Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 1

وَٱلۡعَٰدِيَٰتِ ضَبۡحٗا

Naapa kwa farasi wendao mbio wakipumua,



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 2

فَٱلۡمُورِيَٰتِ قَدۡحٗا

Na wakitoa moto kwa kupiga kwato zao chini,



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 3

فَٱلۡمُغِيرَٰتِ صُبۡحٗا

Wakishambulia wakati wa asubuhi,



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 4

فَأَثَرۡنَ بِهِۦ نَقۡعٗا

Huku wakitimua vumbi,



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 5

فَوَسَطۡنَ بِهِۦ جَمۡعًا

Na wakijitoma kati ya kundi,



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 6

إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لِرَبِّهِۦ لَكَنُودٞ

Hakika mwanaadamu ni mtovu wa fadhila kwa Mola wake Mlezi!



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 7

وَإِنَّهُۥ عَلَىٰ ذَٰلِكَ لَشَهِيدٞ

Na hakika yeye mwenyewe bila ya shaka ni shahidi wa hayo!



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 8

وَإِنَّهُۥ لِحُبِّ ٱلۡخَيۡرِ لَشَدِيدٌ

Naye hakika bila ya shaka anapenda sana (kheri) mali!



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 9

۞أَفَلَا يَعۡلَمُ إِذَا بُعۡثِرَ مَا فِي ٱلۡقُبُورِ

Kwani hajui watakapo fufuliwa waliomo makaburini?



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 10

وَحُصِّلَ مَا فِي ٱلصُّدُورِ

Na yakakusanywa yaliyomo vifuani?



Sure: AL-AADIYAAT 

Vers : 11

إِنَّ رَبَّهُم بِهِمۡ يَوۡمَئِذٖ لَّخَبِيرُۢ

Kwa hakika Mola wao Mlezi siku hiyo bila ya shaka atakuwa na khabari zao wote!