Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 1

وَٱلنَّـٰزِعَٰتِ غَرۡقٗا

Nina apa kwa [Malaika] wanaong’oa (roho) kwa nguvu



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 2

وَٱلنَّـٰشِطَٰتِ نَشۡطٗا

Na (kwa Malaika) wanaotoa (roho) kwa upole



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 3

وَٱلسَّـٰبِحَٰتِ سَبۡحٗا

Na ( kwa Malaika) wanaoogelea sana (katika anga kwa kupanda na kushuka wakitekeleza majukumu waliyopewa na Allah)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 4

فَٱلسَّـٰبِقَٰتِ سَبۡقٗا

Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuongoza (katika kushidana wakati wa kutimiza wajibu wao)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 5

فَٱلۡمُدَبِّرَٰتِ أَمۡرٗا

Kisha (Nina apa kwa Malaika) wenye kuendesha kila jambo (kwa maagizo ya Allah)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 6

يَوۡمَ تَرۡجُفُ ٱلرَّاجِفَةُ

Siku kitakapotetemeka cha kutetemeka



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 7

تَتۡبَعُهَا ٱلرَّادِفَةُ

Na utafuatia mpulizo (mwingine wa pili wa baragumu)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 8

قُلُوبٞ يَوۡمَئِذٖ وَاجِفَةٌ

Siku hiyo nyoyo zitapiga piga (mapigo ya haraka haraka kwa hofu)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 9

أَبۡصَٰرُهَا خَٰشِعَةٞ

Macho yake yatainama chini



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 10

يَقُولُونَ أَءِنَّا لَمَرۡدُودُونَ فِي ٱلۡحَافِرَةِ

Wanasema: Je, hivi sisi kweli tutarudishwa kwenye hali ya kwanza?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 11

أَءِذَا كُنَّا عِظَٰمٗا نَّخِرَةٗ

Je, hata tukiwa ni mifupa iliyosagika na kuoza?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 12

قَالُواْ تِلۡكَ إِذٗا كَرَّةٌ خَاسِرَةٞ

Wanasema: Basi marejeo hayo, ni marejeo yenye hasara!



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 13

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ

Basi hakika huo ni ukelele mmoja tu



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 14

فَإِذَا هُم بِٱلسَّاهِرَةِ

Tahamaki hao watahudhurishwa kwenye ardhi ya mkusanyiko, (wakiwa macho baada ya kufa)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 15

هَلۡ أَتَىٰكَ حَدِيثُ مُوسَىٰٓ

Je, imekufikia habarii ya Mussa?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 16

إِذۡ نَادَىٰهُ رَبُّهُۥ بِٱلۡوَادِ ٱلۡمُقَدَّسِ طُوًى

Mola wake alipo mwita katika bonde takatifu la Tuwaa, akamwambia;



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 17

ٱذۡهَبۡ إِلَىٰ فِرۡعَوۡنَ إِنَّهُۥ طَغَىٰ

Nenda kwa Firauna, hakika yeye amepindukia mipaka



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 18

فَقُلۡ هَل لَّكَ إِلَىٰٓ أَن تَزَكَّىٰ

Umwambie: Je, unataka utakasike?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 19

وَأَهۡدِيَكَ إِلَىٰ رَبِّكَ فَتَخۡشَىٰ

Na nikuongoze kwa Mola wako umuogope?



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 20

فَأَرَىٰهُ ٱلۡأٓيَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰ

Basi akamuonyesha Ishara (muujiza) mkubwa kabisa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 21

فَكَذَّبَ وَعَصَىٰ

Lakini aliikadhibisha na akaasi



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 22

ثُمَّ أَدۡبَرَ يَسۡعَىٰ

Kisha akageuka nyuma na kufanya juhudi, (ya kukanusha)



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 23

فَحَشَرَ فَنَادَىٰ

Akakusanya watu akatangaza



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 24

فَقَالَ أَنَا۠ رَبُّكُمُ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Akasema: Mimi ndiye Mola wenu Mkuu kabisa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 25

فَأَخَذَهُ ٱللَّهُ نَكَالَ ٱلۡأٓخِرَةِ وَٱلۡأُولَىٰٓ

Basi hapo Allah akamshika na kumuadhibu kwa adhabu ya mwisho na mwanzo.[1]


1- - Allah akampa adhabu kwa kauli yake ya mwisho, nayo ni vile kusema: “Mimi ndiye Mola wenu Mlezi aliye mkubwa kabisa. Na akampa adhabu kwa kauli yake ya mwanzo, nayo ni kumkadhibisha Musa”.


Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 26

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَعِبۡرَةٗ لِّمَن يَخۡشَىٰٓ

Hakika katika hayo bila shaka kuna funzo kwa yule anayeogopa



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 27

ءَأَنتُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَمِ ٱلسَّمَآءُۚ بَنَىٰهَا

Je! Ni vigumu zaidi kukuumbeni nyinyi au mbingu? Yeye ndiye aliye ijenga!



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 28

رَفَعَ سَمۡكَهَا فَسَوَّىٰهَا

Akainua kimo chake, na akaiten-geneza vizuri



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 29

وَأَغۡطَشَ لَيۡلَهَا وَأَخۡرَجَ ضُحَىٰهَا

Na akautia giza usiku wake, na akautokeza mchana wake



Sure: ANNAAZIAAT 

Vers : 30

وَٱلۡأَرۡضَ بَعۡدَ ذَٰلِكَ دَحَىٰهَآ

Na ardhi baada ya hayo Akai-tandaza