Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 31

فَحَقَّ عَلَيۡنَا قَوۡلُ رَبِّنَآۖ إِنَّا لَذَآئِقُونَ

Basi hukumu ya Mola wetu Mlezi imekwisha tuthibitikia. Hakika bila ya shaka tutaonja tu adhabu



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 32

فَأَغۡوَيۡنَٰكُمۡ إِنَّا كُنَّا غَٰوِينَ

Tulikupotezeni kwasababu sisi wenyewe tulikuwa wapotovu



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 33

فَإِنَّهُمۡ يَوۡمَئِذٖ فِي ٱلۡعَذَابِ مُشۡتَرِكُونَ

Basi wao kwa hakika siku hiyo watashirikiana katika adhabu pamoja



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 34

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَفۡعَلُ بِٱلۡمُجۡرِمِينَ

Hivyo ndivyo tutakavyo wafanyia wakosefu



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 35

إِنَّهُمۡ كَانُوٓاْ إِذَا قِيلَ لَهُمۡ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا ٱللَّهُ يَسۡتَكۡبِرُونَ

Wao walipo kuwa wakiambiwa La ilaha illa ‘LLahu Hapana mungu ila Allah tu, wanafanya kiburi



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 36

وَيَقُولُونَ أَئِنَّا لَتَارِكُوٓاْ ءَالِهَتِنَا لِشَاعِرٖ مَّجۡنُونِۭ

Na wakisema: Hivyo sisi tuiache miungu yetu kwa ajili ya huyu mtunga mashairi mwendawazimu?



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 37

بَلۡ جَآءَ بِٱلۡحَقِّ وَصَدَّقَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Bali huyu amekuja kwa Haki, na amewasadikisha Mitume



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 38

إِنَّكُمۡ لَذَآئِقُواْ ٱلۡعَذَابِ ٱلۡأَلِيمِ

Hakika nyinyi bila ya shaka mtaionja adhabu chungu



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 39

وَمَا تُجۡزَوۡنَ إِلَّا مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Wala hamlipwi ila hayo mliyo kuwa mkiyafanya



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 40

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Allah walio chaguliwa



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 41

أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمۡ رِزۡقٞ مَّعۡلُومٞ

Hao ndio watakao pata riziki maalumu,



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 42

فَوَٰكِهُ وَهُم مُّكۡرَمُونَ

Matunda, nao wataheshimiwa



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 43

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

Katika Bustani za neema



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 44

عَلَىٰ سُرُرٖ مُّتَقَٰبِلِينَ

Wako juu ya viti wanatazamana



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 45

يُطَافُ عَلَيۡهِم بِكَأۡسٖ مِّن مَّعِينِۭ

Wanazungushiwa kikombe chenye kinywaji cha chemchem



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 46

بَيۡضَآءَ لَذَّةٖ لِّلشَّـٰرِبِينَ

Kinywaji cheupe, kitamu kwa wanywao



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 47

لَا فِيهَا غَوۡلٞ وَلَا هُمۡ عَنۡهَا يُنزَفُونَ

Hakina madhara, wala hakiwaleweshi



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 48

وَعِندَهُمۡ قَٰصِرَٰتُ ٱلطَّرۡفِ عِينٞ

Na watakuwa nao wanawake wenye macho ya staha mazuri



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 49

كَأَنَّهُنَّ بَيۡضٞ مَّكۡنُونٞ

Hao wanawake kama mayai yaliyo hifadhika



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 50

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Waingie kuulizana wenyewe kwa wenyewe



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 51

قَالَ قَآئِلٞ مِّنۡهُمۡ إِنِّي كَانَ لِي قَرِينٞ

Aseme msemaji mmoja miongoni mwao: Hakika mimi nalikuwa na rafiki



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 52

يَقُولُ أَءِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُصَدِّقِينَ

Aliye kuwa akinambia: Hivyo wewe ni katika wanao sadiki



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 53

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَدِينُونَ

Ati tukisha kufa tukawa udongo na mifupa, ndio tutalipwa na kuhesabiwa?



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 54

قَالَ هَلۡ أَنتُم مُّطَّلِعُونَ

Atasema: Je! Nyie mnawaona?



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 55

فَٱطَّلَعَ فَرَءَاهُ فِي سَوَآءِ ٱلۡجَحِيمِ

Basi atachungulia amwone katikati ya Jahannamu



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 56

قَالَ تَٱللَّهِ إِن كِدتَّ لَتُرۡدِينِ

Atasema: Wallahi! Ulikaribia kunipoteza



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 57

وَلَوۡلَا نِعۡمَةُ رَبِّي لَكُنتُ مِنَ ٱلۡمُحۡضَرِينَ

Na lau kuwa si neema ya Mola wangu Mlezi bila ya shaka ningelikuwa miongoni mwa walio hudhurishwa



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 58

أَفَمَا نَحۡنُ بِمَيِّتِينَ

Je! Sisi hatutakufa,



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 59

إِلَّا مَوۡتَتَنَا ٱلۡأُولَىٰ وَمَا نَحۡنُ بِمُعَذَّبِينَ

Isipo kuwa kifo chetu cha kwanza? Wala sisi hatutaadhibiwa



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 60

إِنَّ هَٰذَا لَهُوَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Hakika huku bila ya shaka ndiko kufuzu kukubwa