Sure: MARYAM 

Vers : 91

أَن دَعَوۡاْ لِلرَّحۡمَٰنِ وَلَدٗا

Kwa kudai kwao kuwa (Allah) Mwingi wa Rehema ana mtoto



Sure: MARYAM 

Vers : 92

وَمَا يَنۢبَغِي لِلرَّحۡمَٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا

Na haitakiwi kwa (Allah) Mwingi wa Rehema kuwa na mtoto.[1]


1- - Aya hizi tano 88, 89, 90, 91 na 92 zinakataa kwa ukali itikadi kwamba Mungu ana mtoto. Muislamu hatakiwi kabisa kuikumbatia itikadi hii au kuishabikia. Ni itikadi mbaya mno kiasi kwamba mbingu, ardhi na milima haziivumilii kuisikia.


Sure: MARYAM 

Vers : 93

إِن كُلُّ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ إِلَّآ ءَاتِي ٱلرَّحۡمَٰنِ عَبۡدٗا

Hapana yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake



Sure: MARYAM 

Vers : 94

لَّقَدۡ أَحۡصَىٰهُمۡ وَعَدَّهُمۡ عَدّٗا

Yeye hakika amewadhibiti na amewahesabu sawa sawa



Sure: MARYAM 

Vers : 95

وَكُلُّهُمۡ ءَاتِيهِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَرۡدًا

Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake



Sure: MARYAM 

Vers : 96

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَيَجۡعَلُ لَهُمُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وُدّٗا

Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi



Sure: MARYAM 

Vers : 97

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ ٱلۡمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِۦ قَوۡمٗا لُّدّٗا

Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur’ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wacha Mungu, na uwaonye kwayo watu wabishi



Sure: MARYAM 

Vers : 98

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هَلۡ تُحِسُّ مِنۡهُم مِّنۡ أَحَدٍ أَوۡ تَسۡمَعُ لَهُمۡ رِكۡزَۢا

Na kaumu ngapi tuziangamiza kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao