyopo hapa?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 147

فِي جَنَّـٰتٖ وَعُيُونٖ

Katika mabustani, na chemchem?



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 148

وَزُرُوعٖ وَنَخۡلٖ طَلۡعُهَا هَضِيمٞ

Na konde na mitende yenye makole yaliyo wiva



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 149

وَتَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتٗا فَٰرِهِينَ

Na mnachonga milimani majumba kwa ustadi



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 150

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Basi mcheni Allah, na nitiini mimi