Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 125

وَإِذۡ جَعَلۡنَا ٱلۡبَيۡتَ مَثَابَةٗ لِّلنَّاسِ وَأَمۡنٗا وَٱتَّخِذُواْ مِن مَّقَامِ إِبۡرَٰهِـۧمَ مُصَلّٗىۖ وَعَهِدۡنَآ إِلَىٰٓ إِبۡرَٰهِـۧمَ وَإِسۡمَٰعِيلَ أَن طَهِّرَا بَيۡتِيَ لِلطَّآئِفِينَ وَٱلۡعَٰكِفِينَ وَٱلرُّكَّعِ ٱلسُّجُودِ

Na (kumbuka) tulipoifanya Kaaba sehemu ya watu kurejea na mahali pa amani, nafanyeni mahali aliposimama Ibrahimu mahali pakuswali. Na tukawaagiza Ibrahimu na Ismaili, (kuwa) itwaharisheni Nyumba yangu kwa ajili ya wanaofanya twawafu na wanaokaa itikafu na wanaorukuu na kusujudu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 126

وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِـۧمُ رَبِّ ٱجۡعَلۡ هَٰذَا بَلَدًا ءَامِنٗا وَٱرۡزُقۡ أَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ مَنۡ ءَامَنَ مِنۡهُم بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ قَالَ وَمَن كَفَرَ فَأُمَتِّعُهُۥ قَلِيلٗا ثُمَّ أَضۡطَرُّهُۥٓ إِلَىٰ عَذَابِ ٱلنَّارِۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na (kumbuka) aliposema Ibrahimu: “Ewe Mola wangu, ufanye mji huu (wa Makkah) uwe wa amani, na waruzuku watu wake katika matunda; yule aliye muamini Allah miongoni mwao na kuamini Siku ya Mwisho. (Allah) akasema: Na mwenye kukufuru nitamstarehesha kidogo kisha nitamswaga kwenda kwenye adhabu ya moto, na hatima mbaya mno ni hiyo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 127

وَإِذۡ يَرۡفَعُ إِبۡرَٰهِـۧمُ ٱلۡقَوَاعِدَ مِنَ ٱلۡبَيۡتِ وَإِسۡمَٰعِيلُ رَبَّنَا تَقَبَّلۡ مِنَّآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na (kumbuka wakati) Ibrahimu na Ismaili wanainua misingi ya Kaaba (wakisema): “Ewe Mola wetu, tukubalie. Hakika, wewe ndiye msikivu, mjuzi sana



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 128

رَبَّنَا وَٱجۡعَلۡنَا مُسۡلِمَيۡنِ لَكَ وَمِن ذُرِّيَّتِنَآ أُمَّةٗ مُّسۡلِمَةٗ لَّكَ وَأَرِنَا مَنَاسِكَنَا وَتُبۡ عَلَيۡنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

Ewe Mola wetu, tufanye sisi tuwe watiifu kwako, na katika kizazi chetu wawe umma mtiifu kwako. Na tuelekeze ibada zetu na pokea toba zetu. Hakika wewe tu ndiye mwingi wa kupokea toba mwingi wa rehema



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 129

رَبَّنَا وَٱبۡعَثۡ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡهُمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِكَ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَيُزَكِّيهِمۡۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Ewe Mola wetu, na wapelekee Mtume miongoni mwao, atakayewasomea Aya zako na kuwafundisha kitabu na hekima na kuwatakasa. Hakika wewe tu ndiye mwenye nguvu kubwa mwingi wa hekima



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 144

قَدۡ نَرَىٰ تَقَلُّبَ وَجۡهِكَ فِي ٱلسَّمَآءِۖ فَلَنُوَلِّيَنَّكَ قِبۡلَةٗ تَرۡضَىٰهَاۚ فَوَلِّ وَجۡهَكَ شَطۡرَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَحَيۡثُ مَا كُنتُمۡ فَوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ شَطۡرَهُۥۗ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ لَيَعۡلَمُونَ أَنَّهُ ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّهِمۡۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا يَعۡمَلُونَ

Tunaona ukigeuzageuza uso wako mbinguni. Hakika tunakuelekeza Kibla unachokiridhia, Basi elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtukufu[1]. Na popote muwapo elekezeni nyuso zenu upande huo. Na hakika wale ambao wamepewa kitabu wanajua kwamba hiyo ni haki kutoka kwa Mola wao. Na Allah hakuwa mwenye kughafilika na wanayotenda


1- - Msikiti Mtukufu wa Makka


Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 145

وَلَئِنۡ أَتَيۡتَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ بِكُلِّ ءَايَةٖ مَّا تَبِعُواْ قِبۡلَتَكَۚ وَمَآ أَنتَ بِتَابِعٖ قِبۡلَتَهُمۡۚ وَمَا بَعۡضُهُم بِتَابِعٖ قِبۡلَةَ بَعۡضٖۚ وَلَئِنِ ٱتَّبَعۡتَ أَهۡوَآءَهُم مِّنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَكَ مِنَ ٱلۡعِلۡمِ إِنَّكَ إِذٗا لَّمِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na kwa yakini kabisa kama ungewaletea kila aina ya hoja wale waliopewa kitabu, wasingefuata Kibla chako. Na wewe hutafuata Kibla chao. Na hata wao kwa wao hakuna mwenye kufuata Kibla cha mwingine. Na kama utafuata utashi wa nafsi zao baada ya kukufikia elimu, kwa yakini kabisa utakuwa miongoni mwa Madhalimu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 149

وَمِنۡ حَيۡثُ خَرَجۡتَ فَوَلِّ وَجۡهَكَ شَطۡرَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۖ وَإِنَّهُۥ لَلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Na popote utokapo enda elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtukufu. Na kwa hakika kabisa, hiyo ni haki kutoka kwa Mola wako. Na Allah hakuwa mwenye kughafilika na mnayoyatenda



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 150

وَمِنۡ حَيۡثُ خَرَجۡتَ فَوَلِّ وَجۡهَكَ شَطۡرَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَحَيۡثُ مَا كُنتُمۡ فَوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ شَطۡرَهُۥ لِئَلَّا يَكُونَ لِلنَّاسِ عَلَيۡكُمۡ حُجَّةٌ إِلَّا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡهُمۡ فَلَا تَخۡشَوۡهُمۡ وَٱخۡشَوۡنِي وَلِأُتِمَّ نِعۡمَتِي عَلَيۡكُمۡ وَلَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Na popote utokapoenda elekeza uso wako upande wa Msikiti Mtukufu. Na popote muwapo, elekezeni nyuso zenu upande huo, ili watu wasipate hoja dhidi yenu, isipokuwa madhalimu miongoni mwao. Kwa hiyo, hao msiwaogope, na niogopeni Mimi tu, na ili nitimize neema zangu kwenu, na ili mpate kuongoka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 158

۞إِنَّ ٱلصَّفَا وَٱلۡمَرۡوَةَ مِن شَعَآئِرِ ٱللَّهِۖ فَمَنۡ حَجَّ ٱلۡبَيۡتَ أَوِ ٱعۡتَمَرَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِ أَن يَطَّوَّفَ بِهِمَاۚ وَمَن تَطَوَّعَ خَيۡرٗا فَإِنَّ ٱللَّهَ شَاكِرٌ عَلِيمٌ

Hakika, Swafaa na Mar’wa ni katika alama za[1] Allah. Basi anayehiji (katika) Nyumba (tukufu) au kufanya Umra, si kosa kwake kuizunguka milima miwili hiyo. Na anayefanya wema, kwa yakini, Allah ni Mwenye kushukuru, Mjuzi wa kila jambo


1- - Dini ya Allah


Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 96

إِنَّ أَوَّلَ بَيۡتٖ وُضِعَ لِلنَّاسِ لَلَّذِي بِبَكَّةَ مُبَارَكٗا وَهُدٗى لِّلۡعَٰلَمِينَ

Kwa yakini kabisa, nyumba ya kwanza kabisa kuwekwa (ardhini) kwa ajili ya watu (ili kumuabudu Allah) ni ile (Alkaaba) iliyoko Makkah ikiwa imebarikiwa na ni uongofu kwa walimwengu wote



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 97

فِيهِ ءَايَٰتُۢ بَيِّنَٰتٞ مَّقَامُ إِبۡرَٰهِيمَۖ وَمَن دَخَلَهُۥ كَانَ ءَامِنٗاۗ وَلِلَّهِ عَلَى ٱلنَّاسِ حِجُّ ٱلۡبَيۡتِ مَنِ ٱسۡتَطَاعَ إِلَيۡهِ سَبِيلٗاۚ وَمَن كَفَرَ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَنِيٌّ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Humo kuna alama zilizo wazi; mahala aliposimama Ibrahimu. Na yeyote anayeingia humo anakuwa katika amani. Na ni wajibu kwa watu kuhiji katika nyumba (ya Al-kaaba), kwa mwenye kumudu gharama za kufika huko. Na atakayepinga, basi (ajue kuwa) Allah si muhitaji kwa walimwengu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 2

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تُحِلُّواْ شَعَـٰٓئِرَ ٱللَّهِ وَلَا ٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَلَا ٱلۡهَدۡيَ وَلَا ٱلۡقَلَـٰٓئِدَ وَلَآ ءَآمِّينَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ يَبۡتَغُونَ فَضۡلٗا مِّن رَّبِّهِمۡ وَرِضۡوَٰنٗاۚ وَإِذَا حَلَلۡتُمۡ فَٱصۡطَادُواْۚ وَلَا يَجۡرِمَنَّكُمۡ شَنَـَٔانُ قَوۡمٍ أَن صَدُّوكُمۡ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ أَن تَعۡتَدُواْۘ وَتَعَاوَنُواْ عَلَى ٱلۡبِرِّ وَٱلتَّقۡوَىٰۖ وَلَا تَعَاوَنُواْ عَلَى ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَۖ إِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Enyi mlioamini, msizivunjie heshima alama za (dini) ya Allah[1] wala Miezi Mitukufu[2] wala Hadiy[3] wala vigwe[4], wala wakusudiao Nyumba Takatifu[5] wakitafuta fadhila na radhi za Mola wao. Na mkishatoka (katika Ibada ya Hija au Umrah) basi windeni (mkitaka kufanya hivyo). Na wala kule kuwachukia watu kwa kuwa walikuzuieni kufika Msikiti Mtukufu kusikupelekeeni kuwafanyia uadui (wa kuwaua na mfano wa hilo). Na saidianeni katika wema na ucha Mungu, na msisaidiane katika dhambi na uadui. Na mcheni Allah. Hakika, Allah ni Mkali sana wa kuadhibu


1- - Alama za dini ya Allah ni zile ibada kubwa kama Hija, Umra, Swala, Funga n.k.


2- - Miezi Mitukufu ni minne: Dhul-qaada, Dhulhija, Muharram na Rajab.


3- - Hadiyu ni wanyama wanaopelekwa Makka kwa kuchinjwa katika ibada ya Hija.


4- - Vigwe ni kamba za utambulisho anayofungwa mnyama shingoni ili kumtambulisha kuwa anapelekwa Makkah kwa kuchinjwa katika ibada ya Hija.


5- - Hawa ni wale Waislamu wanaokwenda Makka kwa makusudi ya kufanya ibada ya Hija au Umra.


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 97

۞جَعَلَ ٱللَّهُ ٱلۡكَعۡبَةَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ قِيَٰمٗا لِّلنَّاسِ وَٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَٱلۡهَدۡيَ وَٱلۡقَلَـٰٓئِدَۚ ذَٰلِكَ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَأَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Allah ameifanya Al-Kaaba, Nyumba Tukufu kuwa tegemeo la watu, na kadhalika (ameifanya) Miezi Mitukufu (tegemeo kwa kusitishwa vita) na wanyama wa hadiyi (dhabihu) waliovikwa koja. (Allah amefanya) Hayo ili mjue kwamba Allah anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini, na kwamba Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 34

وَمَا لَهُمۡ أَلَّا يُعَذِّبَهُمُ ٱللَّهُ وَهُمۡ يَصُدُّونَ عَنِ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَمَا كَانُوٓاْ أَوۡلِيَآءَهُۥٓۚ إِنۡ أَوۡلِيَآؤُهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُتَّقُونَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na (Washirikina) wana jambo gani (jema) hata Allah asiwaadhibu (asiwaangamize), na ilhali wanauwekea vikwazo Msikiti Mtukufu (kwa kuwazuia watu kwenda kutekeleza ibada) na wala wao hawakuwa waangalizi wake? Hawakuwa waangalizi wake ila wachaMungu tu, lakini wengi wao hawajui (kuwa hawana haki hiyo ya uangalizi wa Msikiti Mtukufu)



Capítulo: AN-FAL 

Verso : 35

وَمَا كَانَ صَلَاتُهُمۡ عِندَ ٱلۡبَيۡتِ إِلَّا مُكَآءٗ وَتَصۡدِيَةٗۚ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ

Na haikuwa (Swala) ibada yao kwenye Nyumba (Al Kaaba) ila ni kupiga miruzi na makofi tu. Basi (enyi Washirikina) onjeni adhabu (ya duniani kwa kupigwa kwenye vita vya Badri) (na adhabu ya huko Akhera inawangojeni) kwa vile mlivyokuwa mnakufuru



Capítulo: IBRAHIM 

Verso : 37

رَّبَّنَآ إِنِّيٓ أَسۡكَنتُ مِن ذُرِّيَّتِي بِوَادٍ غَيۡرِ ذِي زَرۡعٍ عِندَ بَيۡتِكَ ٱلۡمُحَرَّمِ رَبَّنَا لِيُقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ فَٱجۡعَلۡ أَفۡـِٔدَةٗ مِّنَ ٱلنَّاسِ تَهۡوِيٓ إِلَيۡهِمۡ وَٱرۡزُقۡهُم مِّنَ ٱلثَّمَرَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَشۡكُرُونَ

Mola wetu Mlezi, hakika mimi nimewaweka baadhi ya dhuriya zangu (Ismaili na mama yake) kwenye bonde lisilokuwa na mimea, kwenye Nyumba yako Takatifu, ewe Mola wetu Mlezi, ili wasimamishe Swala. Basi zijaalie nyoyo za watu zielekee kwao, na waruzuku kila aina ya matunda, ili wapate kushukuru



Capítulo: AL-HAJJ 

Verso : 26

وَإِذۡ بَوَّأۡنَا لِإِبۡرَٰهِيمَ مَكَانَ ٱلۡبَيۡتِ أَن لَّا تُشۡرِكۡ بِي شَيۡـٔٗا وَطَهِّرۡ بَيۡتِيَ لِلطَّآئِفِينَ وَٱلۡقَآئِمِينَ وَٱلرُّكَّعِ ٱلسُّجُودِ

Na pale tulipomweka Ibrahim pahala penye ile Nyumba tukam-wambia: Usinishirikishe na chochote; na isafishe Nyumba yangu kwa ajili ya wanao izunguka kwa kutufu, na wanao kaa hapo kwa ibada, na wanao rukuu, na wanao sujudu



Capítulo: AL-HAJJ 

Verso : 29

ثُمَّ لۡيَقۡضُواْ تَفَثَهُمۡ وَلۡيُوفُواْ نُذُورَهُمۡ وَلۡيَطَّوَّفُواْ بِٱلۡبَيۡتِ ٱلۡعَتِيقِ

Kisha wajisafishe taka zao, na waondoe nadhiri zao, na waizunguke Nyumba ya Kale



Capítulo: AL-HAJJ 

Verso : 33

لَكُمۡ فِيهَا مَنَٰفِعُ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى ثُمَّ مَحِلُّهَآ إِلَى ٱلۡبَيۡتِ ٱلۡعَتِيقِ

Katika hao nyinyi mna manufaa mpaka muda maalumu. Kisha pahala pa kuchinjiwa kwake ni kwenye Nyumba ya Kale



Capítulo: AL-QURAISH 

Verso : 3

فَلۡيَعۡبُدُواْ رَبَّ هَٰذَا ٱلۡبَيۡتِ

Kwasababu ya hayo, wamuabudu Mola Mlezi wa Nyumba hii (Tukufu ya Makka)