Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 1

إِذَا ٱلشَّمۡسُ كُوِّرَتۡ

Jua litakapokunjwa kunjwa (na kupotea mwanga wake)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 2

وَإِذَا ٱلنُّجُومُ ٱنكَدَرَتۡ

Na nyota zitikapotiwa giza (zitakapozimwa nuru yake)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 3

وَإِذَا ٱلۡجِبَالُ سُيِّرَتۡ

Na milima itakapoendeshwa (itakapondolewa)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 4

وَإِذَا ٱلۡعِشَارُ عُطِّلَتۡ

Na ngamia wenye mimba pevu watakapotelekezwa



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 5

وَإِذَا ٱلۡوُحُوشُ حُشِرَتۡ

Na wanyama wa mwituni watakapokusanywa



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 6

وَإِذَا ٱلۡبِحَارُ سُجِّرَتۡ

Na bahari zitakapowashwa moto



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 7

وَإِذَا ٱلنُّفُوسُ زُوِّجَتۡ

Na roho zitakapounganishwa na viwiliwili vyao



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 8

وَإِذَا ٱلۡمَوۡءُۥدَةُ سُئِلَتۡ

Na mtoto wa kike aliyezikwa akiwa hai atakapoulizwa



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 9

بِأَيِّ ذَنۢبٖ قُتِلَتۡ

Ameuawa kosa gani?



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 10

وَإِذَا ٱلصُّحُفُ نُشِرَتۡ

Na sahifa (kurasa) za kurekodi (matendo ya waja) zitakapo kunjuliwa, [wakati wa kuhesabiwa watu]



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 11

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ كُشِطَتۡ

Na mbingu itapo ondoshwa pahala pake



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 12

وَإِذَا ٱلۡجَحِيمُ سُعِّرَتۡ

Na Jahannamu itakapo chochewa



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 13

وَإِذَا ٱلۡجَنَّةُ أُزۡلِفَتۡ

Na Pepo ikasogezwa karibu



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 14

عَلِمَتۡ نَفۡسٞ مَّآ أَحۡضَرَتۡ

Kila nafsi itajua ilicho kihudhurisha



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 15

فَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلۡخُنَّسِ

Basi Naapa kwa sayari zinapo rejea nyuma, zinazotoweka (mchana na zinadhihirika usiku)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 16

ٱلۡجَوَارِ ٱلۡكُنَّسِ

Zinazotembea na kujificha



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 17

وَٱلَّيۡلِ إِذَا عَسۡعَسَ

Na naapa kwa usiku unapo pungua giza lake



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 18

وَٱلصُّبۡحِ إِذَا تَنَفَّسَ

Na Naapa kwa asubuhi inapo pambazuka



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 19

إِنَّهُۥ لَقَوۡلُ رَسُولٖ كَرِيمٖ

Hakika hii (Qurani) bila shaka ni kauli (ameifikisha) Mjumbe mtukufu (Jibrili)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 20

ذِي قُوَّةٍ عِندَ ذِي ٱلۡعَرۡشِ مَكِينٖ

Mwenye nguvu na cheo kitukufu kwa (Allah) Anayemiliki ‘Arsh. [Kiti cha Enzi]



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 21

مُّطَاعٖ ثَمَّ أَمِينٖ

Anayetiiwa (na Malaika), mwaminifu huko (mbinguni)



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 22

وَمَا صَاحِبُكُم بِمَجۡنُونٖ

Na wala huyu mwenzenu hana wazimu



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 23

وَلَقَدۡ رَءَاهُ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡمُبِينِ

Na hakika yeye alimwona [Jibrili] kwenye upeo wa macho ulio safi



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 24

وَمَا هُوَ عَلَى ٱلۡغَيۡبِ بِضَنِينٖ

Wala yeye si bakhili kwa [kuelezea mambo ya] ghaibu



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 25

وَمَا هُوَ بِقَوۡلِ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٖ

Na hii (Qurani) si kauli ya shetani aliye fukuzwa kutoka kwenye rehema za Allah



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 26

فَأَيۡنَ تَذۡهَبُونَ

Basi mnakwenda wapi?



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 27

إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرٞ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Hii (Qurani) haikuwa isipokuwa ni ukumbusho kwa walimwengu wote



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 28

لِمَن شَآءَ مِنكُمۡ أَن يَسۡتَقِيمَ

Kwa yule anaye taka miongoni mwenu kwenda sawa



Sure: ATTAK-WIIR 

Vers : 29

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Wala nyinyi hamtataka isipo kuwa atake Allah Mola wa Walimwengu wote