Sure: ANNAJMI 

Vers : 1

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Nina apa kwa nyota zinapozama



Sure: ANNAJMI 

Vers : 2

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Hakupotoka swahibu wenu na wala hakupotoka



Sure: ANNAJMI 

Vers : 3

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Na hasemi (neno lolote lile) kwa utashi wa nafsi (yake)



Sure: ANNAJMI 

Vers : 4

إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa hayo (anayaoyasema) isipokuwa tu ni Wahy unaofunuliwa



Sure: ANNAJMI 

Vers : 5

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha (Malaika Jibrili) Mwenye nguvu kubwa



Sure: ANNAJMI 

Vers : 6

ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye nguvu na hekima na akakaa katika umbile lake halisi



Sure: ANNAJMI 

Vers : 7

وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa katika upeo wa macho



Sure: ANNAJMI 

Vers : 8

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakurubia na akashuka



Sure: ANNAJMI 

Vers : 9

فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Kisha akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi



Sure: ANNAJMI 

Vers : 10

فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

(Allah) Akamfunulia Wahy mja Wake yale Aliyomfunulia Wahy



Sure: ANNAJMI 

Vers : 11

مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Moyo (wake) haukukadhibisha yale aliyoyaona



Sure: ANNAJMI 

Vers : 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnambishia kuhusu yale aliyoyaona?



Sure: ANNAJMI 

Vers : 13

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na hakika alimuona (Jibriyl) kwa mara nyingine



Sure: ANNAJMI 

Vers : 14

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa



Sure: ANNAJMI 

Vers : 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake kuna Jannatu Al-Ma-waa



Sure: ANNAJMI 

Vers : 16

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Ulipoufunika mkunazi huo hicho kilicho ufinika



Sure: ANNAJMI 

Vers : 17

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho lake halikukengeuka wala halikupindukia mipaka



Sure: ANNAJMI 

Vers : 18

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona miongoni mwa Aayaat (ishara, dalili) za Bwana wake kubwa kabisa



Sure: ANNAJMI 

Vers : 19

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmeona (masanamu) Laata na ‘Uzzaa?



Sure: ANNAJMI 

Vers : 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaata mwengine wa tatu?



Sure: ANNAJMI 

Vers : 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?



Sure: ANNAJMI 

Vers : 22

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo basi ni mgao wa dhulma!



Sure: ANNAJMI 

Vers : 23

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Bwana wao mwongozo



Sure: ANNAJMI 

Vers : 24

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Kwani kila Mtu anapata kila anayoyatamani?



Sure: ANNAJMI 

Vers : 25

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Na Allah ndiye mmiliki wa Akhera na Dunia



Sure: ANNAJMI 

Vers : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



Sure: ANNAJMI 

Vers : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



Sure: ANNAJMI 

Vers : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



Sure: ANNAJMI 

Vers : 29

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi achana naye ambaye ameupa mgongo ukumbusho Wetu na wala hataki isipokuwa maisha ya dunia



Sure: ANNAJMI 

Vers : 30

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio upeo wao wa elimu. Hakika Bwana wako ni Mjuzi zaidi wa ambaye amepotoka njia Yake, Naye Mjuzi zaidi wa ambaye ameongoka