Capítulo: QAAF 

Verso : 45

نَّحۡنُ أَعۡلَمُ بِمَا يَقُولُونَۖ وَمَآ أَنتَ عَلَيۡهِم بِجَبَّارٖۖ فَذَكِّرۡ بِٱلۡقُرۡءَانِ مَن يَخَافُ وَعِيدِ

Sisi tunayajua wanayoyasema na wewe hukuwa mwenye kuwatenza nguvu, basi wakumbushe kwa Qur’ani yeyote mwenye kuogopa onyo langu



Capítulo: ADH-DHAARIYAAT 

Verso : 55

وَذَكِّرۡ فَإِنَّ ٱلذِّكۡرَىٰ تَنفَعُ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na kumbusha hakika ukumbusho unawanufaisha waumini



Capítulo: ATTUR 

Verso : 48

وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Na subiri hukumu ya mola wako mlezi na hakika wewe uko machoni kwetu (uangalizi wetu) na msabihi Mola wako mlezi pamoja na kusifu wakati unapoamka



Capítulo: ATTUR 

Verso : 49

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Na katika usiku Msabbih na zinapokuchwa nyota



Capítulo: AL-MUMTAHINA 

Verso : 12

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ إِذَا جَآءَكَ ٱلۡمُؤۡمِنَٰتُ يُبَايِعۡنَكَ عَلَىٰٓ أَن لَّا يُشۡرِكۡنَ بِٱللَّهِ شَيۡـٔٗا وَلَا يَسۡرِقۡنَ وَلَا يَزۡنِينَ وَلَا يَقۡتُلۡنَ أَوۡلَٰدَهُنَّ وَلَا يَأۡتِينَ بِبُهۡتَٰنٖ يَفۡتَرِينَهُۥ بَيۡنَ أَيۡدِيهِنَّ وَأَرۡجُلِهِنَّ وَلَا يَعۡصِينَكَ فِي مَعۡرُوفٖ فَبَايِعۡهُنَّ وَٱسۡتَغۡفِرۡ لَهُنَّ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Ewe Nabii! Wakikujia Waumini wa kike wanafungamana nawe ahadi ya utiifu kwamba hawata mshirikisha Allah na chochote, na wala hawatoiba, na wala hawatozini, na wala hawataua watoto wao, na wala hawatoleta usingiziaji wa kashfa walioizua baina ya mikono yao na miguu yao na wala hawatakuasi katika mema; basi pokea ahadi yao ya utiifu, na waombee maghfirah kwa Allaah. Hakika Allah ni Mwingi wa kughufuria, Mwenye kurehemu



Capítulo: ATTAGHAABUN 

Verso : 12

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَإِنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah, na mt’iini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha (Ujumbe wake) kwa uwazi tu



Capítulo: ATTAHRIIM 

Verso : 9

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّبِيُّ جَٰهِدِ ٱلۡكُفَّارَ وَٱلۡمُنَٰفِقِينَ وَٱغۡلُظۡ عَلَيۡهِمۡۚ وَمَأۡوَىٰهُمۡ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Ee Nabii! Pambana na makafiri na wanafiki na kuwa mshupavu kwao, na makazi yao ni Motoni. Na ni mahali pabaya palioje pa kufikia



Capítulo: ALJINN 

Verso : 23

إِلَّا بَلَٰغٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِسَٰلَٰتِهِۦۚ وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَإِنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًا

Isipokuwa nifikishe Ujumbe utokao kwa Allah, na ujumbe wake. Na wenye kumuasi Allah na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُزَّمِّلُ

Ewe uliye jifunika



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 2

قُمِ ٱلَّيۡلَ إِلَّا قَلِيلٗا

Simama usiku kucha (kuswali) isipokuwa kidogo tu



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 3

نِّصۡفَهُۥٓ أَوِ ٱنقُصۡ مِنۡهُ قَلِيلًا

Nusu yake au ipunguze kidogo



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 4

أَوۡ زِدۡ عَلَيۡهِ وَرَتِّلِ ٱلۡقُرۡءَانَ تَرۡتِيلًا

Au izidishe, na soma Qurani vizuri (kwa kufuata kanuni, sheria na taratibu zake)



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 7

إِنَّ لَكَ فِي ٱلنَّهَارِ سَبۡحٗا طَوِيلٗا

Kwani hakika mchana una shughuli nyingi



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 8

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ وَتَبَتَّلۡ إِلَيۡهِ تَبۡتِيلٗا

Na litaje Jina la Mola wako, na jitolee Kwake kikamilifu



Capítulo: ALMUZZAMMIL 

Verso : 10

وَٱصۡبِرۡ عَلَىٰ مَا يَقُولُونَ وَٱهۡجُرۡهُمۡ هَجۡرٗا جَمِيلٗا

Na subiri juu ya yale wayasemayo, na uwaepuke muepuko wa wema



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 1

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلۡمُدَّثِّرُ

Ewe mwenye kujigubika



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 2

قُمۡ فَأَنذِرۡ

Simama uonye



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 3

وَرَبَّكَ فَكَبِّرۡ

Na Mola wako Mlezi mtukuze



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 4

وَثِيَابَكَ فَطَهِّرۡ

Na nguo zako zisafishe



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 5

وَٱلرُّجۡزَ فَٱهۡجُرۡ

Na (mambo) machafu yahame (yaache)



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 6

وَلَا تَمۡنُن تَسۡتَكۡثِرُ

Wala usitoe (usifanye hisani) kwa kutaraji kuzidishiwa (kupata kingi Zaidi)



Capítulo: ALMUDDATH-THIR 

Verso : 7

وَلِرَبِّكَ فَٱصۡبِرۡ

Na kwa ajili ya Mola wako tu kuwa na subira (kuwa mvumilivu)



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 16

لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ

Usiutikisie ulimi wako huu wahyi (ufunuo) kwa kuufanyia haraka



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 17

إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ

Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 18

فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ

Basi Tunapoisoma (kupitia Jibrili), fuata kusomwa kwake



Capítulo: ALQIYAAMA 

Verso : 19

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ

Kisha ni juu yetu kuubainisha



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 24

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعۡ مِنۡهُمۡ ءَاثِمًا أَوۡ كَفُورٗا

Basi ngojea hukumu ya Mola wako wala usimtii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kukufuru



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 25

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلٗا

Na litaje jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni



Capítulo: AL-INSAAN

Verso : 26

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَٱسۡجُدۡ لَهُۥ وَسَبِّحۡهُ لَيۡلٗا طَوِيلًا

Na usiku msujudie Yeye, na umtakase, (usali kwaajili yake) usiku, wakati mrefu



Capítulo: AL-AALAA 

Verso : 9

فَذَكِّرۡ إِن نَّفَعَتِ ٱلذِّكۡرَىٰ

Basi kumbusha, kama kukumbusha kunafaa