Sure: ANNABAI 

Vers : 1

عَمَّ يَتَسَآءَلُونَ

Wanaulizana nini?



Sure: ANNABAI 

Vers : 2

عَنِ ٱلنَّبَإِ ٱلۡعَظِيمِ

Ni kuhusu habari kubwa sana



Sure: ANNABAI 

Vers : 3

ٱلَّذِي هُمۡ فِيهِ مُخۡتَلِفُونَ

Ambayo wao wanatofautiana ndani yake



Sure: ANNABAI 

Vers : 4

كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

Sihivyo! Karibu watakuja kujua



Sure: ANNABAI 

Vers : 5

ثُمَّ كَلَّا سَيَعۡلَمُونَ

Tena si hivyo! Karibu watakuja kujua



Sure: ANNABAI 

Vers : 6

أَلَمۡ نَجۡعَلِ ٱلۡأَرۡضَ مِهَٰدٗا

Je, kwani hatukuifanya ardhi (kama) tandiko?



Sure: ANNABAI 

Vers : 7

وَٱلۡجِبَالَ أَوۡتَادٗا

Na milima kuwa (kama) vigingi?



Sure: ANNABAI 

Vers : 8

وَخَلَقۡنَٰكُمۡ أَزۡوَٰجٗا

Na Tukakuumbeni kwa jozi; (wanaume na wanawake)?



Sure: ANNABAI 

Vers : 9

وَجَعَلۡنَا نَوۡمَكُمۡ سُبَاتٗا

Na tukafanya kulala kwenu ni mapumziko?



Sure: ANNABAI 

Vers : 10

وَجَعَلۡنَا ٱلَّيۡلَ لِبَاسٗا

Na tukaufanya usiku (ni kama) nguo (ya kukufunikeni)?



Sure: ANNABAI 

Vers : 11

وَجَعَلۡنَا ٱلنَّهَارَ مَعَاشٗا

Na tukaufanya mchana ni wa kuchumia [kutafuta] maisha?



Sure: ANNABAI 

Vers : 12

وَبَنَيۡنَا فَوۡقَكُمۡ سَبۡعٗا شِدَادٗا

Na Tukajenga juu yenu (mbingu) saba imara?



Sure: ANNABAI 

Vers : 13

وَجَعَلۡنَا سِرَاجٗا وَهَّاجٗا

Na tukaifanya taa yenye mwanga na joto



Sure: ANNABAI 

Vers : 14

وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلۡمُعۡصِرَٰتِ مَآءٗ ثَجَّاجٗا

Na tukateremsha maji yanayo anguka kwa kasi kutoka mawinguni



Sure: ANNABAI 

Vers : 15

لِّنُخۡرِجَ بِهِۦ حَبّٗا وَنَبَاتٗا

Ili tutoe [tuoteshe] kwayo nafaka na mimea



Sure: ANNABAI 

Vers : 16

وَجَنَّـٰتٍ أَلۡفَافًا

Na mabustani yenye miti iliyo kamatana



Sure: ANNABAI 

Vers : 17

إِنَّ يَوۡمَ ٱلۡفَصۡلِ كَانَ مِيقَٰتٗا

Hakika siku ya uamuzi,[hukumu] imewekewa wakati wake



Sure: ANNABAI 

Vers : 18

يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِ فَتَأۡتُونَ أَفۡوَاجٗا

Siku litakapopulizwa baragumu, nanyi mtakuja makundi kwa makundi



Sure: ANNABAI 

Vers : 19

وَفُتِحَتِ ٱلسَّمَآءُ فَكَانَتۡ أَبۡوَٰبٗا

Na mbingu zitafunguliwa, ziwe kama milango



Sure: ANNABAI 

Vers : 20

وَسُيِّرَتِ ٱلۡجِبَالُ فَكَانَتۡ سَرَابًا

Na milima itaondolewa na itakuwa kama sarabi, [mangati]



Sure: ANNABAI 

Vers : 21

إِنَّ جَهَنَّمَ كَانَتۡ مِرۡصَادٗا

Hakika moto wa Jahannamu utakuwa ni wenye kuvizia



Sure: ANNABAI 

Vers : 22

لِّلطَّـٰغِينَ مَـَٔابٗا

Kwa walioruka mipaka kwa kuasi ndio makaazi yao



Sure: ANNABAI 

Vers : 23

لَّـٰبِثِينَ فِيهَآ أَحۡقَابٗا

Watabaki humo karne baada ya karne



Sure: ANNABAI 

Vers : 24

لَّا يَذُوقُونَ فِيهَا بَرۡدٗا وَلَا شَرَابًا

Hawatoonja humo cha baridi na wala kinywaji



Sure: ANNABAI 

Vers : 25

إِلَّا حَمِيمٗا وَغَسَّاقٗا

Ila maji yamoto sana na usaha,



Sure: ANNABAI 

Vers : 26

جَزَآءٗ وِفَاقًا

Ndio malipo yao muwafaka



Sure: ANNABAI 

Vers : 27

إِنَّهُمۡ كَانُواْ لَا يَرۡجُونَ حِسَابٗا

Hakika wao walikuwa hawataraji kuhesabiwa



Sure: ANNABAI 

Vers : 28

وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كِذَّابٗا

Na wakikanusha Aya zetu kwa sana



Sure: ANNABAI 

Vers : 29

وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ كِتَٰبٗا

Na kila kitu Sisi tumekidhibiti kwa kukiandika



Sure: ANNABAI 

Vers : 30

فَذُوقُواْ فَلَن نَّزِيدَكُمۡ إِلَّا عَذَابًا

Basi onjeni! Nasi hatutakuzidishieni ila adhabu!