وَأَخۡرَجَتِ ٱلۡأَرۡضُ أَثۡقَالَهَا
Na itakapo toa ardhi mizigo yake!
Compartir :
وَقَالَ ٱلۡإِنسَٰنُ مَا لَهَا
Na mtu akasema: Ina nini?
يَوۡمَئِذٖ تُحَدِّثُ أَخۡبَارَهَا
Siku hiyo itahadithia khabari zake
بِأَنَّ رَبَّكَ أَوۡحَىٰ لَهَا
Kwasababu Mola wake Mlezi ameifunulia!
يَوۡمَئِذٖ يَصۡدُرُ ٱلنَّاسُ أَشۡتَاتٗا لِّيُرَوۡاْ أَعۡمَٰلَهُمۡ
Siku hiyo watu watatoka wakiwa tofauti tofauti wakaonyweshwe vitendo vyao!
فَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٍ خَيۡرٗا يَرَهُۥ
Basi anaye tenda chembe ya wema, atauona!
وَمَن يَعۡمَلۡ مِثۡقَالَ ذَرَّةٖ شَرّٗا يَرَهُۥ
Na anaye tenda chembe ya uovu atauona!
۞أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ
Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?
وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ
Na yakakusanywa yaliyomo vifuani?
إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ
Kwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!
ٱلۡقَارِعَةُ
Inayo gonga!
مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Nini Inayo gonga?
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡقَارِعَةُ
Na nini kitakacho kujuilisha nini Inayo gonga?
يَوۡمَ يَكُونُ ٱلنَّاسُ كَٱلۡفَرَاشِ ٱلۡمَبۡثُوثِ
Siku ambayo watu watakuwa kama nondo (vipepeo) walio tawanyika;
وَتَكُونُ ٱلۡجِبَالُ كَٱلۡعِهۡنِ ٱلۡمَنفُوشِ
Na milima itakuwa kama sufi zilizo chambuliwa!
فَأَمَّا مَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Basi yule ambaye mizani yake itakuwa nzito,
فَهُوَ فِي عِيشَةٖ رَّاضِيَةٖ
Huyo atakuwa katika maisha ya kupendeza
وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ
Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,
فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ
Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!
وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ
Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?
نَارٌ حَامِيَةُۢ
Ni Moto mkali!