Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali, (hakumsadiki Mtume wala Qur’ani)



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 32

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Lakini alikadhibisha na akakengeuka



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Kisha akaenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 34

أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ

Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 35

ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ

Kisha! Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 36

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى

Je, mwanadamu anadhani kuwa ataachwa bure tu?



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 37

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 39

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 40

أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ

Je! Huyo (aliyefanya hivyo) hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?