وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۖ وَيُرۡسِلُ عَلَيۡكُمۡ حَفَظَةً حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ تَوَفَّتۡهُ رُسُلُنَا وَهُمۡ لَا يُفَرِّطُونَ
Na yeye tu ndiye Mwenye nguvu kubwa juu ya waja wake, na anatuma kwenu (Malaika) waangalizi (wanaowalinda binadamu na kutunza kumbukumbu za matendo yao)[1], mpaka kinapomfikia mmoja wenu kifo wajumbe wetu wanamfisha, na hawafanyi uzembe
1- - Rejea Aya ya 11, Sura Arraad (13).
يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ إِمَّا يَأۡتِيَنَّكُمۡ رُسُلٞ مِّنكُمۡ يَقُصُّونَ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتِي فَمَنِ ٱتَّقَىٰ وَأَصۡلَحَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ
Enyi wanadamu, watakapo kufikieni Mitume watokanao na nyinyi wakikuhadithieni Aya zangu[1], basi yeyote atakayekuwa na uchaMungu na akafanya mema basi hawatakuwa na hofu yoyote, na hawatahuzunika
1- - Aya hii wanaitumia baadhi ya watu ili kupotosha. Wanadai kwamba, utume bado unaendelea. Itikadi ya Watu wa Sun ana Jama a ni kwamba, utume umekoma kwa Mtume Muhammad. Hakuna Mtume mwingine baada yake. Tujiulize swali la msingi. Aya hapa kama inasema kuwa Mitume wanaendelea kuja je, hizo Aya za Allah wanazotakiwa kutusomea ziko wapi? Rejea Aya ya 40, Sura Al-ahzab (33). Pia rejea Aya ya 158 ya Sura Al-aaraf (7).
وَلَقَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞۖ فَمَا لَبِثَ أَن جَآءَ بِعِجۡلٍ حَنِيذٖ
Na hakika walikuja wajumbe wetu kwa Ibrahimu kwa bishara njema, wakasema: Salama! Naye akasema: salama! Haukupita muda akaleta ndama wa kuchoma
وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَا لُوطٗا سِيٓءَ بِهِمۡ وَضَاقَ بِهِمۡ ذَرۡعٗا وَقَالَ هَٰذَا يَوۡمٌ عَصِيبٞ
Na pindi wajumbe wetu walipo kuja kwa Lutwi’ alijihisi huzuni na akawaonea dhiki. Na akasema: Hii leo ni siku ngumu sana!
يُنَزِّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ بِٱلرُّوحِ مِنۡ أَمۡرِهِۦ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرُوٓاْ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱتَّقُونِ
Anateremsha Malaika (Jibrili) na wahyi kwa amri yake kwa amtakaye miongoni mwa waja wake (Mitume)(akiwaambia kuwa): Waonyeni watu, wajue kwamba: Hakika hakuna wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa mimi tu; basi niogopeni
قُلۡ نَزَّلَهُۥ رُوحُ ٱلۡقُدُسِ مِن رَّبِّكَ بِٱلۡحَقِّ لِيُثَبِّتَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَهُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُسۡلِمِينَ
Sema: Ameiteremsha Roho mtakatifu (Jibrili) kutoka kwa Mola wako mlezi kwa haki kabisa, ili kuwaimarisha wale walioamini, na kuwa mwongozo na habari njema kwa Waislamu
ٱللَّهُ يَصۡطَفِي مِنَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ رُسُلٗا وَمِنَ ٱلنَّاسِۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعُۢ بَصِيرٞ
Allah huteuwa Wajumbe mion-goni mwa Malaika na miongoni mwa watu. Hakika Allah ni Mwenye kusikia, Mwenye kuona
نَزَلَ بِهِ ٱلرُّوحُ ٱلۡأَمِينُ
Ameuteremsha Roho mua-minifu,(jibril)
وَلَمَّا جَآءَتۡ رُسُلُنَآ إِبۡرَٰهِيمَ بِٱلۡبُشۡرَىٰ قَالُوٓاْ إِنَّا مُهۡلِكُوٓاْ أَهۡلِ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةِۖ إِنَّ أَهۡلَهَا كَانُواْ ظَٰلِمِينَ
Na wajumbe wetu walipo mjia Ibrahim na bishara, walisema: Hakika sisi hapana shaka tutawaangamiza watu wa mji huu, kwani watu wake hakika wamekuwa madhaalimu
وَلَمَّآ أَن جَآءَتۡ رُسُلُنَا لُوطٗا سِيٓءَ بِهِمۡ وَضَاقَ بِهِمۡ ذَرۡعٗاۖ وَقَالُواْ لَا تَخَفۡ وَلَا تَحۡزَنۡ إِنَّا مُنَجُّوكَ وَأَهۡلَكَ إِلَّا ٱمۡرَأَتَكَ كَانَتۡ مِنَ ٱلۡغَٰبِرِينَ
Na wajumbe wetu walipo mfikia Lutwi, alihuzunika kwa ajili yao, na moyo uliona dhiki kwa ajili yao. Wakasema: Usiogope, wala usihuzunike. Hakika sisi tutakuokoa wewe na ahali zako, ila mkeo aliye miongoni mwa wataokaa nyuma
ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ فَاطِرِ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ جَاعِلِ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ رُسُلًا أُوْلِيٓ أَجۡنِحَةٖ مَّثۡنَىٰ وَثُلَٰثَ وَرُبَٰعَۚ يَزِيدُ فِي ٱلۡخَلۡقِ مَا يَشَآءُۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ
Sifa zote njema ni za Allah Muumba wa mbingu na ardhi, aliyewafanya Malaika wajumbe wenye mbawa, mbili mbili na tatu tatu na nne nne. Anazidisha atakacho katika kuumba. Hakika Allah ni Muweza sana wa kila kitu
أَمۡ يَحۡسَبُونَ أَنَّا لَا نَسۡمَعُ سِرَّهُمۡ وَنَجۡوَىٰهُمۚ بَلَىٰ وَرُسُلُنَا لَدَيۡهِمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanadhani kwamba hatusikii siri zao na minong’ono yao? Wapi! Na wajumbe wetu wapo karibu nao, wanayaandika
هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ضَيۡفِ إِبۡرَٰهِيمَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ
Je Imewafikia Habari Za Wageni Wa Ibrahimu Walio Wema (wanao heshimiwa?)
إِذۡ دَخَلُواْ عَلَيۡهِ فَقَالُواْ سَلَٰمٗاۖ قَالَ سَلَٰمٞ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ
Pale Walipoingia Kwake Wakasema Salama, Akasema Salama nyinyi ni Watu nisio kujueni
فَرَاغَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ فَجَآءَ بِعِجۡلٖ سَمِينٖ
Akaenda Kwa Ahli Yake Na Akaja Na Nyama Ya Ndama Aliye nona
فَقَرَّبَهُۥٓ إِلَيۡهِمۡ قَالَ أَلَا تَأۡكُلُونَ
Akawakaribisha na akasema Mbona Hamli?
فَأَوۡجَسَ مِنۡهُمۡ خِيفَةٗۖ قَالُواْ لَا تَخَفۡۖ وَبَشَّرُوهُ بِغُلَٰمٍ عَلِيمٖ
Akahisi Kuwaogopa katika Nafsi Yake Kuhusu Wao, Wakasema Usiogope Na Wakampa Bishara Kwa Kijana mwenye elimu
فَأَقۡبَلَتِ ٱمۡرَأَتُهُۥ فِي صَرَّةٖ فَصَكَّتۡ وَجۡهَهَا وَقَالَتۡ عَجُوزٌ عَقِيمٞ
Ndipo Mkewe akawaelekea na huku akisema Hali Ya kupiga Kelele Na Kujipigapiga Usoni (kwa kustaajabu) Na Akasema Kikongwe Tasa!!
قَالُواْ كَذَٰلِكِ قَالَ رَبُّكِۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡعَلِيمُ
Wakasema Hivyo Ndivyo Alivyosema Bwana Wako Hakika Yeye Ni Mwingi Wa Hekima Na Mjuzi
۞قَالَ فَمَا خَطۡبُكُمۡ أَيُّهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ
Akasema basi Lipi Jambo Lenu Enyi Mliotumwa
قَالُوٓاْ إِنَّآ أُرۡسِلۡنَآ إِلَىٰ قَوۡمٖ مُّجۡرِمِينَ
Wakasema, Sisi Tumetumwa Kwenda Kwa Watu Waovu
لِنُرۡسِلَ عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن طِينٖ
Ili tuwatupie Juu Yao Mawe Yatokanayo Na Udongo
مُّسَوَّمَةً عِندَ رَبِّكَ لِلۡمُسۡرِفِينَ
Yaliyo wekwa Alama kutoka Kwa Bwana Wako Kwa Waliyochupa Mipaka
تَنَزَّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَٱلرُّوحُ فِيهَا بِإِذۡنِ رَبِّهِم مِّن كُلِّ أَمۡرٖ
Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo