Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 1

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ ٱلۡغَٰشِيَةِ

Je, imekufikia habari ya msiba wa kufudikiza (ugongao moyo)?



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 2

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٍ خَٰشِعَةٌ

Siku hiyo nyuso zitainama,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 3

عَامِلَةٞ نَّاصِبَةٞ

Zikifanya kazi, nazo taabani



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 4

تَصۡلَىٰ نَارًا حَامِيَةٗ

Ziingie katika Moto unao waka



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 5

تُسۡقَىٰ مِنۡ عَيۡنٍ ءَانِيَةٖ

Zikinyweshwa kutoka chemchem inayo chemka



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 6

لَّيۡسَ لَهُمۡ طَعَامٌ إِلَّا مِن ضَرِيعٖ

Hawatakuwa na chakula isipo kuwa kichungu chenye miba



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 7

لَّا يُسۡمِنُ وَلَا يُغۡنِي مِن جُوعٖ

Hakinenepeshi wala hakiondoi njaa



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 8

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاعِمَةٞ

Siku hiyo nyuso nyengine zitakuwa kunjufu



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 9

لِّسَعۡيِهَا رَاضِيَةٞ

Zitakuwa radhi kwa juhudi yao,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 10

فِي جَنَّةٍ عَالِيَةٖ

Katika Bustani ya juu



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 11

لَّا تَسۡمَعُ فِيهَا لَٰغِيَةٗ

Hawatasikia humo upuuzi. Humo imo chemchem inayo miminika



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 12

فِيهَا عَيۡنٞ جَارِيَةٞ

Humo imo chemchem inayo miminika



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 13

فِيهَا سُرُرٞ مَّرۡفُوعَةٞ

Humo vimo viti vilivyo nyanyuliwa,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 14

وَأَكۡوَابٞ مَّوۡضُوعَةٞ

Na bilauri zilizo pangwa,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 15

وَنَمَارِقُ مَصۡفُوفَةٞ

Na matakia (yakiwa) safu safu,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 16

وَزَرَابِيُّ مَبۡثُوثَةٌ

Na mazulia yaliyo tandikwa



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 17

أَفَلَا يَنظُرُونَ إِلَى ٱلۡإِبِلِ كَيۡفَ خُلِقَتۡ

Je! Hawamtazami ngamia jinsi alivyo umbwa?



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 18

وَإِلَى ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ رُفِعَتۡ

Na mbingu jinsi ilivyo inuliwa?



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 19

وَإِلَى ٱلۡجِبَالِ كَيۡفَ نُصِبَتۡ

Na milima jinsi ilivyo thibitishwa (simamishwa)?



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 20

وَإِلَى ٱلۡأَرۡضِ كَيۡفَ سُطِحَتۡ

Na ardhi jinsi ilivyo tandazwa?



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 21

فَذَكِّرۡ إِنَّمَآ أَنتَ مُذَكِّرٞ

Basi kumbusha! Hakika wewe ni Mkumbushaji



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 22

لَّسۡتَ عَلَيۡهِم بِمُصَيۡطِرٍ

Wewe si mwenye kuwatawalia



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 23

إِلَّا مَن تَوَلَّىٰ وَكَفَرَ

Lakini anaye rudi nyuma na kukufuru,



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 24

فَيُعَذِّبُهُ ٱللَّهُ ٱلۡعَذَابَ ٱلۡأَكۡبَرَ

Basi Allah Atamuadhibu adhabu kubwa kabisa



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 25

إِنَّ إِلَيۡنَآ إِيَابَهُمۡ

Hakika ni kwetu Sisi ndio marejeo yao



Sure:  AL-GHAASHIYAH 

Vers : 26

ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا حِسَابَهُم

Kisha hakika ni juu yetu Sisi hesabu yao!