Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 27

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

(Walivyo tanabahi!): wakasema Bali sisi tumenyimwa (mavuno yake)!



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 28

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Allah (kuiacha nia yenu mbaya)?



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 29

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: utukufu ni wa mola wetu, hakika tulikuwa wenye kudhulumu



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 30

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 31

قَالُواْ يَٰوَيۡلَنَآ إِنَّا كُنَّا طَٰغِينَ

Wakasema: Ole wetu! Hakika sisi tumekuwa warukao mipaka



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 32

عَسَىٰ رَبُّنَآ أَن يُبۡدِلَنَا خَيۡرٗا مِّنۡهَآ إِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا رَٰغِبُونَ

Asaa Mola wetu akatubadilishia lilio bora kuliko hili. Hakika sisi ni wenye kurejea kwa Mola wetu Mlezi



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 33

كَذَٰلِكَ ٱلۡعَذَابُۖ وَلَعَذَابُ ٱلۡأٓخِرَةِ أَكۡبَرُۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Kama hivyo ndivyo inakuwa adhabu (ya hapa duniani), bila shaka adhabu ya akhera ni kubwa zaidi, laiti wangalijua!