Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 1

يُسَبِّحُ لِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۖ لَهُ ٱلۡمُلۡكُ وَلَهُ ٱلۡحَمۡدُۖ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Vinamsabihi Allah (viumbe) vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi. Ni wake yeye tu ufalme na ni zake yeye tu sifa njema. Na Yeye ni Mwenye uwezawa kila kitu



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 2

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَكُمۡ فَمِنكُمۡ كَافِرٞ وَمِنكُم مُّؤۡمِنٞۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٌ

Yeye ndiye ambaye amekuumbeni. Basi miongoni mwenu yupo aliye kafiri na miongoni mwenu yupo aliye Muumini. Na Allah ni Mwenye kuyaona vyema myatendayo



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 3

خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّ وَصَوَّرَكُمۡ فَأَحۡسَنَ صُوَرَكُمۡۖ وَإِلَيۡهِ ٱلۡمَصِيرُ

Ameumba mbingu na ardhi kwa haki, na amekuumbeni katika sura, kisha akazifanya nzuri sura zenu, na marejeo ni kwake



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 4

يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَيَعۡلَمُ مَا تُسِرُّونَ وَمَا تُعۡلِنُونَۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Anajua yale yaliyomo mbinguni na ardhini, na anayajua yale mnayofanya kwa siri na mnayoyafanya hadharani. Na Allah ni Mjuzi sana wa yaliyomo vifuani



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 5

أَلَمۡ يَأۡتِكُمۡ نَبَؤُاْ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِن قَبۡلُ فَذَاقُواْ وَبَالَ أَمۡرِهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Je, haijakufikieni habari ya wale waliokufuru kabla wakaonja matokeo mabaya ya jambo lao (uovu wa ukafiri)? Na (bila ya shaka yoyote) watapata adhabu iumizayo sana



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 6

ذَٰلِكَ بِأَنَّهُۥ كَانَت تَّأۡتِيهِمۡ رُسُلُهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَقَالُوٓاْ أَبَشَرٞ يَهۡدُونَنَا فَكَفَرُواْ وَتَوَلَّواْۖ وَّٱسۡتَغۡنَى ٱللَّهُۚ وَٱللَّهُ غَنِيٌّ حَمِيدٞ

Hayo ni kwa sababu ilikuwa wakiwafikia Mitume wao kwa hoja zilizo wazi, lakini walisema: Ah! Hivi binaadamu ndio watuongoze? Basi walikufuru na wakakengeuka; na Allah Akawa hana haja nao. Na Allah ni Mkwasi (si mhitaji), ni Mwenye kusifiwa



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 7

زَعَمَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَن لَّن يُبۡعَثُواْۚ قُلۡ بَلَىٰ وَرَبِّي لَتُبۡعَثُنَّ ثُمَّ لَتُنَبَّؤُنَّ بِمَا عَمِلۡتُمۡۚ وَذَٰلِكَ عَلَى ٱللَّهِ يَسِيرٞ

Waliokufuru wamedai kwamba hawatofufuliwa kamwe. Sema: Bali hapana! Naapa Kwa Mola wangu, bila shaka mtafufuliwa, kisha mtajulishwa Kwa yale mliyoyatenda, na hayo kwa Allah ni mepesi



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 8

فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِۦ وَٱلنُّورِ ٱلَّذِيٓ أَنزَلۡنَاۚ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Basi muaminini Allah na Mtume Wake na Nuru (Qurani) Tuliyoiteremsha, na Allah anazo khabari za mnayo yatenda



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 9

يَوۡمَ يَجۡمَعُكُمۡ لِيَوۡمِ ٱلۡجَمۡعِۖ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلتَّغَابُنِۗ وَمَن يُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ وَيَعۡمَلۡ صَٰلِحٗا يُكَفِّرۡ عَنۡهُ سَيِّـَٔاتِهِۦ وَيُدۡخِلۡهُ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Siku Atakayokukusanyeni kwaajili ya Siku ya mkusanyiko. Hiyo ndio Siku ya kupata na kukosa. Basi yeyote anayemuamini Allah na akatenda mema (Allah) Atamfutia maovu yake na Atamuingiza katika Mabustani yapitayo chini yake mito, watadumu humo milele. Huko ndiko kufuzu kukubwa



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 10

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَكَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ خَٰلِدِينَ فِيهَاۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Na wale waliokufuru na wakakadhibisha Aya (na ishara, dalili) Zetu hao ndio watu wa motoni, watadumu humo milele. Na hayo ndiyo mafikio mabaya



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 11

مَآ أَصَابَ مِن مُّصِيبَةٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ وَمَن يُؤۡمِنۢ بِٱللَّهِ يَهۡدِ قَلۡبَهُۥۚ وَٱللَّهُ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Haufiki msiba wowote ila kwa idhini ya Allah. Na mwenye kumuamini Allah huuongoa moyo wake. Na Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 12

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَإِنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah, na mt’iini Mtume. Mkigeuka, basi hakika juu ya Mtume wetu ni kufikisha (Ujumbe wake) kwa uwazi tu



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 13

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۚ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ

Allah, hapana Mungu wa Kuabudiwa kwa haki ila Yeye tu. Na juu ya Allah pekee nawategemee Waumini



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 14

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُوٓاْ إِنَّ مِنۡ أَزۡوَٰجِكُمۡ وَأَوۡلَٰدِكُمۡ عَدُوّٗا لَّكُمۡ فَٱحۡذَرُوهُمۡۚ وَإِن تَعۡفُواْ وَتَصۡفَحُواْ وَتَغۡفِرُواْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ

Enyi walioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu ni maadui kwenu, basi tahadharini nao. Na mkisamehe na mkapuuza na mkayafutilia mbali, basi hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwenye kurehemu



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 15

إِنَّمَآ أَمۡوَٰلُكُمۡ وَأَوۡلَٰدُكُمۡ فِتۡنَةٞۚ وَٱللَّهُ عِندَهُۥٓ أَجۡرٌ عَظِيمٞ

Hakika Mali zenu na watoto wenu ni jaribio. Na Kwa Allah upo ujira mkubwa



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 16

فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ مَا ٱسۡتَطَعۡتُمۡ وَٱسۡمَعُواْ وَأَطِيعُواْ وَأَنفِقُواْ خَيۡرٗا لِّأَنفُسِكُمۡۗ وَمَن يُوقَ شُحَّ نَفۡسِهِۦ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Basi mcheni Allah muwezavyo, na sikilizeni; na tiini na toeni (kwa ajili ya Allah) itakuwa kheri kwa ajili ya nafsi zenu. Na yeyote anayeepushwa na ubakhili (tamaa ya uchu wa nafsi yake), basi hao ndio wenye kufaulu (kufanikiwa)



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 17

إِن تُقۡرِضُواْ ٱللَّهَ قَرۡضًا حَسَنٗا يُضَٰعِفۡهُ لَكُمۡ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡۚ وَٱللَّهُ شَكُورٌ حَلِيمٌ

Mkimkopesha Mwenyezi Mungu mkopo mzuri, atakuzidishieni maradufu, na atakusameheni. Na Allah ni Mwenye kupokea shukurani, Mpole, (Mvumilivu)



Sure: ATTAGHAABUN 

Vers : 18

عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Mwenye kujua ghaibi (siri) na dhahiri, Mwenye nguvu, Mwenye hekima