Sure: AL-QALAM 

Vers : 1

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Nina apa kwa kalamu na yale wayoyaandika



Sure: AL-QALAM 

Vers : 2

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

(Kwamba) Wewe (Muhammad) kwa neema ya Mola wako Mlezi (aliyokupa) sio mwendawazimu



Sure: AL-QALAM 

Vers : 3

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo (makubwa) yasiyo katika



Sure: AL-QALAM 

Vers : 4

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe uko juu ya tabia njema sana



Sure: AL-QALAM 

Vers : 5

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Basi hivi karibuni utaona, na wao wataona



Sure: AL-QALAM 

Vers : 6

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

(Kwamba) Ni nani mwenye kichaa miongoni mwenu



Sure: AL-QALAM 

Vers : 7

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika, Mola wako Mlezi ndiye amjuae zaidi aliyepotea njia yake, ndiye awajuae zaidi walioongoka



Sure: AL-QALAM 

Vers : 8

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwatii wanao kadhibisha



Sure: AL-QALAM 

Vers : 9

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Wangependa uwe laini (ulegeze msimamo wako), nao wawe laini (walegeze msimamo wao na wakufuate)



Sure: AL-QALAM 

Vers : 10

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimtii kila mwapaji sana, aliye dhalili,



Sure: AL-QALAM 

Vers : 11

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mwingi wa kusengenya, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha



Sure: AL-QALAM 

Vers : 12

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwingi wa kuzuia ya kheri, aliyependukia katika kuwadhulumu (Watu) mwingi wa kutenda dhambi



Sure: AL-QALAM 

Vers : 13

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkavu, na juu ya hayo ni mwana haramu (kujipachika tu kabila)



Sure: AL-QALAM 

Vers : 14

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Kwakuwa tu ni mwenye kumiliki mali na watoto?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 15

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!



Sure: AL-QALAM 

Vers : 16

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Karibuni tutamtia kovu juu ya pua



Sure: AL-QALAM 

Vers : 17

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika sisi Tumewajaribu (Maquraysh) kama Tulivyowajaribu watu wa shamba pale walipo apa kuwa bila shaka watayavuna (matunda yake) watakapo pambaukiwa asubuhi



Sure: AL-QALAM 

Vers : 18

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Na wala hawakusema In-Shaa Allaah (Allah akipenda)!



Sure: AL-QALAM 

Vers : 19

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi (shamba lao) likazungukwa na (moto) kutoka kwa mola wako ilihali wao wamelala



Sure: AL-QALAM 

Vers : 20

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama lilovunwa (ilion-g’olewa mimea yake)



Sure: AL-QALAM 

Vers : 21

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Wakaitana, pale walipopam-baukiwa asubuhi



Sure: AL-QALAM 

Vers : 22

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Kwamba nendeni asubuhi mapema shambani mwenu, mkiwa mnataka kuvuna



Sure: AL-QALAM 

Vers : 23

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Wakatoka na huku wanakwenda kimya kimya wakinong’onezana



Sure: AL-QALAM 

Vers : 24

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Wakisema kwamba:: leo Maskini asiingie humo mwenu kinyume cha utashi wenu



Sure: AL-QALAM 

Vers : 25

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Wakatoka asubuhi mapema kwa kusudio la nguvu, wakidhani wana uwezo (wa kuwazuia maskini)



Sure: AL-QALAM 

Vers : 26

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipoliona (shamba lao) wakasema: Hakika sisi bila shaka Tumepotea



Sure: AL-QALAM 

Vers : 27

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

(Walivyo tanabahi!): wakasema Bali sisi tumenyimwa (mavuno yake)!



Sure: AL-QALAM 

Vers : 28

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Allah (kuiacha nia yenu mbaya)?



Sure: AL-QALAM 

Vers : 29

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: utukufu ni wa mola wetu, hakika tulikuwa wenye kudhulumu



Sure: AL-QALAM 

Vers : 30

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana