Sure: YAASIIN 

Vers : 1

يسٓ

Yaasiin



Sure: YAASIIN 

Vers : 2

وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡحَكِيمِ

Nina apa kwa Qur’ani yenye hekima (nyingi)



Sure: YAASIIN 

Vers : 3

إِنَّكَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

(Kwamba) Hakika kabisa, wewe ni miongoni mwa Mitume



Sure: YAASIIN 

Vers : 4

عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

(Uko) Juu ya njia iliyo nyooka



Sure: YAASIIN 

Vers : 5

تَنزِيلَ ٱلۡعَزِيزِ ٱلرَّحِيمِ

(Ni) Uteremsho wa (Allah) Mwenye nguvu kubwa, Mwenye kurehemu sana



Sure: YAASIIN 

Vers : 6

لِتُنذِرَ قَوۡمٗا مَّآ أُنذِرَ ءَابَآؤُهُمۡ فَهُمۡ غَٰفِلُونَ

(Wewe ni Mtume uliyetumwa) Ili uwaonye watu ambao baba zao hawakuonywa, na kwa hiyo basi wao wamekuwa wenye kughafilika



Sure: YAASIIN 

Vers : 7

لَقَدۡ حَقَّ ٱلۡقَوۡلُ عَلَىٰٓ أَكۡثَرِهِمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Bila ya shaka yoyote, kauli imekwisha thibiti juu ya wengi wao sana, kwa hivyo hawaamini



Sure: YAASIIN 

Vers : 8

إِنَّا جَعَلۡنَا فِيٓ أَعۡنَٰقِهِمۡ أَغۡلَٰلٗا فَهِيَ إِلَى ٱلۡأَذۡقَانِ فَهُم مُّقۡمَحُونَ

Tumeweka makongwa shingoni mwao, yakawafika videvuni. Kwa hivyo vichwa vyao viko juu tu



Sure: YAASIIN 

Vers : 9

وَجَعَلۡنَا مِنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ سَدّٗا وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ سَدّٗا فَأَغۡشَيۡنَٰهُمۡ فَهُمۡ لَا يُبۡصِرُونَ

Tumeweka kizuizi mbele yao, na kizuizi nyuma yao, na tumewafunika macho yao; kwa hivyo hawaoni



Sure: YAASIIN 

Vers : 10

وَسَوَآءٌ عَلَيۡهِمۡ ءَأَنذَرۡتَهُمۡ أَمۡ لَمۡ تُنذِرۡهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Ni sawa sawa kwao ukiwaonya au usiwaonye, hawataamini



Sure: YAASIIN 

Vers : 11

إِنَّمَا تُنذِرُ مَنِ ٱتَّبَعَ ٱلذِّكۡرَ وَخَشِيَ ٱلرَّحۡمَٰنَ بِٱلۡغَيۡبِۖ فَبَشِّرۡهُ بِمَغۡفِرَةٖ وَأَجۡرٖ كَرِيمٍ

Hakika wewe unamuonya mwenye kufuata ukumbusho, na akamcha Arrahman, Mwingi wa Rehema, kwa ghaibu. Basi mbashirie huyo msamaha na ujira mwema



Sure: YAASIIN 

Vers : 12

إِنَّا نَحۡنُ نُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَنَكۡتُبُ مَا قَدَّمُواْ وَءَاثَٰرَهُمۡۚ وَكُلَّ شَيۡءٍ أَحۡصَيۡنَٰهُ فِيٓ إِمَامٖ مُّبِينٖ

Hakika Sisi tunawafufua wafu, na tunayaandika wanayo yatanguliza, na wanayo yaacha nyuma. Na kila kitu tumekihifadhi katika daftari asli lenye kubainisha



Sure: YAASIIN 

Vers : 13

وَٱضۡرِبۡ لَهُم مَّثَلًا أَصۡحَٰبَ ٱلۡقَرۡيَةِ إِذۡ جَآءَهَا ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Na wapigie mfano wa wakaazi wa mji walipo wafikia waliotumwa



Sure: YAASIIN 

Vers : 14

إِذۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَيۡهِمُ ٱثۡنَيۡنِ فَكَذَّبُوهُمَا فَعَزَّزۡنَا بِثَالِثٖ فَقَالُوٓاْ إِنَّآ إِلَيۡكُم مُّرۡسَلُونَ

Tulipo watumia wawili, wakawakanusha. Basi tukawazi-dishia nguvu kwa mwingine wa tatu. Wakasema: Hakika sisi tumetumwa kwenu



Sure: YAASIIN 

Vers : 15

قَالُواْ مَآ أَنتُمۡ إِلَّا بَشَرٞ مِّثۡلُنَا وَمَآ أَنزَلَ ٱلرَّحۡمَٰنُ مِن شَيۡءٍ إِنۡ أَنتُمۡ إِلَّا تَكۡذِبُونَ

Wakasema: Nyinyi si chochote ila ni watu kama sisi. Na Mwingi wa Rehema hakuteremsha kitu. Nyinyi mnasema uwongo tu!



Sure: YAASIIN 

Vers : 16

قَالُواْ رَبُّنَا يَعۡلَمُ إِنَّآ إِلَيۡكُمۡ لَمُرۡسَلُونَ

Wakasema: Mola wetu Mlezi anajua kwamba hakika sisi tumetumwa kwenu



Sure: YAASIIN 

Vers : 17

وَمَا عَلَيۡنَآ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Wala si juu yetu ila kufikisha ujumbe ulio wazi



Sure: YAASIIN 

Vers : 18

قَالُوٓاْ إِنَّا تَطَيَّرۡنَا بِكُمۡۖ لَئِن لَّمۡ تَنتَهُواْ لَنَرۡجُمَنَّكُمۡ وَلَيَمَسَّنَّكُم مِّنَّا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Wakasema: Sisi tumeagua kuwa nyinyi ni wakorofi. Ikiwa hamtaacha basi kwa yakini tutakupigeni mawe, na mtapata adhabu chungu kutoka kwetu



Sure: YAASIIN 

Vers : 19

قَالُواْ طَـٰٓئِرُكُم مَّعَكُمۡ أَئِن ذُكِّرۡتُمۚ بَلۡ أَنتُمۡ قَوۡمٞ مُّسۡرِفُونَ

Wakasema: Ukorofi wenu mnao wenyewe! Je! Ni kwa kuwa mnakumbushwa? Ama nyinyi ni watu walio pindukia mipaka



Sure: YAASIIN 

Vers : 20

وَجَآءَ مِنۡ أَقۡصَا ٱلۡمَدِينَةِ رَجُلٞ يَسۡعَىٰ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱتَّبِعُواْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na akaja mtu mbio kutokea upande wa mbali wa mjini, akasema: Enyi watu wangu! Wafuateni hawa walio tumwa



Sure: YAASIIN 

Vers : 21

ٱتَّبِعُواْ مَن لَّا يَسۡـَٔلُكُمۡ أَجۡرٗا وَهُم مُّهۡتَدُونَ

Wafuateni ambao hawakutakini ujira, hali yakuwa wenyewe wameongoka



Sure: YAASIIN 

Vers : 22

وَمَالِيَ لَآ أَعۡبُدُ ٱلَّذِي فَطَرَنِي وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Na kwanini nisimuabudu yule aliye niumba na kwake mtarejeshwa?



Sure: YAASIIN 

Vers : 23

ءَأَتَّخِذُ مِن دُونِهِۦٓ ءَالِهَةً إِن يُرِدۡنِ ٱلرَّحۡمَٰنُ بِضُرّٖ لَّا تُغۡنِ عَنِّي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا يُنقِذُونِ

Je! Niishike miungu mingine badala yake? Arrahmani, Mwingi wa Rehema, akinitakia madhara uombezi wa hao hautanifaa kitu, wala hawataniokoa



Sure: YAASIIN 

Vers : 24

إِنِّيٓ إِذٗا لَّفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

Basi hakika mimi hapo nitakuwa katika upotovu ulio dhaahiri



Sure: YAASIIN 

Vers : 25

إِنِّيٓ ءَامَنتُ بِرَبِّكُمۡ فَٱسۡمَعُونِ

Hakika mimi nimemuamini Mola wenu Mlezi, basi nisikilizeni!



Sure: YAASIIN 

Vers : 26

قِيلَ ٱدۡخُلِ ٱلۡجَنَّةَۖ قَالَ يَٰلَيۡتَ قَوۡمِي يَعۡلَمُونَ

Akaambiwa: Ingia Peponi! Akasema: Laiti kuwa watu wangu wangeli jua



Sure: YAASIIN 

Vers : 27

بِمَا غَفَرَ لِي رَبِّي وَجَعَلَنِي مِنَ ٱلۡمُكۡرَمِينَ

Jinsi Mola wangu Mlezi alivyo nisamehe, na akanifanya miongoni mwa walio heshimiwa



Sure: YAASIIN 

Vers : 28

۞وَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَىٰ قَوۡمِهِۦ مِنۢ بَعۡدِهِۦ مِن جُندٖ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ وَمَا كُنَّا مُنزِلِينَ

Na hatukuwateremshia kaumu yake baada yake jeshi kutoka mbinguni, wala si wenye kuteremsha



Sure: YAASIIN 

Vers : 29

إِن كَانَتۡ إِلَّا صَيۡحَةٗ وَٰحِدَةٗ فَإِذَا هُمۡ خَٰمِدُونَ

Hakukuwa ila ukelele mmoja tu; na mara walizimwa!



Sure: YAASIIN 

Vers : 30

يَٰحَسۡرَةً عَلَى ٱلۡعِبَادِۚ مَا يَأۡتِيهِم مِّن رَّسُولٍ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Nawasikitikia waja wangu. Hawajii Mtume ila wao humkejeli