Sure: AL-INSAAN

Vers : 1

هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا

Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 2

إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا

Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona



Sure: AL-INSAAN

Vers : 3

إِنَّا هَدَيۡنَٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرٗا وَإِمَّا كَفُورًا

Hakika, sisi tumemuongoza (tumempa mwongozo unaofikishwa na Mitume); ama awe mwenye kushukuru au mwenye kukufuru



Sure: AL-INSAAN

Vers : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



Sure: AL-INSAAN

Vers : 5

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ يَشۡرَبُونَ مِن كَأۡسٖ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا

Hakika, watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri



Sure: AL-INSAAN

Vers : 6

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفۡجِيرٗا

Ni chemchem watakayoinywa waja wa Allah, wakiifanya imiminike kwa wingi



Sure: AL-INSAAN

Vers : 7

يُوفُونَ بِٱلنَّذۡرِ وَيَخَافُونَ يَوۡمٗا كَانَ شَرُّهُۥ مُسۡتَطِيرٗا

Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea sana



Sure: AL-INSAAN

Vers : 8

وَيُطۡعِمُونَ ٱلطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ مِسۡكِينٗا وَيَتِيمٗا وَأَسِيرًا

Na wanalisha chakula, pamoja na kukipenda kwake, (wanawalisha) masikini na mayatima na mateka



Sure: AL-INSAAN

Vers : 9

إِنَّمَا نُطۡعِمُكُمۡ لِوَجۡهِ ٱللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمۡ جَزَآءٗ وَلَا شُكُورًا

Hakika sisi tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi za Allah. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani



Sure: AL-INSAAN

Vers : 10

إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوۡمًا عَبُوسٗا قَمۡطَرِيرٗا

Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu



Sure: AL-INSAAN

Vers : 11

فَوَقَىٰهُمُ ٱللَّهُ شَرَّ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمِ وَلَقَّىٰهُمۡ نَضۡرَةٗ وَسُرُورٗا

Basi Allah Atawakinga na shari ya siku hiyo, na Atawapa nuru na kuwakutanisha na uchangamfu na furaha



Sure: AL-INSAAN

Vers : 12

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُواْ جَنَّةٗ وَحَرِيرٗا

Na Atawalipa kwasababu ya kusubiri kwao, Pepo na nguo za hariri



Sure: AL-INSAAN

Vers : 13

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِۖ لَا يَرَوۡنَ فِيهَا شَمۡسٗا وَلَا زَمۡهَرِيرٗا

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona (hawatahisi) humo jua kali wala baridi kali.[1]


1- - Aya ni dalili kuwa Akhera kuna adhabu ya Baridi. Kama alivyopokea Imamu Bukhariy na Muslim- kutoka kwa Abuu Hurairah (Allah amuwiye radhh) amesema; amesema Mtume wa Allah (Rehema na amani ziwe juu yake):-


Sure: AL-INSAAN

Vers : 14

وَدَانِيَةً عَلَيۡهِمۡ ظِلَٰلُهَا وَذُلِّلَتۡ قُطُوفُهَا تَذۡلِيلٗا

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning’inia mpaka chini



Sure: AL-INSAAN

Vers : 15

وَيُطَافُ عَلَيۡهِم بِـَٔانِيَةٖ مِّن فِضَّةٖ وَأَكۡوَابٖ كَانَتۡ قَوَارِيرَا۠

Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na bilauri zilokuwa za vigae



Sure: AL-INSAAN

Vers : 16

قَوَارِيرَاْ مِن فِضَّةٖ قَدَّرُوهَا تَقۡدِيرٗا

Vigae safi kutokana na fedha wamezipima kwa kipimo



Sure: AL-INSAAN

Vers : 17

وَيُسۡقَوۡنَ فِيهَا كَأۡسٗا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi



Sure: AL-INSAAN

Vers : 18

عَيۡنٗا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلۡسَبِيلٗا

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil



Sure: AL-INSAAN

Vers : 19

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيۡتَهُمۡ حَسِبۡتَهُمۡ لُؤۡلُؤٗا مَّنثُورٗا

Na watawazungukia wavulana wasio pevuka wakiwatumikia, ukiwaona utadhani ni lulu zilizo tawanywa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 20

وَإِذَا رَأَيۡتَ ثَمَّ رَأَيۡتَ نَعِيمٗا وَمُلۡكٗا كَبِيرًا

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 21

عَٰلِيَهُمۡ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضۡرٞ وَإِسۡتَبۡرَقٞۖ وَحُلُّوٓاْ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٖ وَسَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ شَرَابٗا طَهُورًا

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Sure: AL-INSAAN

Vers : 23

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ تَنزِيلٗا

Hakika Sisi tumekuteremshia Qur’ani kidogo kidogo (hatua kwa hatua)



Sure: AL-INSAAN

Vers : 24

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعۡ مِنۡهُمۡ ءَاثِمًا أَوۡ كَفُورٗا

Basi ngojea hukumu ya Mola wako wala usimtii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kukufuru



Sure: AL-INSAAN

Vers : 25

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلٗا

Na litaje jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni



Sure: AL-INSAAN

Vers : 26

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَٱسۡجُدۡ لَهُۥ وَسَبِّحۡهُ لَيۡلٗا طَوِيلًا

Na usiku msujudie Yeye, na umtakase, (usali kwaajili yake) usiku, wakati mrefu



Sure: AL-INSAAN

Vers : 27

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ يُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَآءَهُمۡ يَوۡمٗا ثَقِيلٗا

Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito, (ya Kiyama)



Sure: AL-INSAAN

Vers : 28

نَّحۡنُ خَلَقۡنَٰهُمۡ وَشَدَدۡنَآ أَسۡرَهُمۡۖ وَإِذَا شِئۡنَا بَدَّلۡنَآ أَمۡثَٰلَهُمۡ تَبۡدِيلًا

Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao



Sure: AL-INSAAN

Vers : 29

إِنَّ هَٰذِهِۦ تَذۡكِرَةٞۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلٗا

Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake



Sure: AL-INSAAN

Vers : 30

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Wala hamuwezi kutaka ila atakapo Allah. Hakika Allah ni Mwenye elimu, Mwenye hekima