Sure: ATTUR 

Vers : 1

وَٱلطُّورِ

Nina apa kwa mlima wa Tur



Sure: ATTUR 

Vers : 2

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa kitabu kilichoandikwa



Sure: ATTUR 

Vers : 3

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika karatasi ya ngozi nyembamba iliyokunjuliwa



Sure: ATTUR 

Vers : 4

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na (nina apa) kwa Nyumba iliyoimarishwa (iliyojengwa imara)



Sure: ATTUR 

Vers : 5

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na (nina apa) kwa sakafu (za mbingu) zilizonyanyuliwa



Sure: ATTUR 

Vers : 6

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na (nina apa) kwa bahari yenye kuwashwa moto)



Sure: ATTUR 

Vers : 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

(Nina apa kwamba) Hakika, adhabu ya Mola wako Mlezi bila ya shaka yoyote itatokea



Sure: ATTUR 

Vers : 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia



Sure: ATTUR 

Vers : 9

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku hiyo mbingu itatikisika kutikisika kikweli



Sure: ATTUR 

Vers : 10

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na majabali yatatembea mwendo wa kasi



Sure: ATTUR 

Vers : 11

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao Siku hiyo kwa wakadhibishao



Sure: ATTUR 

Vers : 12

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wamo katika kushughulika na upuuzi wakicheza



Sure: ATTUR 

Vers : 13

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watasukumwa katika Moto wa Jahannam kwa msukumo wa nguvu



Sure: ATTUR 

Vers : 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Huu ndio ule moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha



Sure: ATTUR 

Vers : 15

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, hivi ni uchawi huu au nyinyi hamuoni?



Sure: ATTUR 

Vers : 16

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Ingieni muungue humo kwenye Jahannam, mkistahamili au msistahamili ni sawasawa kwenu, hakika hapana ila mnalipwa yale mliyokuwa mkiyatenda



Sure: ATTUR 

Vers : 17

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema



Sure: ATTUR 

Vers : 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahia kwa ambayo Amewapa Mola wao, na Akawaokoa na adhabu ya moto uwakao vikali mno



Sure: ATTUR 

Vers : 19

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kwa sababu ya mliyokuwa mnatenda



Sure: ATTUR 

Vers : 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hali ya kuegemea juu ya makochi ya fakhari yaliyopangwa safu safu, na Tutawaozesha huwr ‘ayn, (wanawake weupe) wazuri wenye macho makubwa ya kupendeza



Sure: ATTUR 

Vers : 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na wakafuatwa na dhuriya wao kwa Imani Tutawakutanisha nao dhuriya wao na Hatutawapunguzia katika ‘amali zao kitu chochote. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma



Sure: ATTUR 

Vers : 22

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na Tutawapa matunda na nyama katika ambavyo wanatamani



Sure: ATTUR 

Vers : 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watabadilishana humo gilasi za mvinyo usiosababisha maneno ya upuuzi na wala ya dhambi



Sure: ATTUR 

Vers : 24

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Na watawazungukia watumishi vijana kwa ajili yao kana kwamba ni lulu zilizohifadhiwa



Sure: ATTUR 

Vers : 25

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengine wakiulizana



Sure: ATTUR 

Vers : 26

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Watasema hakika sisi tulikua kabla ya hapa kwa watu wetu wenye kuwafanyia upole



Sure: ATTUR 

Vers : 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Allah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya mvuke wa moto (unaobabua)



Sure: ATTUR 

Vers : 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi tulikuwa tunamuabudu kabla ya hapa hakika yeye ni mwema mwingi wa rehma



Sure: ATTUR 

Vers : 29

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha (Ewe Muhammad) na haukua wewe kwa neema ya mola wako mlezi kuhani wala mwendawazimu



Sure: ATTUR 

Vers : 30

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema (huyu Muhammad þ ni) mshairi, tunamtarajia kupatikana maafa ya dahari