Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 31

وَلَوۡ أَنَّ قُرۡءَانٗا سُيِّرَتۡ بِهِ ٱلۡجِبَالُ أَوۡ قُطِّعَتۡ بِهِ ٱلۡأَرۡضُ أَوۡ كُلِّمَ بِهِ ٱلۡمَوۡتَىٰۗ بَل لِّلَّهِ ٱلۡأَمۡرُ جَمِيعًاۗ أَفَلَمۡ يَاْيۡـَٔسِ ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ أَن لَّوۡ يَشَآءُ ٱللَّهُ لَهَدَى ٱلنَّاسَ جَمِيعٗاۗ وَلَا يَزَالُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ تُصِيبُهُم بِمَا صَنَعُواْ قَارِعَةٌ أَوۡ تَحُلُّ قَرِيبٗا مِّن دَارِهِمۡ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ وَعۡدُ ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُخۡلِفُ ٱلۡمِيعَادَ

(Hii Qur’an ilitosha kabisa kuwa muujiza, lau wangekuwa na akili) Na kama ingelikuwa (hii) Qur’ani ndiyo itumikayo kung’olea milima (kwa kule kuteremka na kusomwa kwake), au kupasuliwa ardhi (ili iwe mito, n.k) na kusemeshewa wafu (kusomewa ili wawe hai), (basi ingelikuwa hii Qur’ani! Na pia wasingeamini). Bali mambo yote ni ya Allah. Je, hawajajua walioamini kwamba lau Allah angependa bila ya shaka angewaongoa watu wote (wawe waumini)? Wala wale waliokufuru hawaachi kusibiwa na majanga kwa waliyoyatenda, au ikawateremkia (adhabu) karibu na nyumbani kwao, mpaka ifike ahadi ya Allah. Hakika Allah havunji miadi yake



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 32

وَلَقَدِ ٱسۡتُهۡزِئَ بِرُسُلٖ مِّن قَبۡلِكَ فَأَمۡلَيۡتُ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ ثُمَّ أَخَذۡتُهُمۡۖ فَكَيۡفَ كَانَ عِقَابِ

Na hakika walifanyiwa kejeli Mitume waliokuwa kabla yako. Na nikawapa muda (wa kujitafakari na kutubu) wale waliokufuru, kisha nikawashika (kwa adhabu kali), Basi ilikuwaje adhabu yangu (itokanayo na shere na kufuru zao)!?



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 33

أَفَمَنۡ هُوَ قَآئِمٌ عَلَىٰ كُلِّ نَفۡسِۭ بِمَا كَسَبَتۡۗ وَجَعَلُواْ لِلَّهِ شُرَكَآءَ قُلۡ سَمُّوهُمۡۚ أَمۡ تُنَبِّـُٔونَهُۥ بِمَا لَا يَعۡلَمُ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَم بِظَٰهِرٖ مِّنَ ٱلۡقَوۡلِۗ بَلۡ زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ مَكۡرُهُمۡ وَصُدُّواْ عَنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَن يُضۡلِلِ ٱللَّهُ فَمَا لَهُۥ مِنۡ هَادٖ

Je, (analingana sawa yule) Msimamizi wa kila nafsi (na Mjuzi) wa wachumayo, na wakamfanyia Allah washirika! Sema watajeni. Au ndio mnampa (Allah) habari ya (washirika) asio na habari nao katika (mbingu na) ardhi; au (ndio mnawasifu hao washirika) kwa maneno matupu? Bali waliokufuru wamepambiwa vitimbi vyao na wamezuiliwa njia (ya haki). Na ambaye Allah amemuacha apotee basi hana wa kumuongoa



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 34

لَّهُمۡ عَذَابٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَشَقُّۖ وَمَا لَهُم مِّنَ ٱللَّهِ مِن وَاقٖ

(Hao makafiri) Wana adhabu katika maisha ya dunia, na adhabu ya Akhera ni nzito mno. Na wala hawatakuwa na wa kuwahami na (adhabu ya) Allah



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 35

۞مَّثَلُ ٱلۡجَنَّةِ ٱلَّتِي وُعِدَ ٱلۡمُتَّقُونَۖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ أُكُلُهَا دَآئِمٞ وَظِلُّهَاۚ تِلۡكَ عُقۡبَى ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْۚ وَّعُقۡبَى ٱلۡكَٰفِرِينَ ٱلنَّارُ

Mfano wa Pepo waliyoahidiwa wacha Mungu, inapita mbele yake mito, matunda yake hayana msimu, na pia kivuli chake. Huu ndio mwisho wa wale waliojilinda. Na mwisho wa makafiri ni Moto



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 36

وَٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ يَفۡرَحُونَ بِمَآ أُنزِلَ إِلَيۡكَۖ وَمِنَ ٱلۡأَحۡزَابِ مَن يُنكِرُ بَعۡضَهُۥۚ قُلۡ إِنَّمَآ أُمِرۡتُ أَنۡ أَعۡبُدَ ٱللَّهَ وَلَآ أُشۡرِكَ بِهِۦٓۚ إِلَيۡهِ أَدۡعُواْ وَإِلَيۡهِ مَـَٔابِ

Na wale tuliowapa Kitabu wanafurahia yale uliyoteremshiwa[1]. Na katika makundi mengine wapo wanaoyakataa baadhi yake[2]. Sema: Nimeamrishwa nimuabudu Allah, na wala nisimshirikishe. Kuelekea kwake Yeye tu ndiyo ninaita (watu), na kwake Yeye tu ndio marejeo yangu


1- - Wanaolengwa kuifurahikia Qura’n hapa ni wale wa Yahudi waliosilimu katika enzi za Mtume akiwemo
Abdallah bin Salam na wenzake.

2- - Na wapo baadhi ya Wayahudi kama vile Ka’b bin Al-ashraf na wenzake walikuwa wanayapinga wazi wazi
baadhi ya yale yaliyoteremshwa kwa Mtume.


Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 37

وَكَذَٰلِكَ أَنزَلۡنَٰهُ حُكۡمًا عَرَبِيّٗاۚ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم بَعۡدَ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ مَا لَكَ مِنَ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا وَاقٖ

Na kama hivi (tulivyoiteremsha hii Qur’an ikiwa imesheheni misingi ya dini) tumeiteremsha (pia hii) Qur’ani kuwa ni hukumu (kwa lugha ya) Kiarabu (ili ifahamike na kuhifadhiwa kwa wepesi). Na ukifuata matamanio yao baada ya kukujia elimu, hutakuwa na rafiki wala mlinzi wa kukukinga (na adhabu ya Allah



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 38

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا رُسُلٗا مِّن قَبۡلِكَ وَجَعَلۡنَا لَهُمۡ أَزۡوَٰجٗا وَذُرِّيَّةٗۚ وَمَا كَانَ لِرَسُولٍ أَن يَأۡتِيَ بِـَٔايَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ لِكُلِّ أَجَلٖ كِتَابٞ

Na hakika Sisi tuliwatuma Mitume kabla yako, na tukawajaalia wawe na wake na watoto dhuriya (kama ulivyo wewe). Na haiwi kwa Mtume kuleta miujiza isipokuwa kwa idhini ya Allah. Kila kipindi kina hukumu yake



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 39

يَمۡحُواْ ٱللَّهُ مَا يَشَآءُ وَيُثۡبِتُۖ وَعِندَهُۥٓ أُمُّ ٱلۡكِتَٰبِ

Allah hufuta na huthibitisha ayatakayo (katika hukumu zake). Na asili ya hukumu zote ipo kwake



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 40

وَإِن مَّا نُرِيَنَّكَ بَعۡضَ ٱلَّذِي نَعِدُهُمۡ أَوۡ نَتَوَفَّيَنَّكَ فَإِنَّمَا عَلَيۡكَ ٱلۡبَلَٰغُ وَعَلَيۡنَا ٱلۡحِسَابُ

Na iwapo tutakuonesha baadhi ya (adhabu) tulizowaahidi au tukakufisha kabla yake (kabla ya kuwaadhibu), haikuwa jukumu lako wewe isipokuwa ni kufikisha ujumbe na juu yetu ni hesabu



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 41

أَوَلَمۡ يَرَوۡاْ أَنَّا نَأۡتِي ٱلۡأَرۡضَ نَنقُصُهَا مِنۡ أَطۡرَافِهَاۚ وَٱللَّهُ يَحۡكُمُ لَا مُعَقِّبَ لِحُكۡمِهِۦۚ وَهُوَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

Je, (watu wa Makkah na wengine) hawaoni tunavyo ipunguza ardhi (wanayoishi) nchani mwake?[1] Na Allah anahukumu, na hapana wa kupinga hukumu yake, naye ni Mwepesi wa kuhesabu


1- - Kusudio la kupunguzwa kwa ardhi hapa, ni pamoja na kuangamizwa na kutawaliwa na Waislamu baadhi
ya mipaka au maeneo yake.


Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 42

وَقَدۡ مَكَرَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَلِلَّهِ ٱلۡمَكۡرُ جَمِيعٗاۖ يَعۡلَمُ مَا تَكۡسِبُ كُلُّ نَفۡسٖۗ وَسَيَعۡلَمُ ٱلۡكُفَّـٰرُ لِمَنۡ عُقۡبَى ٱلدَّارِ

Na (hawa makafiri) walishafanya vitimbi (kwa Manabii) waliokuwa kabla yao, lakini Allah ndiye Mwenye mipango yote. Yeye anajua inayo chuma kila nafsi. Na makafiri watajua ni ya nani nyumba ya mwisho Akhera



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 43

وَيَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ لَسۡتَ مُرۡسَلٗاۚ قُلۡ كَفَىٰ بِٱللَّهِ شَهِيدَۢا بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡ وَمَنۡ عِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡكِتَٰبِ

Na wanasema waliokufuru: Wewe hukutumwa (si Mtume wa Allah). Sema: Allah anatosha kuwa shahidi baina yangu na nyinyi (kuhusu usahihi wa Utume wangu), na pia yule mwenye elimu ya Kitabu (kama anakiamini kitabu chake)