Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 31

ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قَرۡنًا ءَاخَرِينَ

Kisha baada yao tukaanzisha kizazi kingine



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 32

فَأَرۡسَلۡنَا فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ

Tukawapelekea Mtume miongoni mwao, kuwaambia: Muabuduni Allah! Hamna mungu asiye kuwa Yeye. Jee, hamuogopi?



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 33

وَقَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِهِ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱلۡأٓخِرَةِ وَأَتۡرَفۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَا مَا هَٰذَآ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُكُمۡ يَأۡكُلُ مِمَّا تَأۡكُلُونَ مِنۡهُ وَيَشۡرَبُ مِمَّا تَشۡرَبُونَ

Na wakasema wakubwa katika watu wake waliokufuru na kukadhibisha mkutano wa Akhera na tuliwatajirisha katika maisha ya dunia, huyu siye ila ni mtu kama nyinyi anakula katika vile mnavyokula na anakunywa katika vile mnavyokunywa



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 34

وَلَئِنۡ أَطَعۡتُم بَشَرٗا مِّثۡلَكُمۡ إِنَّكُمۡ إِذٗا لَّخَٰسِرُونَ

Na lau mtamtii binadamu kama nyinyi, basi nyinyi mtakuwa ni wenye kupata hasara (kwa kuwaacha waungu wenu na kumfuata yeye)



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 35

أَيَعِدُكُمۡ أَنَّكُمۡ إِذَا مِتُّمۡ وَكُنتُمۡ تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَنَّكُم مُّخۡرَجُونَ

Hivyo anakuahidini ati ya kwamba mtakapo kufa na mkawa udongo na mifupa kuwa mtatolewa?



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 36

۞هَيۡهَاتَ هَيۡهَاتَ لِمَا تُوعَدُونَ

Hayawi! Hayawi hayo mnayo ahidiwa



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 37

إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا نَمُوتُ وَنَحۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ

Hapana ila uhai wetu wa duniani tu, tunakufa na kuishi basi. Wala sisi hatutafufuliwa



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 38

إِنۡ هُوَ إِلَّا رَجُلٌ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبٗا وَمَا نَحۡنُ لَهُۥ بِمُؤۡمِنِينَ

Huyu si lolote ila ni mtu anaye mzulia Allah uongo, wala sisi sio wa kumuamini



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 39

قَالَ رَبِّ ٱنصُرۡنِي بِمَا كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Ninusuru kwasababu wananikanusha



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 40

قَالَ عَمَّا قَلِيلٖ لَّيُصۡبِحُنَّ نَٰدِمِينَ

(Allah) akasema: Baada ya muda mchache watakuwa wenye kujuta



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 41

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ بِٱلۡحَقِّ فَجَعَلۡنَٰهُمۡ غُثَآءٗۚ فَبُعۡدٗا لِّلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Basi ukawanyakua ukelele kwa haki, na tukawafanya kama takataka zinazo elea juu ya maji. Ikapotelea mbali kaumu ya madhalimu!



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 42

ثُمَّ أَنشَأۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِمۡ قُرُونًا ءَاخَرِينَ

Kisha tukaleta baada yao vizazi vingine



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 43

مَا تَسۡبِقُ مِنۡ أُمَّةٍ أَجَلَهَا وَمَا يَسۡتَـٔۡخِرُونَ

Hapana umma uwezao kutan-guliza ajali yake wala kuikawiza



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 44

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا رُسُلَنَا تَتۡرَاۖ كُلَّ مَا جَآءَ أُمَّةٗ رَّسُولُهَا كَذَّبُوهُۖ فَأَتۡبَعۡنَا بَعۡضَهُم بَعۡضٗا وَجَعَلۡنَٰهُمۡ أَحَادِيثَۚ فَبُعۡدٗا لِّقَوۡمٖ لَّا يُؤۡمِنُونَ

Kisha tukawatuma Mitume wetu, mmoja baada ya mmoja. Kila umma alipo wafikia Mtume wao walimkanusha. Tukawafua-tanisha hawa baada ya hawa, na tukawafanya ni hadithi za kusimuliwa. Wakapotelea mbali watu wasio amini



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 45

ثُمَّ أَرۡسَلۡنَا مُوسَىٰ وَأَخَاهُ هَٰرُونَ بِـَٔايَٰتِنَا وَسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Kisha tukamtuma Mussa na nduguye, Haaruni, pamoja na ishara zetu na hoja zilizo wazi



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 46

إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ وَمَلَإِيْهِۦ فَٱسۡتَكۡبَرُواْ وَكَانُواْ قَوۡمًا عَالِينَ

Kumwendea Firauni na wakuu wake. Lakini walijivuna, nao walikuwa watu majeuri



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 47

فَقَالُوٓاْ أَنُؤۡمِنُ لِبَشَرَيۡنِ مِثۡلِنَا وَقَوۡمُهُمَا لَنَا عَٰبِدُونَ

Wakasema: Je, tuwaamini wawili hawa wanaadamu kama sisi, na ambao watu wao ni watumwa wetu?



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 48

فَكَذَّبُوهُمَا فَكَانُواْ مِنَ ٱلۡمُهۡلَكِينَ

Basi wakawakanusha, na wakawa miongoni mwa walio angamizwa



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 49

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ لَعَلَّهُمۡ يَهۡتَدُونَ

Na hakika tulimpa Mussa Kitabu ili wapate kuongoka



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 50

وَجَعَلۡنَا ٱبۡنَ مَرۡيَمَ وَأُمَّهُۥٓ ءَايَةٗ وَءَاوَيۡنَٰهُمَآ إِلَىٰ رَبۡوَةٖ ذَاتِ قَرَارٖ وَمَعِينٖ

Na tukamfanya mwana wa Mariamu na mama yake kuwa ni Ishara, na tukawapa makimbilio kwenda mahali palipo inuka penye utulivu na chemchem za maji



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 51

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلرُّسُلُ كُلُواْ مِنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَٱعۡمَلُواْ صَٰلِحًاۖ إِنِّي بِمَا تَعۡمَلُونَ عَلِيمٞ

Enyi Mitume! Kuleni vyakula vizuri na tendeni mema. Hakika Mimi ni Mjuzi wa mnayo yatenda



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 52

وَإِنَّ هَٰذِهِۦٓ أُمَّتُكُمۡ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ وَأَنَا۠ رَبُّكُمۡ فَٱتَّقُونِ

Na kwa yakini huu Umma wenu ni Umma mmoja, na Mimi ni Mola wenu Mlezi, basi nicheni Mimi



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 53

فَتَقَطَّعُوٓاْ أَمۡرَهُم بَيۡنَهُمۡ زُبُرٗاۖ كُلُّ حِزۡبِۭ بِمَا لَدَيۡهِمۡ فَرِحُونَ

Lakini walikatiana jambo lao mapande mbali mbali. Kila kundi likifurahia kwa waliyo nayo



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 54

فَذَرۡهُمۡ فِي غَمۡرَتِهِمۡ حَتَّىٰ حِينٍ

Basi waache katika ghafla yao kwa muda



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 55

أَيَحۡسَبُونَ أَنَّمَا نُمِدُّهُم بِهِۦ مِن مَّالٖ وَبَنِينَ

Je! Wanadhani ya kuwa kwa vile tunavyo wapa mali na watoto



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 56

نُسَارِعُ لَهُمۡ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۚ بَل لَّا يَشۡعُرُونَ

Ndio tunawahimizia kheri? Lakini wenyewe hawatambui



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 57

إِنَّ ٱلَّذِينَ هُم مِّنۡ خَشۡيَةِ رَبِّهِم مُّشۡفِقُونَ

Kwa hakika hao ambao kwa kumwogopa Mola wao Mlezi wananyenyekea



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 58

وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِ رَبِّهِمۡ يُؤۡمِنُونَ

Na wale ambao Ishara za Mola wao Mlezi wanaziamini



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 59

وَٱلَّذِينَ هُم بِرَبِّهِمۡ لَا يُشۡرِكُونَ

Na wale ambao hawa mshirikishi Mola wao Mlezi



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 60

وَٱلَّذِينَ يُؤۡتُونَ مَآ ءَاتَواْ وَّقُلُوبُهُمۡ وَجِلَةٌ أَنَّهُمۡ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ رَٰجِعُونَ

Na wale ambao wanatoa walicho pewa, na hali nyoyo zao zinaogopa kwa kuwa watarejea kwa Mola wao Mlezi,